Nimezisoma hoja zako.Inaelekea wewe ni mtu wa dogma.Unaamini kila kilichopo kwenye hii Biblia ya leo kimetoka kwa Mungu na hakina mkono wa binadamu,wakati ni binadamu haohao ndiyo walioandika vitabu vya Biblia kwa mikono yao na kuviweka katika huu mtiririko tulionao.
Kwa mfano injili ya Marko original manuscript iliishia 16:8 na kunakoendelea ni watu tu walikaa wakaamua kujazia ili ilete maana kusudiwa,sijui unajua hili?
Kwa haya maandiko yako yanaonesha ujinga [kutokujua] mkubwa ulionao kuhusiana na maandiko na kilichofanya yakawepo kwa utaratibu uliopo
Lakini cha kushangaza zaidi ya kushangaa kwenyewe ni kuwa umenilaumu mimi kwa "kuamini" kuwa kila kilichopo kwenye biblia kuwa kimetoka kwa Mungu bila kutiwa mikono na watu wakati watu hao hao ndio walioandika,halafu ukaweka kioja kingine kuwa "original manuscript" eti iliishia sijui 16:8,hapo kuna vioja viwili
1: Inaonekana hujui mtu anamaanisha nini anaposema hayo ni maandiko kutoka kwa Mungu kwasababu kitendo chako cha kudai kuwa unashangaa wakati maandiko yenyewe yameandikwa na watu inaonesha umaimuna mkubwa sana ulionao kuhusiana na suala zima la uandishi na kauli ya "maneno kutoka kwa Mungu"
2: Umedai kuwa kuna "original manuscript",sijui huo u-original unautoa wapi na kipa hiyo manuscript yako kutokana na hiyo dhana hapo juu,kama maandiko yote yameandikwa na wanadamu basi either yote ni original au yote ni fake kutokana na context ya maelezo yako hapo juu na sijui kama una uwezo wa kung'amua hili
Kwa kifupi umohoroja tu hapa na hakuna ulichosema chenye mantiki
Iron Lady yuko sawa kabisa.
Nadhani hata hujui maana ya "sawa" wewe
Hivi hujui hata wewe uko sawa?
Mtu yoyote yuko sawa kutokana na kile anachokisema ila kuthibitisha asemacho ni suala lingine
Nikikuambia uthibitishe haya maelezo yako tutakesha hapa
Na kikubwa sana hapa hatutafuti mshindi bali tunaweka maelezo ambayo kama kuna msomaji ataona yana mashiko basi atayachukua na kuyafanyia kazi,kama unatafuta aliye sawa na asie sawa utakesha kwa kuwa hata hiyo sawa yenyewe inategemea na mtu mwenyewe anaeona jambo kuwa sawa
Wewe unaweza kuona ni sawa kujisaidia shambani mwako ili hiyo mbolea inayotoka tumboni mwako irutubishe mazao utakayokuja kulima baadae na kuna mwingine hataona ni sawa kufanya hivyo na nyote mkawa sawa kwa mujibu wa kila mmoja
Biblia tunayoijua leo,ni tofauti na Biblia za mwanzo.Kuna vitabu viliondolewa na ukiuliza kwanini viliondolewa,watakwambia ni heretical.Ukiuliza wamejuaje ni heretical na kwanini hivi vilivyopo visiwe heretical?Hutapata majibu ya kuridhisha.
Kabla ya kuanza kutupigia gitaa lako la "hii biblia tuliyonayo leo haiko sawa na ya mwanzo" inabidi kwanza uthibitishw uwepo wa hiyo biblia na pia uthibitishe kuwa mwanzo ni kitu gani halafu thibitishe madai yao kuwa ni heretical kuwa sio ya kweli maana wao kutokukupa majibu ya "kukuridhisha" wewe sio uthibitisho wa kuwa hayo maandiko ambayo kwanza hata hujayathibitisha kama yapo kuwa sio heretical
Kwenye codex Sinaiticus,moja kati ya Biblia za mwanzo kabisa;kulikuwa na epistle of Barnabas.Leo kwenye Biblia,hii barua ya Barnabas haipo.Na huyu Barnabas alikuwa karibu sana na Paulo na ndiye aliyemtambulisha Paulo kwa kina Peter na John na James,waliokuwa wanaendesha ukristo Jerusalem.Ni mtu muhimu sana katika kuusambaza ukristo mpaka ukafikia hapa ulipofikia.Lakini barua yake(mtu ambaye aliongea ana kwa ana na kina James na Peter na Paulo),ikaonekana haifai na watu ambao hata hawakumjua huyo Peter na John na Paulo walikuwa ni watu wa namna gani
Tatizo lako kubwa ni wewe kudhani kuwa kitendo cha mtu kuongea na mitume basi akiandika barua basi nayo ni neno la Mungu
Mbona humsemi Timotheo?
Hivi unajua kuwa ni wangapi waliongea na mitume?
Unataka maandiko yao wote yawepo kwenye biblia ili iweje?
Sio kila walichokiandika kinawekwa kwenye maandiko matakatifu na ndio maana nakuambia kuwa wewe una umaimuna mkubwa sana kwenye eneo hili na kibaya zaidi hujajua hilo
Njoo tujadili mkuu kama una muda japo tuko nje ya mada husika!
Tayari nimeshajadili!