Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,513
- 113,641
Wanabodi,
Nilikuwa naangalia bunge kuapishwa kwa waheshimiwa wabunge wapya.
Ilipofika zamu ya Mhe. Upendo Furaha Peneza akiapa, nikamkumbuka Regia Mtema (RIP).
Kwa waumini wa 'life after life' na mambo ya 'reincarnation' mtanielewa!.
Kwa wafuatiliaji wa tanthiliya ya "Part of Me" kwenye Telemundo, tumemshuhudia Tajiri Monica Sorano, kabla ya kukutwa na umauti, alimtafuta mdada masikini Adrriana na bond naye!. Monica alipofariki, Adriana akaibuka na kukamilisha yale yote Monica aliyoyataka!.
Huyu mbunge Mhe. Upendo Furaha Peneza, alikuwa ni mshiriki tuu wa shindano la Maisha Plus. Ikatokea Regia akamuona akaja humu jf kumtafuta kwa bandiko hili Namtafuta Upendo Peneza wa Maisha Plus
[QUOTE Regia Mtema]Ni muda kidogo umepita bila kujua huyu binti Upendo yuko wapi.Nina shida nae sana kuna kazi nataka kufanya nae..namfeel sana huyo binti.
Tafadhali kwa wale mnaofahamu aliko naomba mnijulishe tafadhali.
Asanete sana.[/QUOTE] Baada ya muda akampata na kupandisha bandiko hili
Nimempata Upendo Peneza
ambapo hata hivyo hakusema anamtafutia nini!.[QUOTE Regia Mtema]Wiki chache zilizopita nilijithilokeza hadharani nikimtafuta Upendo wa Maisha Plus One katika jukwaa hili la Celebrities.Wengine walinikatisha tamaa wakiniona kama mimi ni fataki,wengine walinitia moyo,na wengine wakaniconnect na binti huyu..Nimewasiliana naye na kufanya appointment naye ya kuonana naye ana kwa ana kwaajili ya shughuli niliyokuwa nataka nifanye naye. I met with her yesterday evening tukazungumza kwa sana.Natarajia kufanya naye shughuli iliniyonifanya nimtafute.Tutakuwa wote Morogoro,Dodoma,Iringa,Arusha na Dar.
Namshukuru sana Masika na wengineo kwa kuniunganisha naye.Asanteni sana wote.[/QUOTE]
Kuna shughuli fulani nataka kufanya nae...Nitawajulish baadaye.
Asante sana FL1.Hatuko kwenye operesheni zinduka tuko kwenye operesheni lala salama.
Hapana ni kazi maalum Mkuu.Usiogope..Yuko salama 100%
Baada ya kumpata, baada ya muda wa kutosha kutimiza alichomtafutia, ndipo Regia akaenda ile safari...!.
Jee inawezekana ujio wa Upendo Furaha Peneza bungeni has something to do with kule kutafutwa na Regia?!.
Angalizo:Msije kutafsiri kuwa kuwa namuuliza Marehemu au namchunguza Maehemu, wala hili sio swali kuwa Jee Regia alikuwa anamtafutia nini Upendo Peneza, wala Upendo ambaye ni member humu, hatakiwi kuja kujibu Regia alimtafutia nini bali hili ni bandiko la mambo ya "life after life!" ambayo huwa hayazungumzwi bali yanashuhudiwa tuu kwenye performance!.
Paskali
Ref: Mnaweza kumsoma Upendo Furaha Peneza humu
- Upendo Furaha Peneza (@UpendoPeneza) | Twitte
- Upendo Furaha Peneza: Gold in the rough. Vijana CHADEMA mpo?
- Upendo Peneza ni malkia Nzinga Mbandi wa BAVICHA
- Upendo Peneza: Nahitaji kushinda na nitashinda
- Upendo Peneza leo Bungeni; Huyu Dada ana uwezo mkubwa sana
- Upendo Peneza wa CHADEMA atoboa siri ya CHADEMA na Sabodo
- Mungu amenipa nafasi nyingine ya kumtumikia na kutumikia watu wake. Praise be to God!
- Upendo Peneza kapata ajali Geita akitokea kwenye Mikutano ya Kampeni (05 Dec 2014)
- Upendo Peneza ataja sifa za mwanaume wa kumuoa
- Upendo Peneza (CHADEMA) awalaumu Wabunge wanaohama vyama. Asema chaguzi za marudio ni kucheza pesa za wananchi!
- Mheshimiwa Upendo Peneza asisitiza amani akiwa ziarani na Waziri Mkuu
- Mbunge Upendo Peneza(CHADEMA) akamatwa Geita mjini, aachiwa kwa dhamana
- Je, Rais wetu, Magufuli anasoma JF? Rais, Please msikilize Binti huyu, ana hoja ya Msingi!
Na kuhusu life after life
life after death
Dou you believe life after death ?
Do you believe in life after death?
Nini hutokea baada ya kufa?
Topic: Kifo ni nini na usababishwa na nini?
Topic: Kifo: Ni stahili yetu au adhabu?
Nakanusha kusifia na kuunga mkono Katiba inayo pendekezwa