Lindi na Mtwara wameshalipiza kisasi

Lindi na Mtwara wameshalipiza kisasi

mimi nilikua mtwara nimeondoka leo
ngoja nikuulize kitu,sehemu ambayo wenyeviti wa mtaa ccm walika zaidi ya mia leo wanabaki 53 huo ni ushindi?

Kwenye percentages ama? Sasa 53 ni below 50? Hata dunia inamajira tofauti ndio maana hata matukio yanakuja tofauti. Haiwezi kuwa kila siku mambo yale yale ila kushindwa ni kushindwa tu hakuna mjadala!
 
huko kusini hayo maisha ndio chaguo lao usiwalazimishe kukimbizana na maendeleo
 
ImageUploadedByJamiiForums1418678797.593180.jpg
Ni dharau kias gan mtu kuweka pic ya chama choon choo chenyewe cha shimo
 
Jamiiforums kama facebook tu siku hizi ni Kigenge cha jobless kabisa , watu wanaandika mipasho kama watoto wa kike. Utaongeaje bila data subir matokeo yatoke tuone hitimisho lako. Na matokeo yakikamilika wanaoongea kitu cha maana ni kina Pasco tu humu ndio ambao unaweza angalau kusoma mabandiko yao hapa, ila waliobaki vilaza wanaandika ujinga tu hapa, hayo mahaba yao sijui hata wanayapeleka wapi aisee!

Umeona eenh? Utoto mwingi...
 
Kwa hatua waliyofikia mtwara ni ya kupongezwa, ccm hali yao ni mbaya sana sasa hivi ushindi wao wanautegemea kuupata kwenye mapingamizi tu. Shame on them.
 
vuta nikuvute ukisema lindi na mtwara wamelipiza kisasi utasemaje dodoma ambako tumezoa kura na arusha tumewapoka Chadema baadhi ya viti na manyara na kwingineko kwiingi ambako tumeshinda kwa kishindo??? wale wana mtwara ni cuf asilia ndio maana chadema hawatii pua pale na nikuhakikishie tu kuwa mwakani utashika mdomo kwa sapraizi ya mwak kwani hawahawa unaodai wamelipiza kisasi ndio hawahawa watakaowageuka na kutupigia sisi kura

Hivi wewe unajielewa kweli? Arusha mmewapoka chadema viti gani?
Kukusaidia ni kuwa Arusha chadema walikuwa na viti 7 tu kabla ya uchaguzi huu.
 
Hajawahi na hatawahi kuwa mwanaCCM kwa sababu tunafahamu vizuri sana ID iliyoko nyuma ya VUTA-NKUVUTE.

Huyu ni kijana wa BAVICHA ambaye anatokea mkoa wa Pwani na ana shahada ya sheria kutoka UDSM.

Unaweza ukaendelea kuamini unavyoamini lakini mwenye macho haambiwi tazama!

Mkuu, Poleni sana. Ndio demokrasia hiyo...Jitahidini 2019 inshallah mtaweza kurejesha vijiji na kata zota
 
Kwani nchi hii mbona umaskini huko mikoa mingi tuu? shinyanga ,Singida!....
Mtwara Matokeo!

CCM wameshinda mitaa 58
Wapinzani mitaa 53!

ikumbukwe kwamba Mitaa 100 CCM walipita bila kupingwa!

Kama mlitumia kigezo cha umaskini kutaka kuwadanya watakuwa wamewashitukia maana nchi hii umaskini huko mikoa mingi kwanza sasa hivi Mtwara kuna maendeleo sana!

Poleni sana
haa haa, mkuu kama umasikini uko mikoa mingi, kwa nini tuendelee kubaki na ccm? Ccm must go, imechoka.
 
Kukumbatia CCM ni kukumbatia umasikini. Nyie wazee na wakina mama achaneni na liccm
 
Mimi binafsi ngoja nisubiri matokeo rasmi, siamini watu humu! Jana usiku kwa mfano arusha, watu walikuwa ni "eh chadema kachukua huku, Nasari anatisha kabeba arusha yote" leo nasikia matangazo, ccm imeshinda Arusha!! Ngoja ningoje tu matokeo rasmi, naona huku kuna ushabiki tu wa mahaba!
katika mitaa 155 ya jiji la arusha Cdm wameshinda mitaa 110 na ccm mitaa 43, mitaa mi2 uchaguzi unafanyika leo! Utake usitake habari ndo hiyo!
 
Kwa ccm na serikali yake waliyoyatenda mtwara hawakupaswa kupewa hata mtaa mmoja! Ccm wanapaswa kufutwa kabisa mtwara na tanzania kiujumla.
 
Suala la Umaskini kwa Mtwara siyo kweli kabisa. Ni wilaya ya Mtwara Rural tu ndo umaskini unaonekana, lakini kitaifa Mrwara haipo katika mikoa maskini.

Tuje kwenye uchaguz, bado matokeo kule ni 50/50. Kule Msimbat ambako ni chimbuko la ges ya asili CCM kuna mitaa ilipata kura0. Na kwenye ushindani lazima kila mrengo upate kura. Kama Arusha bado kwa uchaguz huu wa vitongoji kwa mujibu wa Dira ya Dunia BBC jana Cdm na CCm bado ilikuwa ni 50-50 ambayo ni good move bado. Cha msingi somo la elimu ya uraia na kujitambua lisiishie wakati huu tu. Liendelezwe kwa katiba inayopendekezwa na uchaguzi mkuu 2015, na opposition ikiweka malengo na kupata wabunge 180-200, hata kama wasishinde urais; nchi itanyooka tu kwa kuwa maamuz ya NDiyooo Bungeni hayatakuwepo. Ndiyooo yamesababisha mambo mengi ya ovyo kupita ambayo hayana tija kwa Taifa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom