Lindi na Mtwara wameshalipiza kisasi

Lindi na Mtwara wameshalipiza kisasi

Taratibu ila kwa uhakika...hakuna lisilo na mwisho,hii ni ishara kabisa ya mwisho kuwa ccm imekufa..
 
msimbati ndiko wamefunga kazi moja kwa moja

wamepiga chini ccm mazima,,

shenzy type panapo uhai tutakutana mwakani

eti wanakuja na gia ya kujifanya wanamalizia bara bara ya nangurukuru haisaidii hiyo.

Leteni wanajeshi wapige kura sasa

lazima tuwafunze adabu safari hii

woyoooooooo
 
Jamani hiki ni KIAMA. GEITA YOTE IMEPIGWA. UKAWA KIDEDEA KWA 97%
 
Tunasubiri Nape atoe statement kuwa ccm imepoteza vitongoji vingapi
Sasa hivi wanangoja kuja na majumuisho kuonyesha kwamba kati ya vijiji 5000 wao wamepata vijiji 3500 kwahiyo wamepata ushindi wa kishindo.

Ukiwauliza walikuwa na vijiji vingapi 2009, watakwambia hiyo sio hoja, hoja wameshinda kwa asilimia 80.

Ndio maana huwaoni wakina Msalani humu jukwaani. wanaandaa press release za ushindi.
 
Tuliwaambia Lumumba kwamba chama cha siasa si majengo bali ni kukubalika kwa sera za chama husika kwa wananchi - wakatubishia, tena wakatubeza na kuendelea na tabia yao ya somba-somba watu kwa malori na mabasi kwenda kwenye mikutano yao huku wakigawa fulana, kofia na wali - pamoja na burudani kede kede toka kwa wasanii maarufu eti hiyo ndiyo njia yao ya kuzinadi sera zao.

Sasa ngoja tuone mwenezi wao atakuja na PAUKWA gani kuhusu pigo hili la uchaguzi.

Wao hawajui kitu cha muhimu kwa binadamu sio kumpa samaki (majengo) bali kumfundisha namna ya kuvua samaki (elimu ya uraia). Wanaishi kwa mazoea na hayo majengo (maofisi) mengi yalijengwa wakati wa baba wa taifa tena kwa nguvu ya umma leo wameyafanya vijiwe vya fitina, majungu, na kuendekeza ushirikina. Hawana tofauti na wazee wa timu za Yanga na simba wasio na miradi ya kueleweka bali kusubiri kuchuma kwenye timu hizo tu. Ni nani asiyeona jinsi viongozi wengi wa ccm wa sasa wasivyoweza kujenga hoja mbele ya jamii zaidi ya kusubiri kwenda kwenye matamasha kama wageni rasmi na kuishia kutoa hutuba zisizo na hata chembe ya swali?

Baada ya uchaguzi wa 2010 ccm kupita kwa nguvu ya jeshi na tume ya uchaguzi waliamua kuleta watu wakupambana mitandaoni tena kwa wazo toka kwa vijana wa ccm akina Mwigulu na Nape, ajabu na kweli hoja walizokuja nazo sio za maendeleo bali ni Slaa kapora mke wa mtu, Mbowe ni mchaga, Zitto anachukiwa kwakuwa sio mkristo/mchaga. Hivi kweli kwa hoja za namna hii unategemea chama kilete maendeleo. Kama ninayosema ni uwongo niambieni siku Msalani, Ifweero, Lizaboni wameleta wazo lenye maana kwa watanzania hapa jukwaani. Kwa chama kikubwa na kikongwe kama ccm ulitegemea walete watu kupambana mitandaoni kwa ujengaji hoja ule? Kituko cha mwaka hata wabunge na viongozi wengi wa ccm wakichangia bungeni na mitaani unaona kabisa wanachongea ni kile kile wanachoongea akina Lizaboni, Ifweero and co. Ukiangalia mawazo hayo ya akina Nape, Mwigulu na January yalikubaliwa na viongozi wazee wa chama chao kwani walidhani hivyo ndio vitu vijana wanapenda. Na kwamba eti akina Mwigulu na kundi lake ndio think tank ya chama chao na huku wakiwadaganya wazee hao ili wawape hela za kifasadi kwa kuwaokoa na dhoruba ya mabadiliko na kuwaepusha na maisha ya jela kwa yale waliyoifanyia nchi hii kupitia mikataba ya kifasadi. Matunda ya vijana wa ccm kuwapotosha wazee wa ccm pia yalionekana wakati wa bunge la katiba kupitia P. Makonda mpaka kufikia kupewa nafasi na S. 6 eti kuwakilisha vijana wa jf. Lakini kwa jinsi vijana walivyomkana kila mtu alijionea hapa jukwaani. Na waliomuunga mkono ni walewale wanaongoza kwa hoja za kipuuzi akina Lizaboni, Ifweero, Msalani nk. Kwa ccm hiyo unategemea jeshi la polisi linalonukwa rushwa kutokutumika vibaya kuzuia mabadiliko?
 
Arusha ni soo..... mtaani kwetu ccmscrow chini, Urassa wa CHADEMA kachukua.

Bandu bandu humaliza gogo....
 
Sasa hivi wanangoja kuja na majumuisho kuonyesha kwamba kati ya vijiji 5000 wao wamepata vijiji 3500 kwahiyo wamepata ushindi wa kishindo.

Ukiwauliza walikuwa na vijiji vingapi 2009, watakwambia hiyo sio hoja, hoja wameshinda kwa asilimia 80.

Ndio maana huwaoni wakina Msalani humu jukwaani. wanaandaa press release za ushindi.


Ndugu yangu umekosea akina Msalani, Lizaboni leo wako humu jukwaani lakini kwa id mpya tu, angalia kuna id mpya zimefunguliwa leo lakini maudhui ya uchangiaji wao ni uleule wa akina msalani. Kila nikiwaona leo humu jukwaani nawaambie wachukue hela za mwisho mwisho na wakafungue shughuli halali kwani umri unazidi kuwatupa mkono na chama ndio hivyo kinaelekea kupoteza dola. Leo hili power ya propangada ya chopa tatu kata tatu haipo kwani daftari lilotumika safari hii sio lile chovu ambalo hata tume inakiri limechezewa. NI jipya japo liliandikishwa kwa hila ya muda mfupi lakini wangalau vijana wamejitambua na kutekeleza wajibu wao. Ukweli huu wameuona na leo wako kwenye kikao cha ndani wanakaririshwa propaganda za kizee toka nchi za ulaya mashariki tayari kwa kuja kujibu mashambulizi hapa jukwaani. Ngoja matokeo rasmi yatoke utawaona hapa wakija kifua mbele na hoja za kizee.

Ila ukweli ulieendee jeshi la polisi kwani limekuwa ni mpiga kura wa uhakika toka chama cha mapinduzi na tegemeo pekee la kuleta machafuko nchini ili ccm wangalau ilazimishe serekali ya umoja wa kitaifa. Naomba tuendelee kuhimiza vijana kujiandikisha na kupiga kura uchaguzi mkuu ujao wangalau upinzani ushinde viti vingi vya ubunge mbona mwizi wetu tutakuwa tumemkamata. Mimi nilihakikisha nimeshwawishi vijana 50 wajiandikishe kupiga kura na jana wamefanya kweli,kwa mara ya kwanza mtaani kwenu uongozi wa cdm umeshinda. Sijitii voucher niliweka kwenye simu kwani vijana hao niliwafuatilia na kuwahiza kama mwalimu mkuu kuhakikisha wanapiga kura. Sisi wapenda mabadiliko wote tukijipa jukumu la kushawishi, kulazimisha wangalau kila mtu watu 100+ kujiandikisha na kupiga kura mbona wangalau 50/50 ya wabunge tunaipata na hapo sheria nyingi zitawekwa sawa.
 
Kuna mtu anaitwa Lizaboni anatumia vibaya ID ya chama , anyang'anywe , nakujulisha wewe kwa vile ID zote za chama pale lumumba ziko chini yako .
 
Tusubiri matokeo kamili. Hizi porojo za Kinondoni tumezichoka sasa

Mnajitokeza kwa kuvizia si mnakuwaga mnadandia nyuzi humu tena mnakuwa wa kwanza mkipokezana upuuzi hahahahahaaaaa leo mnachungulia hahahahahaaaa!!
 
Tuliwaambia Lumumba kwamba chama cha siasa si majengo bali ni kukubalika kwa sera za chama husika kwa wananchi - wakatubishia, tena wakatubeza na kuendelea na tabia yao ya somba-somba watu kwa malori na mabasi kwenda kwenye mikutano yao huku wakigawa fulana, kofia na wali - pamoja na burudani kede kede toka kwa wasanii maarufu eti hiyo ndiyo njia yao ya kuzinadi sera zao.

Sasa ngoja tuone mwenezi wao atakuja na PAUKWA gani kuhusu pigo hili la uchaguzi.


View attachment 211239
 
Huyu jamaa anaeitwa lizaboni Ana roho ya paka. Wenzake wote wamekimbia ff msalani wote siwaoni hapa. Ana roho ngumy Sana huyu jamaa .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom