Limbwata la gundi na kamba

Limbwata la gundi na kamba

Jamaniiii hili ata kuwa kafanyiwa mtu wangu wa karibu sana! Hasemi kitu kwa mkewe ana achwa nyumbani mke aba rudi usiku wa manane kalewa chakari na ana fungua gate! Ana achiwa mtoto wife ngomani hukooo! Ndugu tume baki kuduwaa! Ukijaribu kuongea ana kukasirikia
Kashawekwa kwenye chungu huyo... Mpelekeni kwenye maombi tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda hata mkurugenzi wa HR department kwenye taasis yangu alimfanyia boss wetu hayo. Yule mdada mzembe, kazi za ofisi yake nyingi haziendi zimelala. Kazi ndogo anaweza kukaa nayo zaidi ya miaka miwili lakini boss anaona sawa. Wakati watu wa idara nyingine anafuatilia sana ufanyaji kazi wao.
 
Ndugu wote wame kaa kando mke kavurugana nao! Je bila kufunguliwa ata kuja kurudi kawaida au ndiyo basi tena? Yaani amekuwa kama ana ogopa ndugu haji hata misibani na cm hapokei! Ni mimi tuu ndiyo naelewana kiasi na huyo bibie! Ila siyo mke wa kwanza alimtoa mwenzie! Kamfanya baba mpka ana mkataa mwanae ambaye ame mkuta huyo mama! Juzi graduu ya mtoto ana maliza chuo mzee hakwenda na cm kazima kabisa! Yaani mambo ni mengi haya ni baadhi!
Hiko kimwanamke kina dhambi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.
Kashawekwa kwenye chungu huyo... Mpelekeni kwenye maombi tu

Sent using Jamii Forums mobile app
downloadfile-18.jpeg


Jr
 
Katika lugha ya kitabibu uchawi huu huwa unajulikana kama “ TEKO “ kwa sababu mtu aliye lishwa uchawi huu anakuwa kama mtu aliye tekwa na mtu mwenye silaha nzito mfano bunduki. Mtu akitekwa kwa bunduki ile bunduki inakuwa sio bunduki tena bali inakuwa “ Remote Control” ambayo kazi yake ni kumcontrol mtekwaji na kumuamuru kufanya anacho kitaka.

Mtu aliye lishwa uchawi huu hufanya kila kitu anacho amriwa kufanya na mtekaji.

Uchawi huu umeharibu maisha ya watu wengi sana. Familia nyingi zime vunjika kwa sababu ya uchawi. Watoto wengi wametelekezwa na kuharibikiwa maisha kwa sababu ya uchawi huu. Kibaya zaidi wahanga wa uchawi huu wanazidi kuongezeka siku hata siku. kuhusu namna ya kujikinga dhidi ya uchawi huu pamoja na kuwazindua watu ambao tayari wamelishwa uchawi huu.



Sent using i phone x
 
Eeeh raha ya mwanaume awe na sauti.... Akiongea mtu ujue Kuna mwanaume anaongea, sio jitu lipo tu kama msukule kila kitu ndio.... Mambo gani haya

Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa Zesh. Familia inayoogozwa na mwanaume ndiyo familia nzuri na inapendeza hata machoni pa jamii.

Hata mama anapata na kufurahia haki yake ya kuwa mama, kama vile kuwatuliza watoto wake watukutu kwa kuwaambia waache utundu mara moja kabla baba yao ajarudi kuwachapa. Siyo baba ndiyo unawaambia hayo watoto eti mama atakuja kuwachapa kisa umepewa limbwata, hii hainogi hata kidogo!!!
 
Nimekuwa nikipokea ujumbe kutoka kwa watu wengi wakiniomba nitoe somo kuhusu namna ya kujikinga dhidi ya uchawi huu pamoja na kuwazindua watu ambao tayari wamelishwa uchawi huu.
Kwahiyo unaiweza hii kazi ya kuwazindua waliozindikwa?
 
Baadhi ya vitu na vijua

Sent using i phone x
Haya, well-done, tutakutafuta ili utuangalie hata sisi tusiojua kama tumezindikwa malimbwata au lah. Ili tuwe na uhakika.

Maana jamii tunazoishi hivi viini macho vipo, wengine hasa wanawake wanazindikana ili mtu fulani aharibikiwe kimaisha asifanikiwe au mitoto ya jirani yake inazindikwa isiwe na maendeleo.

Hayo yote ni aina tu za malimbwata na waswahili wanafanyiziana. Japo kiimani tunafundishwa tusiabudu miungu wengine. Watu magumu yakiwazidia imani inawatoka wanakuja kwa wataalamu kama wewe walao kuchekiwa kama kuna linaloendelea kwao.
 
Niko kijijini kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka lakini pia nikiendelea kutafiti maarifa mapya na utaalam wa nguvu za giza, ushirikina na ulozi kwa matumizi chanya ya kilinge... Nia ikiwa ni kuwasaidia wahitaji.

Hizi habari za malimbwata kwa ajili ya kumshika mpenzi, mke au mume... Na wengine huenda mbali zaidi... Kwa ajili ya kumshika mwajiri au boss si ngeni kabisa masikioni mwetu... Na malimbwata maarufu yakiwa ni kwa kutumia vyakula na vinywaji.

Kuna hili limbwata baya zaidi.. Limbwata la kutiwa gundi mdomoni au kufungwa kamba.. La kutiwa gundi mdomoni hilo sahau kutongoza nje ama kuwa na kibezi mbele ya mwenza wako... Hapa mhitaji akifika kwa mganga hupewa kinyago chenye umbo la kiume na gundi ya maji au plasta.. Mhusika huelekezwa kukitia gundi mdomoni ama kukiziba na plasta huku akinuia kwa kutaja jina la mtu wake

Ukiachana na hilo la gundi kuna hili la kamba.. Kuna kamba kama za aina tatu hivi
Kamba laini
Kamba ngumu
Kamba ngumu na nzito

Aina ya kamba hutegemea na uimara kiroho wa mhusika anayetaka kufanyiwa... Mhitaji akifika kwa mganga atapewa kinyago chenye umbo la kiume na kamba husika.. Kamba hiyo atatakiwa aifunge shingoni, au miguuni au mikononi... Lakini pia inaweza kufungwa kote kwa pamoja huku akinuia

Baada ya hapo aliyefungwa hatakuwa na sauti tena kwenye lolote.. Atakuwa ni mtu wa kuamrishwa na kufuata maelekezo tuu... Utaburuta na kuburuza utakavyo.

Hili la kamba hutumika pia kufunga sehemu za siri za jinsia zote... Mwanamke akifungwa ndoa inaweza hata kusambaratika kwakuwa anakuwa hana hamu tena. Akifungwa mwanaume hupata ukhanithi.
Vikambakamba vipini pini na vigundigundi kwenye mapochi sio vitu vizuri sana


. View attachment 1304613View attachment 1304614

Jr
Kkkkkkkk,duh!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom