Leonardo Da-Vinci

Leonardo Da-Vinci

Jibu:

'Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni wa anaye muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu (Qur'an) na Manabii (woote !), na ana wapa mali, kwa kupenda kwake, jamaa na mayatima, na masikini na wasafiri, na waombao, na katika ugombozi (kutoa mtu katika utumwa) na akawa ana shika Sala, na akatoa Zaka na wanao timiza ahadi yao wanapo ahidi, na wanao vumilia katika shida na dhara na wakati wa Vita. Hao ndio waliosadikisha, na hao ndio wajilindao.
Qur'an: 2:177.

Asante,asipoelewa mtu hapa basi ana lake jambo.Ana haki ya kukataa ama kukubali na wewe umefikisha ujumbe.
 
Nimekuuliza kama wewe una tatizo na hilo ulilolisema na wala sijakuuliza kama post yangu hiyo ina tatizo

Unaweza kuelewa kweli wewe?

Usielewa ni wewe ! ..........mimi nilikuwa naweka msisitizo kwenye post yako ya No 309, ya kuwa mungu mwingine alitoa kafara ya mwanawe wa pekee !.............mbali na hao ulio wataja wewe. uzaivaa !??:wave: Eiyer
 
Last edited by a moderator:
Usielewa ni wewe ! ..........mimi nilikuwa naweka msisitizo kwenye post yako ya No 309, ya kuwa mungu mwingine alitoa kafara ya mwanawe wa pekee !.............mbali na hao ulio wataja wewe. uzaivaa !??:wave: Eiyer
Kaazi kweli kweli!
 
Kwa haya maandiko yako yanaonesha ujinga [kutokujua] mkubwa ulionao kuhusiana na maandiko na kilichofanya yakawepo kwa utaratibu uliopo

Lakini cha kushangaza zaidi ya kushangaa kwenyewe ni kuwa umenilaumu mimi kwa "kuamini" kuwa kila kilichopo kwenye biblia kuwa kimetoka kwa Mungu bila kutiwa mikono na watu wakati watu hao hao ndio walioandika,halafu ukaweka kioja kingine kuwa "original manuscript" eti iliishia sijui 16:8,hapo kuna vioja viwili

1: Inaonekana hujui mtu anamaanisha nini anaposema hayo ni maandiko kutoka kwa Mungu kwasababu kitendo chako cha kudai kuwa unashangaa wakati maandiko yenyewe yameandikwa na watu inaonesha umaimuna mkubwa sana ulionao kuhusiana na suala zima la uandishi na kauli ya "maneno kutoka kwa Mungu"

2: Umedai kuwa kuna "original manuscript",sijui huo u-original unautoa wapi na kipa hiyo manuscript yako kutokana na hiyo dhana hapo juu,kama maandiko yote yameandikwa na wanadamu basi either yote ni original au yote ni fake kutokana na context ya maelezo yako hapo juu na sijui kama una uwezo wa kung'amua hili

Kwa kifupi umohoroja tu hapa na hakuna ulichosema chenye mantiki

Nadhani hata hujui maana ya "sawa" wewe

Hivi hujui hata wewe uko sawa?

Mtu yoyote yuko sawa kutokana na kile anachokisema ila kuthibitisha asemacho ni suala lingine

Nikikuambia uthibitishe haya maelezo yako tutakesha hapa

Na kikubwa sana hapa hatutafuti mshindi bali tunaweka maelezo ambayo kama kuna msomaji ataona yana mashiko basi atayachukua na kuyafanyia kazi,kama unatafuta aliye sawa na asie sawa utakesha kwa kuwa hata hiyo sawa yenyewe inategemea na mtu mwenyewe anaeona jambo kuwa sawa

Wewe unaweza kuona ni sawa kujisaidia shambani mwako ili hiyo mbolea inayotoka tumboni mwako irutubishe mazao utakayokuja kulima baadae na kuna mwingine hataona ni sawa kufanya hivyo na nyote mkawa sawa kwa mujibu wa kila mmoja

Kabla ya kuanza kutupigia gitaa lako la "hii biblia tuliyonayo leo haiko sawa na ya mwanzo" inabidi kwanza uthibitishw uwepo wa hiyo biblia na pia uthibitishe kuwa mwanzo ni kitu gani halafu thibitishe madai yao kuwa ni heretical kuwa sio ya kweli maana wao kutokukupa majibu ya "kukuridhisha" wewe sio uthibitisho wa kuwa hayo maandiko ambayo kwanza hata hujayathibitisha kama yapo kuwa sio heretical

Tatizo lako kubwa ni wewe kudhani kuwa kitendo cha mtu kuongea na mitume basi akiandika barua basi nayo ni neno la Mungu

Mbona humsemi Timotheo?
Hivi unajua kuwa ni wangapi waliongea na mitume?
Unataka maandiko yao wote yawepo kwenye biblia ili iweje?

Sio kila walichokiandika kinawekwa kwenye maandiko matakatifu na ndio maana nakuambia kuwa wewe una umaimuna mkubwa sana kwenye eneo hili na kibaya zaidi hujajua hilo

Tayari nimeshajadili!


Wewe ndiye mjinga kwa kudhani kuwa Biblia yote ina maneno ya Mungu as if imeshushwa tu magically from the clouds.Huna unachokijua zaidi ya dogma uliyolishwa na ukameza mazimamazima kama zuzu.
Hapo nimekugusa kidogo tu,povu zinakutoka.Nikikwambia tujadili John na nani aliandika,kwanini iko tofauti utaweza?Tujadili synoptic problem,Q source, utaweza?Tujadili Matthew,lengo lake nini,alikuwa nani,kwanini kawekwa mwanzo na style yake ya uandishi ilimlenga nani utaweza wewe?

Hakuna Mungu aliyeshusha wala kuandika Biblia.Ni binadamu walikaa na kuandika yote unayoyaona kwenye hiyo Biblia yako na ndiyo maana kuna contradictions nyingi mno kwenye hivi vitabu.Kusema kuwa walikuwa divinely inspired ndipo wakaandika ni hoja iso mashiko,kwavile the immediate qtn ni kwanini wawe wao na asiwe myahudi Josephus?au Mary of Magdala?Nani anaweka standards kuwa huyu ni divinely inspired na huyu siye?Kajuaje?na wewe na mimi tunajuaje?

Biblia haikuandikwa siku moja kwa pamoja kutoka source moja.Lazima uelewe ukweli huu kwanza.Maisha ya Yesu na mafundisho yake yalianza kuandikwa miaka zaidi ya hamsini baada ya kufa kwake.Kulikuwa na waandishi wa mwanzo kabisa kuanzia 60-150AD ambao miongoni mwao ndiye huyu Mark wa gospel according to Mark inayoishia 16:8 kabla ya viongezeo.Hizi kazi za mwanzo ndizo original manuscripts au original source/primary source ya vitabu vya hii Biblia unayoitumia.Kwahiyo baadaye zilifuata additions humo,translations na revisions nyingi tu(ambazo zilifanywa na watu pia) mpaka ikapatikana hii Biblia ya sasa.

Kuamini kuwa kitabu kilichoandikwa 60AD kwa Kigiriki au Kiebrania ni sawasawa kabisa kwa asilimia mia na unachokisoma leo kwenye Lugha ya Kiingereza au Kiswahili baada ya misukosuko mingi ya kijamii na kisiasa ya tawala za kipagani na hata za kidini iliyotokea katika sehemu ambazo vitabu hivi viliasiliwa, ni umbumbumbu usio mfano na sitashangaa nikisikia wewe ni mmoja wapo wa mateja yaliyokubuhu katika maombi ya manabii feki wa zama hizi waliochipukia kwa wingi duniani na kutapeli watu wengi wasio na maarifa kuhusu imani wanazofuata.

Halafu usiniwekee maneno ambayo sikuandika.Hakuna niliposema kuwa mtu akiongea na mitume basi anachoandika ni neno la Mungu.Nilichohoji ni kwanini vitabu vingine viliondolewa kwenye Biblia na vingine viliachwa na nilikupa mfano wa codex sinaiticus uende ukasome,na ungeona kuwa kulikuwa na barua ya Barnabas ambayo ilikuja kuondolewa baadaye.

Jifunze kwanza historia ya Ukristo na Biblia kabla ya kuanza kutoa povu kwa vitu usivyovielewa vizuri.
 
Mkuu ukitaka tujadili vitabu vya Apocrypha kwa mrengo wa kwamba walio viondoa walikosea tutakuwa tunakosea sana....M
Maana hata Martin Luther aliondoa vitabu 7 vya Agano la kale akabakiwa na vitabu 66.....Pia alitaka kuondoa kitabu cha James ila reformer wenzake wakina Calvin walimkataza....
Huenda leo kuna wakristo wangekuwa na vitabu 26 vya agano Jipya..

Sasa cha msingi ni kujua kwann waliviondoa.....Kwann waliviita Heretical....Kwasababu hata Injili zilikuwa 24 ila kwenye mtaguso wa Effeso walichambua wakabakiza 4...Sasa mm naamini kuna sababu nzuri tuu ya kuvikataa vitabu hivyo..

Kumbuka Biblia ni mkusanyiko..

Eiyer tafadhali usiharibu mjadala maana naona huna unalolifahamu zaidi ya hisia kali na ushabiki huku ukijawa na maswali ambayo hata wewe huwezi kuyajibu japikuwa umeyauliza..


Kwanini unadhani tunakosea tukijadili kuwa walikosea kuvikataa apocrypha?Kwanini unadhani kuvikataa ama kuviondoa na kuviita apocrypha ni uamuzi sahihi?

Leo pale Vatican(Roma) ndani ya Basilica la St.Peter,ukiingia chini kule kwenye grottoes kuna kaburi la Peter,lakini hakuna any biblical connection iso na shaka kati ya Peter and Rome.Acts of Peter ingeweza kuziba pengo hili kwavile inataja mpaka martyrdom wakati wa utawala wa Nero.au unaonaje mkuu?au tuamini zaidi ahadith za Eusebius?

Mkuu taja hizo injili 24 zilizochambuliwa kwenye mtaguso wa Efeso tuzichambue na sisi tuone shida ilikuwa nini hasa mpaka vikaachwa.Ili mjadala uwe mzuri ni vizuri ukavitaja wewe hivyo vitabu 24.Nadhani unajua hata John ilikuwa aondolewe,sasa sijui kama unajua kwanini alibakizwa?
 
Kwani sisi ni nani na tunaishi kwa uwezo wa nani mkuu?

Tuna chochote kwenye maisha yetu ambacho tumekipata kwa uwezo wetu [kama tunao]?


Sisi ni binadamu mkuu

Kwani mkuu laptop unayotumia umeipata kwa uwezo wa nani labda,si umepiga kazi au?


Au unamanisha kapata vitu gani ambavyo hatujapata kwa uwezo wetu,labda uvitaje!

Tunaishi kwa kwa pumzi ,vyakula na maji,na mahitaji mengine yanayofanikisha hili.

I will back.
 
Wewe ndiye mjinga kwa kudhani kuwa Biblia yote ina maneno ya Mungu as if imeshushwa tu magically from the clouds.Huna unachokijua zaidi ya dogma uliyolishwa na ukameza mazimamazima kama zuzu.
Hapo nimekugusa kidogo tu,povu zinakutoka.Nikikwambia tujadili John na nani aliandika,kwanini iko tofauti utaweza?Tujadili synoptic problem,Q source, utaweza?Tujadili Matthew,lengo lake nini,alikuwa nani,kwanini kawekwa mwanzo na style yake ya uandishi ilimlenga nani utaweza wewe?
Hujanielewa kabisa au inawezekana huna uwezo wa kuelewa kama utakuwa umesoma maelezo yangu
Hilo litakuwa wazi kwa yoyote ambae atakuja na kusoma maelezo yangu na yako
Hakuna Mungu aliyeshusha wala kuandika Biblia.Ni binadamu walikaa na kuandika yote unayoyaona kwenye hiyo Biblia yako na ndiyo maana kuna contradictions nyingi mno kwenye hivi vitabu.Kusema kuwa walikuwa divinely inspired ndipo wakaandika ni hoja iso mashiko,kwavile the immediate qtn ni kwanini wawe wao na asiwe myahudi Josephus?au Mary of Magdala?Nani anaweka standards kuwa huyu ni divinely inspired na huyu siye?Kajuaje?na wewe na mimi tunajuaje?
Ndugu nakushauri badala ya kuandika tu hebu uwe unasoma maandiko yangu na kama mara moja inakushinda kuelewa basi soma mara nyingi uwezavyo ili ukija kujibu ujibu kwa hoja ambayo inakuwa na mashiko

Hiki ulichokiandika hapa nimeshakitolea maelezo nikikujibu tena tutakuwa tunarudia kitu kile kile bila sababu ya msingi
Kabla ya kujibu nilichokuandikia unaendelea kuongeza maswali na kwa mwendo huu yatakushinda tu,madai yako ya kuwepo kujikinza kwenye Biblia hujayatolea maelezo ya kutosha hivyo nayaacha kama yalivyo
Biblia haikuandikwa siku moja kwa pamoja kutoka source moja.Lazima uelewe ukweli huu kwanza.Maisha ya Yesu na mafundisho yake yalianza kuandikwa miaka zaidi ya hamsini baada ya kufa kwake.Kulikuwa na waandishi wa mwanzo kabisa kuanzia 60-150AD ambao miongoni mwao ndiye huyu Mark wa gospel according to Mark inayoishia 16:8 kabla ya viongezeo.Hizi kazi za mwanzo ndizo original manuscripts au original source/primary source ya vitabu vya hii Biblia unayoitumia.Kwahiyo baadaye zilifuata additions humo,translations na revisions nyingi tu(ambazo zilifanywa na watu pia) mpaka ikapatikana hii Biblia ya sasa.
Unajua unaweza kuwa unasema kweli lakini ili iwe kweli na watu wakubali sio tu wewe kuandika hapa bali ni kuambatanisha na ushahidi ndugu yangu

Kusema tu sijui injili ilikuwa inaishia hapa au pale utakuwa kama vile unapiga story za kwenye kahawa tu

Najua kuwa biblia haikuandikwa siku moja lakini kitendo cha wewe kudai kuwa haikuandikwa kutoka kwenye source moja kinanilazimu nikudai uniambie hiyo source nyingine ni ipi au zipi kama ziko nyingi na unipe ushahidi wa hilo na uj\niambie umejuaje
Kuamini kuwa kitabu kilichoandikwa 60AD kwa Kigiriki au Kiebrania ni sawasawa kabisa kwa asilimia mia na unachokisoma leo kwenye Lugha ya Kiingereza au Kiswahili baada ya misukosuko mingi ya kijamii na kisiasa ya tawala za kipagani na hata za kidini iliyotokea katika sehemu ambazo vitabu hivi viliasiliwa, ni umbumbumbu usio mfano na sitashangaa nikisikia wewe ni mmoja wapo wa mateja yaliyokubuhu katika maombi ya manabii feki wa zama hizi waliochipukia kwa wingi duniani na kutapeli watu wengi wasio na maarifa kuhusu imani wanazofuata.
Usiwe unapenda ku assume kwa sababu sio sahihi kwa mtu makini kufanya hivyo

Tatizo lako unadhani kila mtu anafuata mambo kimkumbo wakati sio kweli,unapojadiliana na mtu usi assume kuwa hajui,weka nondo zako kisha umpime,so far sijaona chochote ulichokiweka hapa ambacho ni cha msingi naona unaleta maoni yako tu kitu ambacho siwezi kukijadili kwani siko hapa kujadili maoni bali fact
Halafu usiniwekee maneno ambayo sikuandika.Hakuna niliposema kuwa mtu akiongea na mitume basi anachoandika ni neno la Mungu.Nilichohoji ni kwanini vitabu vingine viliondolewa kwenye Biblia na vingine viliachwa na nilikupa mfano wa codex sinaiticus uende ukasome,na ungeona kuwa kulikuwa na barua ya Barnabas ambayo ilikuja kuondolewa baadaye.
Una matatizo makubwa sana ya kuelewa wewe
Jifunze kwanza historia ya Ukristo na Biblia kabla ya kuanza kutoa povu kwa vitu usivyovielewa vizuri.
Sijazungumza chochote kuhusiana na historia sijui umejuaje kuwa sijui historia

Una assume sana wewe,hebu punguza!
 
Sisi ni binadamu mkuu

Kwani mkuu laptop unayotumia umeipata kwa uwezo wa nani labda,si umepiga kazi au?


Au unamanisha kapata vitu gani ambavyo hatujapata kwa uwezo wetu,labda uvitaje!

Tunaishi kwa kwa pumzi ,vyakula na maji,na mahitaji mengine yanayofanikisha hili.

I will back.

Wewe uwepo wako unategemea mazingira kwa maana ya chakula unachokula,maji hewa n.k,vyote hivi visipokuwepo huwezi kuishi na hivyo vyote vinakuwepo kwasababu ya kanuni zinazouendesha ulimwengu na yupo aliyeziweka hizo kanuni,huna chako hapo hata kimoja na hata wewe mwenyewe sio wako bali unamilikiwa

Hizo unazoita nguvu ukiulizwa ulikozitoa utajibu nini mkuu?
 
Hujanielewa kabisa au inawezekana huna uwezo wa kuelewa kama utakuwa umesoma maelezo yangu
Hilo litakuwa wazi kwa yoyote ambae atakuja na kusoma maelezo yangu na yako

Ndugu nakushauri badala ya kuandika tu hebu uwe unasoma maandiko yangu na kama mara moja inakushinda kuelewa basi soma mara nyingi uwezavyo ili ukija kujibu ujibu kwa hoja ambayo inakuwa na mashiko

Hiki ulichokiandika hapa nimeshakitolea maelezo nikikujibu tena tutakuwa tunarudia kitu kile kile bila sababu ya msingi
Kabla ya kujibu nilichokuandikia unaendelea kuongeza maswali na kwa mwendo huu yatakushinda tu,madai yako ya kuwepo kujikinza kwenye Biblia hujayatolea maelezo ya kutosha hivyo nayaacha kama yalivyo

Unajua unaweza kuwa unasema kweli lakini ili iwe kweli na watu wakubali sio tu wewe kuandika hapa bali ni kuambatanisha na ushahidi ndugu yangu

Kusema tu sijui injili ilikuwa inaishia hapa au pale utakuwa kama vile unapiga story za kwenye kahawa tu

Najua kuwa biblia haikuandikwa siku moja lakini kitendo cha wewe kudai kuwa haikuandikwa kutoka kwenye source moja kinanilazimu nikudai uniambie hiyo source nyingine ni ipi au zipi kama ziko nyingi na unipe ushahidi wa hilo na uj\niambie umejuaje

Usiwe unapenda ku assume kwa sababu sio sahihi kwa mtu makini kufanya hivyo

Tatizo lako unadhani kila mtu anafuata mambo kimkumbo wakati sio kweli,unapojadiliana na mtu usi assume kuwa hajui,weka nondo zako kisha umpime,so far sijaona chochote ulichokiweka hapa ambacho ni cha msingi naona unaleta maoni yako tu kitu ambacho siwezi kukijadili kwani siko hapa kujadili maoni bali fact

Una matatizo makubwa sana ya kuelewa wewe

Sijazungumza chochote kuhusiana na historia sijui umejuaje kuwa sijui historia

Una assume sana wewe,hebu punguza!


Kumbe wewe ni zaidi ya mjinga.Unapenda ligi za kubishana tu hata kama huna hoja.Nimekupa mifano mingi na hints uende ukajisomee lakini kumbe unataka utafuniwe kila kitu hapa,sasa patatosha kweli nikianza kujaza ma soft copies ya vitabu na makala mbalimbali?

Mjadala mzuri ni kusoma kwanza halafu tunaleta hoja zetu baada ya kuelewa tulichosoma.Sasa acha ubishi wa kijinga,nenda kasome kwanza waandishi wa vitabu vya Biblia wa mwanzo walikuwa nani anzia na waandishi wa agano jipya(Injili),kasome umuhimu wa vulgate la Jerome,synoptic problem,Q source,codex sinaiticus,apocrypha.Kisha soma decretum gelasianum,synod of Hippo ya 393AD na Carthage ya 397AD na maazimio yake halafu ukishaelewa ndipo uje tujadiliane,walau niwe kwenye nafasi ya kujadiliana na mtu mwenye uelewa kidogo na siye mwenye kujibanza kwenye imani yake aliyokaririshwa.
 
Kumbe wewe ni zaidi ya mjinga.Unapenda ligi za kubishana tu hata kama huna hoja.Nimekupa mifano mingi na hints uende ukajisomee lakini kumbe unataka utafuniwe kila kitu hapa,sasa patatosha kweli nikianza kujaza ma soft copies ya vitabu na makala mbalimbali?
Sawa mimi ni zaidi ya mjinga

Mjinga kwa tafsiri yako ni yule ambae anaedai ushahidi wa madai yako

Halafu unanishangaza zaidi kwa kusema nakutaka ulete copy za vitabu,nani kasema haya?
Ninachokitaka kwako sio copy ya maandishi ya mtu mwingine kwasababu najua matatizo ya copy,unaweza ukaleta kitu ambacho hata wewe mletaji hujakielewa na nikikuuliza hutakuwa na majibu,ninachotaka ulete hapa ni kile ulichokielewa huko ulikosoma ukiambatanisha na ushahidi na sio copy
Mjadala mzuri ni kusoma kwanza halafu tunaleta hoja zetu baada ya kuelewa tulichosoma.Sasa acha ubishi wa kijinga,nenda kasome kwanza waandishi wa vitabu vya Biblia wa mwanzo walikuwa nani anzia na waandishi wa agano jipya(Injili),kasome umuhimu wa vulgate la Jerome,synoptic problem,Q source,codex sinaiticus,apocrypha.Kisha soma decretum gelasianum,synod of Hippo ya 393AD na Carthage ya 397AD na maazimio yake halafu ukishaelewa ndipo uje tujadiliane,walau niwe kwenye nafasi ya kujadiliana na mtu mwenye uelewa kidogo na siye mwenye kujibanza kwenye imani yake aliyokaririshwa.
Umejuaje sijui hayo uliyoyaorodhesha?

Aliyekuambia siijui historia ni nani?
Tatizo lako wewe ni kuandika kile unachofikiria na kudhani ndicho hali halisi,nikikuuliza ni wapi umeleta fact za kihistoria na nikakuambia ni uongo utajibu kitu gani?

Kama una chochote kuhusiana na hayo uliyosema leta hapa na ushahidi,kitu gani kinakushinda?

Badala ya kuleta hoja unakuja na hadithi zako eti injili ya kwanza ni sijui nani na ilikuwa inaishia sijui wapi bila hata kuleta ushahidi na kutuambia huo ushahidi ulikoutolea na unataka tu tukubaliane na wewe bila kuhoji

Halafu eti mimi ni zaidi ya mjinga......!!
 
Sawa mimi ni zaidi ya mjinga

Mjinga kwa tafsiri yako ni yule ambae anaedai ushahidi wa madai yako

Halafu unanishangaza zaidi kwa kusema nakutaka ulete copy za vitabu,nani kasema haya?
Ninachokitaka kwako sio copy ya maandishi ya mtu mwingine kwasababu najua matatizo ya copy,unaweza ukaleta kitu ambacho hata wewe mletaji hujakielewa na nikikuuliza hutakuwa na majibu,ninachotaka ulete hapa ni kile ulichokielewa huko ulikosoma ukiambatanisha na ushahidi na sio copy

Umejuaje sijui hayo uliyoyaorodhesha?

Aliyekuambia siijui historia ni nani?
Tatizo lako wewe ni kuandika kile unachofikiria na kudhani ndicho hali halisi,nikikuuliza ni wapi umeleta fact za kihistoria na nikakuambia ni uongo utajibu kitu gani?

Kama una chochote kuhusiana na hayo uliyosema leta hapa na ushahidi,kitu gani kinakushinda?

Badala ya kuleta hoja unakuja na hadithi zako eti injili ya kwanza ni sijui nani na ilikuwa inaishia sijui wapi bila hata kuleta ushahidi na kutuambia huo ushahidi ulikoutolea na unataka tu tukubaliane na wewe bila kuhoji

Halafu eti mimi ni zaidi ya mjinga......!!


Hujui,nenda kasome hizo hints nilizokupa.Kuna shida gani kukubali kuwa hujui kitu?Maandishi yako yanaonyesha hujui maana unaleta ubishi wa kijinga kabisa,unaoonyesha kuwa huijui historia ya Biblia na huijui Biblia yenyewe nje ya dogma ya kukaririshwa.

Kwenye hiyo mitaguzo niliyokuambia ukasome iliyofanyika karne ya nne na tano ndipo vitabu vya Biblia vya canon vilianza kurasmishwa na kuwa listed na vingine vikaanza kuitwa apocrypha.Sasa ni historia ndefu wewe unataka nikusimulie yote hapa,na vitabu vyote nilivyosoma.Yaani umeshindwa kabisa kutafuta maarifa nje ya box la dogma pamoja na kukua kote huku kwa teknolojia?Ku google tu 'ending(s) of Mark' huwezi,synoptic problem huwezi?

Kama hutaki kusoma kwanza na ukaendeleza hoja za kijinga,sitapoteza muda wangu na wewe.Bora nimsubiri mkuu otorong'ong'o labda tutaweza kuwa na mjadala wenye manufaa manake anaonyesha anajua.
 
Hujui,nenda kasome hizo hints nilizokupa.Kuna shida gani kukubali kuwa hujui kitu?Maandishi yako yanaonyesha hujui maana unaleta ubishi wa kijinga kabisa,unaoonyesha kuwa huijui historia ya Biblia na huijui Biblia yenyewe nje ya dogma ya kukaririshwa.

Kwenye hiyo mitaguzo niliyokuambia ukasome iliyofanyika karne ya nne na tano ndipo vitabu vya Biblia vya canon vilianza kurasmishwa na kuwa listed na vingine vikaanza kuitwa apocrypha.Sasa ni historia ndefu wewe unataka nikusimulie yote hapa,na vitabu vyote nilivyosoma.Yaani umeshindwa kabisa kutafuta maarifa nje ya box la dogma pamoja na kukua kote huku kwa teknolojia?Ku google tu 'ending(s) of Mark' huwezi,synoptic problem huwezi?

Kama hutaki kusoma kwanza na ukaendeleza hoja za kijinga,sitapoteza muda wangu na wewe.Bora nimsubiri mkuu otorong'ong'o labda tutaweza kuwa na mjadala wenye manufaa manake anaonyesha anajua.

Aiseee .....

Haya ndugu yangu,endelea na ku assume hivyo hivyo

Sijui kitu

Wacha niendelee na mambo mengine!
 
Eiyer umeiona ndugu yangu hao vipofu hawaoni labda kuwaombea tunadiffer IQ MKUU
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom