Life begins at 40 Vs Midlife crisis

Life begins at 40 Vs Midlife crisis

hapana... Unajua hatujui kuzimu kupoje... Sasa unapokufa unaacha madeni badala ya mali... Unaenda kutana na kitu usichokitegemea
Ukifa ndio imeisha hiyo mkuu, kuzimu na mbinguni ni hapahapa duniani, kama unaishi kwa kutegemea kuna better life baada ya hapa duniani, basi hauishi utakua unasubiria kufa
 
pole sana ERoni

mimi nadhani niko kwenye 'quarter life crisis' ndo namalizia teens zangu mseleleko wa kuhudumiwa na wazazi ndo unaisha, shule ndo namalizia, nawaza maisha yatakuwaje kujitegemea ndo kunaanza na I'm starting from almost zero...
Ni wakati wa kujiweka sawa, ili depression zisikupate.
 
Furahia kila siku Mungu anapokupa zawadi ya uhai.

Future na kesho yako iko mikononi mwa Mungu.

Kuna watu wana kila kitu leo jumapili familia zinakwenda kuwatembelea magerezani.

Ukiishi kama mpagani ndio utababaishwa na swala la umri.

Kwanza Bongo kwa kipato halali bila kufika miaka 50 plus hutoboi ng'oo utapata pesa ya kula tu na kuhifadhi matofali yasiibiwe.

Hapo kwenye kufurahia life kila siku ni mtihani kweli kweli. Unajua wengi wetu tunaona kama furaha ni kitu cha kukipata ukifanikisha jambo flani lakini ukilifikia, bado unaweka vigezo vingine na mwisho wa siku unakuwa si wa kuyafurahia maisha..

Sometimes nawish ningekuwa na mindset kama ya wamama wa uswazi, unakuta anakaanga mihogo ya kuuza asubuhi ili apate hela ya unga na fungu la dagaa. Baada ya hapo anasindikiza jua kwa umbeya na kama mlevi anakunywa double kiki yake. Maisha yanaenda bila stress

Ila haya ya kuangalia huna gari, nyumba, stable career mara utengeneze image ya kuendana na wenzio, yaani expectations kubwa kubwa ni stress tupu hadi tunashindwa enjoy simple things in life.
 
Maneno "life begins at 40" yana maana kuwa mtu akifika umri wa miaka 40, maisha yanakuwa bora zaidi, labda kwa sababu tayari mtu keshapata skills, experiences na namna bora ya kuyafurahia maisha. Msemo huu ulitungwa na mwanafalsafa Pitkins na umejipatia umaarufu mkubwa hapa duniani.

Katika kusomasoma kwangu nimekuja kufaham kwamba kumbe kuna watu wakifikia 40 wanapata hofu ya maisha(hapo hata mimi nikaanza kuwa na hofu), wanahisi uzee unakuja, ujana unaondoka, vile walivyokuwa wakiyafurahia maisha kama kujirusha, kula ujana vyote vinapotea ghafla.

Tunapoingia umri huu wa 40+, tunaanza kujitambua zaidi, kutambua thamani yetu zaidi na kutojali maisha na mawazo hasi ya wengine. Na hapa ndio hoja inapokuja, kwamba kwa mwafrika wa kawaida je ni kweli kwamba life begins at 40? Maana yapo mengi sana tunafatiliana, mtu kaacha yake anasumbukia ya jirani ili mradi tu amuumize au apate furaha kumuona mwenzake anaumia.

Wanasema at 46 life is at the peak, yaani kumbe ukifika 46 ndio umefikia peak ya maisha yako, baada ya hapo ile graph inaanza kushuka taratibu hadi upigwe chepe. Na wengine wanasema ukifika 40+ unatakiwa uwe tayari umefikia malengo yako kwa asilimia 90, kuzaa, kulea, career, kujenga, kusomesha...

Sasa je, nini kinaleta midlife crisis?

Kwa nini katika umri huo mara nyingi tunasemwa kuwa we're going through midlife crisis?

Je, ni kwa sababu huenda hatujafikia malengo yetu ya kimaisha na hivyo kufanya maisha kuwa na ukakasi?

Imagine katika umri huu:
● Huna mke/familia(very optional)
□ Watoto wadogo hawajaanza hata chekechea(kina sie).
● Hujawa na sehemu ya kujibanza(kijumba).
○ Hujawa stable career wise, bado unajitafuta.
Ni lazima kichwa kiwake moto, lazima stress levels ziwe juu na usipoangalia unaweza kupata sonona.

Msije na hoja ya maokoto tu.

Happy Sunday, mtuombee sie wakosefu!!
Kila msemo duniani una tabia za kibaguzi kwa watu ipendayo.Tusing'ang'anie misemo isiyoendana na uhalisia tulionao.Mmiliki wa KFC afufuke atupe miongozo.
 
Kwamba mtu akiwa 40+ awe tayari amewekeza na pesa zinamfuata tu mkuu? Sasa mbona wengi wetu ndio tunaanza kujitafuta, tulichelewa either kusoma, kupata watoto, kuwekeza...

Do we still have another chance?
Nyie ndo toeni ushuhuda mnajionaje onaje
 
maamuzi magumu haya,

umewaza nini, au ndo ile 'ndoa ni utapeli'😂
Kama binaadamu kuna vitu vingine unaona kabisa havikuumbwa kwaajili yako. Na enjoy sana nikiwa mwenyewe na uhuru wangu binafsi, labda nikilewa ndo napenda kuwa na watu karibu, ila nikiwa sober sipendelea kabisa social life wala mambo ya kuwa na wanawake/mwanamke wa kuniganda
 
Kwamba mtu akiwa 40+ awe tayari amewekeza na pesa zinamfuata tu mkuu? Sasa mbona wengi wetu ndio tunaanza kujitafuta, tulichelewa either kusoma, kupata watoto, kuwekeza...

Do we still have another chance?
Imagine unamaliza chuo at 25 years
 
I Think maisha hua yanaanza kuonekana yako speed pale unapoanza kupata watoto.
Because, hapo ndo hua tunaanza ku calculate umri.
Mfano umepata mtoto wa kwanza at 35 yrs as a man unapiga hesabu kuwa on average hadi amalize form six ni 19 yrs. So ukijumlisha na 35, unakua na 54yrs, tayari ndo unastaafu at 55. Hapo bado hajaenda chuo.
Na hapo hujapata wengine. Hiyo ndo inafanya kichwa iwake moto kabisaaaa
Very confusing
 
Binafsi sikuwah kufikiri kama umri ungekuja kuwa kitu serious cha kunichanganya moaka pale nilipo realize my life purpose.Yan toka nimekuja kujua ni wapi ninatakiwa kutulia na kuwekeza akili na nguvu zangu hapo, basi huwa naona kama muda unakimbia balaa mpaka kichwa kinauma.
Imefika hatua ya kutamani hata siku 1 ingekua angalau na masaa 30.

Huwa kuna time najilaumu kwamba akil hii nilionayo sasa kwanin sikua nayo nikiwa at around 26 years??

Anyway, cha msingi wakuu tupambane.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom