The Knowledge Seeker
JF-Expert Member
- Apr 13, 2019
- 4,226
- 6,372
Age is just a number and being Old that's the feelings..
( Buddhism )
( Buddhism )
Huwa ni mwisho ngapi 30 au?Ujana ushaisha hapo
Kwa Tanzania hiyo principle haifanyi kazi.Maneno "life begins at 40" yana maana kuwa mtu akifika umri wa miaka 40, maisha yanakuwa bora zaidi, labda kwa sababu tayari mtu keshapata skills, experiences na namna bora ya kuyafurahia maisha. Msemo huu ulitungwa na mwanafalsafa Pitkins na umejipatia umaarufu mkubwa hapa duniani.
Katika kusomasoma kwangu nimekuja kufaham kwamba kumbe kuna watu wakifikia 40 wanapata hofu ya maisha(hapo hata mimi nikaanza kuwa na hofu), wanahisi uzee unakuja, ujana unaondoka, vile walivyokuwa wakiyafurahia maisha kama kujirusha, kula ujana vyote vinapotea ghafla.
Tunapoingia umri huu wa 40+, tunaanza kujitambua zaidi, kutambua thamani yetu zaidi na kutojali maisha na mawazo hasi ya wengine. Na hapa ndio hoja inapokuja, kwamba kwa mwafrika wa kawaida je ni kweli kwamba life begins at 40? Maana yapo mengi sana tunafatiliana, mtu kaacha yake anasumbukia ya jirani ili mradi tu amuumize au apate furaha kumuona mwenzake anaumia.
Wanasema at 46 life is at the peak, yaani kumbe ukifika 46 ndio umefikia peak ya maisha yako, baada ya hapo ile graph inaanza kushuka taratibu hadi upigwe chepe. Na wengine wanasema ukifika 40+ unatakiwa uwe tayari umefikia malengo yako kwa asilimia 90, kuzaa, kulea, career, kujenga, kusomesha...
Sasa je, nini kinaleta midlife crisis?
Kwa nini katika umri huo mara nyingi tunasemwa kuwa we're going through midlife crisis?
Je, ni kwa sababu huenda hatujafikia malengo yetu ya kimaisha na hivyo kufanya maisha kuwa na ukakasi?
Imagine katika umri huu:
● Huna mke/familia(very optional)
□ Watoto wadogo hawajaanza hata chekechea(kina sie).
● Hujawa na sehemu ya kujibanza(kijumba).
○ Hujawa stable career wise, bado unajitafuta.
Ni lazima kichwa kiwake moto, lazima stress levels ziwe juu na usipoangalia unaweza kupata sonona.
Msije na hoja ya maokoto tu.
Happy Sunday, mtuombee sie wakosefu!!
Huwa ni mwisho ngap 30 au?
At 25 career wise bado, family bado, maendeleo bado, huenda hata shule bado kumaliza.Mi naona Life begins at 25, ukifika miaka 25 akili zote za utoto zinakua zimeisha huwazi tena kupiga picha kali,kucheza games, kama ramani hazijakaa sawa na unaakili timam hata usingizi huwa unakata katkat ya usiku wa manane
Na ukiendekeza mitandao ya kijamii unaona vijana wa umri wako wametoboa unaweza kujikuta hata furaha unakosa kabisa, ni umri mgumu sana vijana wengi wanajitoa uhai hapa 25-35, kwasababu changamoto za maisha zimeanza rasmi
25-35 ni muda ambao kijana unakuwa na msongo wa mawazo sana hasa kama umetokea familia zetu za chini ya dollar 1.Na swali langu lililenga hapo, kwamba hiyo life begins at 40 kwa Afrika na Tanzania inafanya kazi?
Sijasema at 46 umezeeka, ila wanasema umri huo upo katikati ya lifespan yako, nguvu na akili zipo kwenye peak yake.Asiwadanganye mtu wanangu
Maisha yanakuja jinsi yalivyo na hakuna wa kujua kesho
Hiyo 40 kama utafika ni uwezo wake Mola kwa wanaoamini hili
Wengi mna bahati kwa sasa kupata nasaha na kushauriwa humu, wengine wamekula maisha bila kujua
Wengine pia hata umshauri vipi bado atakula Bata bila kuwaza kuwekeza
Mimi sikuwa mtu wa starehe bali ni mtu wa kusafiri sana na kuiona Dunia, yaani ndio hobby yangu ila sasa nimepunguza kiasi ingawa bado nasafiri
Vijana kuweka akiba ni muhimu sana na 40 isiwatishe kwani nina over 60 na bado napiga kazi sana
Nani kawaambia ukifika 46 umezeeka sio kweli
Pigeni kazi sana mkiwa vijana msiwe watu wa kuomba omba
okay poa lakini ni kulingana mtu mwenyewe, mwingine 25 ni matured kabisa kama mtu mzima mwenye 40.35 hadi 40 hapo...
Ndio maana kwa nchi yetu, ruksa ya umri wa kugombea Urais ni miaka 40 +
Na wale wenye 18, 19 na 20 wao wapo kundi gani?35 hadi 40 hapo...
Ndio maana kwa nchi yetu, ruksa ya umri wa kugombea Urais ni miaka 40 +
Tofauti utaiona ukiwa apeche alolo, majukumu ni mengi yanakuangalia huna jinsi ya kusolve unajiona hopeless...ukiwa na ukwasi 40 is just a number.Huu msemo upo kama inspiration ya kupambana na kujiandaa vyema kwa walio chini ya 40 yrs, kutokana na uhalisia wa maisha ya binadamu akifikisha miaka 40 uwezo wake kwenye mambo mengi unakuwa sio sawa na ilivyokuwa kabla.
Nimejaribu tu kuwaza huenda huwa ni hivyo naomba wale ambao ni 40+ watupe experience yenye uhalisia.
Kwa hiyo Sasa sie wenye 40 graph yetu ndio inashuka au vipi?🥲Miaka 40+ wanasema umefikia peak ya graph ya maisha.
Frankly speaking Sina stress hata kidogo za uzee wala sioni aibu kusema nikaapproch 40....Nina stress mambo yangu ya pesa yakienda ndivyo sivyo only that!Wewe subiri kidogo, wanasema wakati unaapproach 40 unapata stress za uzee, imewahi kukutokea? Au ndio vile maokoto sio haba huna stress?