Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Wana JF,
Nafikiri kwenye kila madawa kuna madawa makali, ya kati na ya chini. Yote yanakuwa madawa. Sasa katika hayo msemayo, kuna yanayoharibu kweli mtu uwezo wake wa kufikiri na anakuwa zezeta. Kuna yale yanayomfanya kupunguza ukali na kuna mengine ni kuaminishwa tu na mwanamke kwa kufikiri anapendwa, anaacha complex za kijinga na hapo mapenzi yanakolea/
Huko kwetu nilishasikia mifano kadhaa kwenye familia yetu. Mbili ni wanawake walioolewa kwenye familia na hawa walikuwa MBOGO kwa waume zao na cha kutisha walikuwa wakitembeza KIPIGO kwa waume zao. Sasa kwa sababu wanaume nao hawakuwa legelege, kwa kweli mkono ulitembezwa, meno yalirushwa, miiko, vyungu na "MPANTI" , sijui mnaita kibanio kwa kiswahili? ule mti umekaa kama Y ili kudhibiti sufuria au chungu cha ugali. Kesi ya kwanza sijui ila kesi ya pili nakumbuka marehemu baba yangu alihusika katika kutafuta dawa ya kumpoza huyo dada. Hadi leo hii wako pamoja.
Nyingine nilisikia ilikuwa ni kutoka familia ya shemeji yangu. Kwenye familia hiyo, anatoka Mwalimu Juma. Huyu Mzee alikuwa anasifika Tabora kuwa unaweza kumwacha Sikonge na ukaondoka na gari, ukifika Tabora mjini unamkuta anacheza bao. Na wanakuambia kaanza kucheza zamani tu. Katika hiyo familia, kuna jamaa aliolea humo. Ila huyo mke (dada ya shemeji yangu) alikuwa KICHAA/Mbogo sana kwa mumewe. Vurugu, matusi, ngumi nk ikawa kitu cha kawaida. Ndugu zake huyo dada kuona hayo, wakaamua kumfuata shemeji na kumuuliza kama anahitaji msaada. Jamaa akakiri kuwa maji yako shingoni na kibaya ni kuwa anampenda mkewe. Basi Mwalimu Juma alitengeneza dawa na jamaa akapewa ili amuwekee mkewe. Dada yule alituliza hayo maguvu yake na hadi leo wanaishi pamoja.
Nafikiri kila dawa ina ubaya na uzuri wake na inategemea tu unaitumia vipi. Moto, maji, Kisu nk vyote ni vizuri na muhimu kwa binadamu ila ukitumia vibaya, madhara yake .......
Nafikiri kwenye kila madawa kuna madawa makali, ya kati na ya chini. Yote yanakuwa madawa. Sasa katika hayo msemayo, kuna yanayoharibu kweli mtu uwezo wake wa kufikiri na anakuwa zezeta. Kuna yale yanayomfanya kupunguza ukali na kuna mengine ni kuaminishwa tu na mwanamke kwa kufikiri anapendwa, anaacha complex za kijinga na hapo mapenzi yanakolea/
Huko kwetu nilishasikia mifano kadhaa kwenye familia yetu. Mbili ni wanawake walioolewa kwenye familia na hawa walikuwa MBOGO kwa waume zao na cha kutisha walikuwa wakitembeza KIPIGO kwa waume zao. Sasa kwa sababu wanaume nao hawakuwa legelege, kwa kweli mkono ulitembezwa, meno yalirushwa, miiko, vyungu na "MPANTI" , sijui mnaita kibanio kwa kiswahili? ule mti umekaa kama Y ili kudhibiti sufuria au chungu cha ugali. Kesi ya kwanza sijui ila kesi ya pili nakumbuka marehemu baba yangu alihusika katika kutafuta dawa ya kumpoza huyo dada. Hadi leo hii wako pamoja.
Nyingine nilisikia ilikuwa ni kutoka familia ya shemeji yangu. Kwenye familia hiyo, anatoka Mwalimu Juma. Huyu Mzee alikuwa anasifika Tabora kuwa unaweza kumwacha Sikonge na ukaondoka na gari, ukifika Tabora mjini unamkuta anacheza bao. Na wanakuambia kaanza kucheza zamani tu. Katika hiyo familia, kuna jamaa aliolea humo. Ila huyo mke (dada ya shemeji yangu) alikuwa KICHAA/Mbogo sana kwa mumewe. Vurugu, matusi, ngumi nk ikawa kitu cha kawaida. Ndugu zake huyo dada kuona hayo, wakaamua kumfuata shemeji na kumuuliza kama anahitaji msaada. Jamaa akakiri kuwa maji yako shingoni na kibaya ni kuwa anampenda mkewe. Basi Mwalimu Juma alitengeneza dawa na jamaa akapewa ili amuwekee mkewe. Dada yule alituliza hayo maguvu yake na hadi leo wanaishi pamoja.
Nafikiri kila dawa ina ubaya na uzuri wake na inategemea tu unaitumia vipi. Moto, maji, Kisu nk vyote ni vizuri na muhimu kwa binadamu ila ukitumia vibaya, madhara yake .......