Mohamed R
JF-Expert Member
- Mar 28, 2013
- 2,232
- 426
Pole kiongozi, binafsi naona ndani ya sisiem umebaki peke yako unaoumizwa na utendaji wa chama chako.
1. Ulikataa kwenda arusha mwaka jana na ulisema kwa nini huendi.
2. Ulisema pia baada ya ziara yako ya nyanda za juu kusini na mitaa hiyo ya Mtwara na Lindi.
Pia mengi tu umekuwa muwazi kulingana na hali halisi.
Lakini kauli za Mwenzio Nape huwa unazisikia? Kejeli zako je? Matusi yake kwa wapinzani na kusema shida za watanzania je? Katembea karibu nchi nzima kwa kodi zetu huku akitutukana. Lini uliwahi kumuona akikubali kuwa hali ni mbaya kwa chama chenu? Juzi wakati anafunga kampeni ulisikia kauli yake?
Ushauri wangu kwako ni kuangalia ustaarabu wa nini cha kufanya, kama unaona gari hiyo ya miaka ya 70 inakusumbua nunua nyingine ya kisasa na hiyo paki mahala au tupa huko iwe screpa.
1. Ulikataa kwenda arusha mwaka jana na ulisema kwa nini huendi.
2. Ulisema pia baada ya ziara yako ya nyanda za juu kusini na mitaa hiyo ya Mtwara na Lindi.
Pia mengi tu umekuwa muwazi kulingana na hali halisi.
Lakini kauli za Mwenzio Nape huwa unazisikia? Kejeli zako je? Matusi yake kwa wapinzani na kusema shida za watanzania je? Katembea karibu nchi nzima kwa kodi zetu huku akitutukana. Lini uliwahi kumuona akikubali kuwa hali ni mbaya kwa chama chenu? Juzi wakati anafunga kampeni ulisikia kauli yake?
Ushauri wangu kwako ni kuangalia ustaarabu wa nini cha kufanya, kama unaona gari hiyo ya miaka ya 70 inakusumbua nunua nyingine ya kisasa na hiyo paki mahala au tupa huko iwe screpa.
Hali ni tete huko Lindi na Mtwara kwa CCM. Matokeo yanayotufikia hapa Ofisi Ndogo za Chama,Lumumba si vutizi. UKAWA wametupoka sehemu nyingi huko.CUF imetamalaki. CUF imetetea mitaa yake na kupoka mingine toka CCM.Wana-Lindi na Mtwara hatimaye wamelipa kisasi na kuonesha kinyongo chao juu ya sakata la gesi asilia.
Kipigo cha gesi kimejibiwa na kipigo cha kura. Sijui mwakani itakuwaje. Wana-Lindi na Mtwara tusameheni jamani.Tuliteleza.Hatutarudia tena.Safari hii mkiliona jeshi huko basi liko Kambini au limekuja kujenga madaraja na miundombinu mingine.
Kujikwaa si kuanguka.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam