Life begins at 40 Vs Midlife crisis

ERoni

JF-Expert Member
Jan 9, 2013
43,678
90,162
Maneno "life begins at 40" yana maana kuwa mtu akifika umri wa miaka 40, maisha yanakuwa bora zaidi, labda kwa sababu tayari mtu keshapata skills, experiences na namna bora ya kuyafurahia maisha. Msemo huu ulitungwa na mwanafalsafa Pitkins na umejipatia umaarufu mkubwa hapa duniani.

Katika kusomasoma kwangu nimekuja kufaham kwamba kumbe kuna watu wakifikia 40 wanapata hofu ya maisha(hapo hata mimi nikaanza kuwa na hofu), wanahisi uzee unakuja, ujana unaondoka, vile walivyokuwa wakiyafurahia maisha kama kujirusha, kula ujana vyote vinapotea ghafla.

Tunapoingia umri huu wa 40+, tunaanza kujitambua zaidi, kutambua thamani yetu zaidi na kutojali maisha na mawazo hasi ya wengine. Na hapa ndio hoja inapokuja, kwamba kwa mwafrika wa kawaida je ni kweli kwamba life begins at 40? Maana yapo mengi sana tunafatiliana, mtu kaacha yake anasumbukia ya jirani ili mradi tu amuumize au apate furaha kumuona mwenzake anaumia.

Wanasema at 46 life is at the peak, yaani kumbe ukifika 46 ndio umefikia peak ya maisha yako, baada ya hapo ile graph inaanza kushuka taratibu hadi upigwe chepe. Na wengine wanasema ukifika 40+ unatakiwa uwe tayari umefikia malengo yako kwa asilimia 90, kuzaa, kulea, career, kujenga, kusomesha...

Sasa je, nini kinaleta midlife crisis?

Kwanini katika umri huo mara nyingi tunasemwa kuwa we're going through midlife crisis?

Je, ni kwa sababu huenda hatujafikia malengo yetu ya kimaisha na hivyo kufanya maisha kuwa na ukakasi?

Imagine katika umri huu:
● Huna mke/familia(very optional)
□ Watoto wadogo hawajaanza hata chekechea(kina sie).
● Hujawa na sehemu ya kujibanza(kijumba).
○ Hujawa stable career wise, bado unajitafuta.
Ni lazima kichwa kiwake moto, lazima stress levels ziwe juu na usipoangalia unaweza kupata sonona.

Msije na hoja ya maokoto tu.

Happy Sunday, mtuombee sie wakosefu!!
 
Huu msemo upo kama inspiration ya kupambana na kujiandaa vyema kwa walio chini ya 40 yrs, kutokana na uhalisia wa maisha ya binadamu akifikisha miaka 40 uwezo wake kwenye mambo mengi unakuwa sio sawa na ilivyokuwa kabla.

Nimejaribu tu kuwaza huenda huwa ni hivyo naomba wale ambao ni 40+ watupe experience yenye uhalisia.
 
Ni kweli Maisha yanaanza 40, umri huo unategemewa uwe umejiandaa na uzee, umeshawekeza, unamalizia malizia vitu vidogo vidogo ili ukifika 50 upumzike ule mafao, uenjoy maisha yaliyobaki, ujiandae na magonjwa na jinsi ya kupambana nayo.

Ukifika 40, bado huna ramani lazima hofu ikuingie, uwe depressed na wengi huanza kukata tamaa kwa kujihisi ndio basi, kumbe 40 inakupa last chance ya kupambania kujiandalia 50 yako.

Wito wangu kwa vijana tupige kazi bila kuchoka, fainali uzeeni.
 
Kuna kuishi na kuishia, nafikiri ukifika 40 unaianza safari ya kuishia duniani. Ila ukifika 30 unatakiwa kuwa umeanza kufanya kilichokuleta duniani.

Na ukiwa 20-29/30 hapo unatakiwa kuishi, huna stress, unazo nguvu zakutosha kuzurura, una uwezo wa kupata furaha kwa jambo dogo (mizuka).

Japo hii sio kwa wote maana kuna watu wana muaka 16 na wana stress zakutosha plus majukumu, ila kwa wengi au standard ya kidunia huo nivumri wa kuishi yaani kufurahia uwepo wako hapa duniani bila stress kali.
 
Kwa nini??
Sababu pesa ni chombo cha kufanyia kazi kiuchumi, sasa kukiweka ndani ni kuzuia kufanya kazi hivyo ni sawa na kuwa na shamba usilolima

Pia pesa inashuka thamani kila kukitokea mfumko wa bei, japo ni kwa kiasi kidogo sana cha asilimia ila taratibu thamani inashuka kila mwaka 1%-6%

Badala ya kutunza pesa, kinachotakiwa ni kuitoa pesa ikafanye kazi na wewe kukusanya mali (asset) ila usinunue vitu vinavyohitaji pesa kuvitunza (liability).

Au kama sio kununua mali, basi itoe pesa yako ikafanye kazi kwa njia ya hisa au mitaji kwenye biashara za watu, sio lazima kila mtu afanye biashara ila ni muhimu kila mwenye pesa aitoe ikafanye biashara/uzalishaji.

Mimi sio mtaalamu wa uchumi, ila ni jambo nililojifunza kwenye mihangaiko ya maisha Mkuu, so sitaweza kujibu maswali technical ya kiuchumi.

Labda kama una maswali yahusuyo sheria, mf. Namna gani unaweza itoa pesa yako ikafanye kazi kwenye biashara za watu na ubaki salama huku ukipata faida, hapo ntakujibu kwa ufasaha.
 
Kuna kuishi na kuishia, nafikiri ukifika 40 unaianza safari ya kuishia duniani. Ila ukifika 30 unatakiwa kuwa umeanza kufanya kilichokuleta duniani.

Na ukiwa 20-29/30 hapo unatakiwa kuishi, huna stress, unazo nguvu zakutosha kuzurura, una uwezo wa kupata furaha kwa jambo dogo (mizuka).

Japo hii sio kwa wote maana kuna watu wana muaka 16 na wana stress zakutosha plus majukumu, ila kwa wengi au standard ya kidunia huo nivumri wa kuishi yaani kufurahia uwepo wako hapa duniani bila stress kali.
Miaka 40+ wanasema umefikia peak ya graph ya maisha.
 
Ni kweli Maisha yanaanza 40, umri huo unategemewa uwe umejiandaa na uzee, umeshawekeza, unamalizia malizia vitu vidogo vidogo ili ukifika 50 upumzike ule mafao, uenjoy maisha yaliyobaki, ujiandae na magonjwa na jinsi ya kupambana nayo,

Ukifika 40, bado huna ramani lazima hofu ikuingie, uwe depressed na wengi huanza kukata tamaa kwa kujihisi ndio basi, kumbe 40 inakupa last chance ya kupambania kujiandalia 50 yako,

Wito wangu kwa vijana tupige kazi bila kuchoka, fainali uzeeni.
Ukifika 45 watoto wako watakuwa na umri gani mkuu.?
 
I Think maisha huwa yanaanza kuonekana yako speed pale unapoanza kupata watoto. Because, hapo ndo huwa tunaanza ku calculate umri.

Mfano umepata mtoto wa kwanza at 35 yrs as a man unapiga hesabu kuwa on average hadi amalize form six ni 19 yrs. So ukijumlisha na 35, unakuwa na 54yrs, tayari ndo unastaafu at 55. Hapo bado hajaenda chuo.
Na hapo hujapata wengine. Hiyo ndo inafanya kichwa iwake moto kabisaaaa
 
Back
Top Bottom