Leo nimefanya mkutano wa tatu jijini Arusha. Sijazomewa

Ndugu zangu Watanzania hawa ndio aina ya viongozi wenu...
Wanajipima utendaji wao kwa kelele za wananchi...
Imani ya mtu huyu ni kwamba kama hujazomewa basi unakubalika...
Na zaidi sio kukubalika tu bali hata kazi ya mikono yake inakubalika...
Hii sio sawa, bali ni aina mojawapo ya utapeli na ulimbukeni...
Watanzania msikubali kuendeshwa na watu wa namna hii maana ni aina ya viongozi wa msimu...
 
Nilikuwepo maeneo ya Mianzini na umezomewa sana.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Wana jf nimefanya mikutano mitatu mpaka sasa hakuna hata mkutano mmoja nimepatwa na kelele ya aina yeyote. Anayedhani kuna mkutano nimezomewa aendelee kuamini hivyohivyo, majibu yanakuja tar 16.
Whether umezomewa au hujazomewa, lakini mimi nakuonya uache kumdhalilisha yule kijana mliyemmwagia tindikali kule Igunga, na kuanza kumtembeza kama kinyago kwenye mikutano eti huo nao ni mtaji wenu kisiasa? Hammutendei haki kabisa yule kijana japo ni maskini. Kama mnataka kumpa kazi ya kampeni, mpeni lakini si kupita kwenye kila mkutano nchi nzima mkimdhalilisha kutokana na ulemavu mliousababisha wenyewe. Ni nani asiyewajua CCM kwa mbinu zenu za kuwatuma polisi waue kwenye mikutano ya CHADEMA ili mpate mtaji wa kisiasa kwamba CHADEMA wameua? Yaani mkiwa mnatafuta kura roho ya utanzania huwa inawatoka kabisa, badala yake mnatumia nguvu nyingi tu kuhakikisha mnashinda bila kujali mnawaachaje watanzania mara baada ya uchaguzi. Ni spirit hiyo hiyo ndiyo imepelekea nchi kuingia kwenye udini. Hebu wekeni maslahi ya nchi mbele kwanza kabla ya kujifikiria ushindi wetu peke yake.
 
Mwigulu kubali tu yaishe, siku zinalingana tu lakjini hazifanani! Kila sehemu in sifa na haiba yake. Singida ni tofauti na Arusha, kigoma ni tofauti na Singida na Mwanza ni tofauti na Tabora n.k.
 
Wana jf nimefanya mikutano mitatu mpaka sasa hakuna hata mkutano mmoja nimepatwa na kelele ya aina yeyote. Anayedhani kuna mkutano nimezomewa aendelee kuamini hivyohivyo, majibu yanakuja tar 16.

........mwigulu.mwigulu,mwigulu,ungekuwa na hekima na busara,ungefanya kampeni za kistaarabu.Siwezi kukutofautisha na kobe juu ya mti,huwezi kupanda wala kushuka.Kwa kifupi nenda shule.......................
 

hv unajua gfsonwin nakuheshimu sana, ila eti wewe ni damu moja na lile lidubwasha la mafisadi naona unanitesa sana!
 
Last edited by a moderator:
Hivi wewe Kabinti unamlengo gani mbona cjawahi kuona post yako ikiunga chochote na kupinga kila kitu na vyama vyote unavipinga unda chama ili uwe unakiunga mkono
 
Acha kuleta propaganda zako hapa.
Wewe kila siku unasema tukabiliane na CCM, Tupigane nao na tujilinde huku ukiambia wenzako wawe mstari wa mbele lakini cha ajabu katika misukosuko yote ambayo viongozi, wanachama na wapenzi wameisha pata since 1992 hujawahi hata mara moja kukamatwa achilia mbali kujeruhiwa.

There's something FISHY in you ikichukuliwa wewe ndiyo huwa wa kwanza kwenda mahakamani kushuhudia kesi za viongozi, wanachama na wapenzi wa CDM huku ukirusha LIVE kutoka mahakamani.

Kama kweli una msongo wa kuipigania CDM, kwa nini hujawahi hapa kukamatwa, kupigwa au kupelekwa mahakamani?.

Hii tetesi za u-DOUBLE AGENT kukuhusu wewe inawezekana zikawa ni kweli.
 
Wana jf nimefanya mikutano mitatu mpaka sasa hakuna hata mkutano mmoja nimepatwa na kelele ya aina yeyote. Anayedhani kuna mkutano nimezomewa aendelee kuamini hivyohivyo, majibu yanakuja tar 16.

Kwa akili hii ya utawala ni hatari,
kuwa makini si vyote vinavyosemwa ni lazima ukanushe na kupiga kelele, sometime pita kama msomaji tu utajijengea heshima!

Kwa nn hujifunzi ndg unawaangusha hata wenye mapenzi mema na CCM!

akili kama hii ni hatari hata katika utawala.

Poor management knowledge!
 
Kwa hiyo unamaanisha we ni zaidi ya mwenyekiti wako ambaye amesha zoea kuzomewa
 
Yaani ulienda kufanya mkutano ukitegemea kuzomewa? Kweli wewe na CCM yako hamnazo. Kiongozi unategemea kuzomewa ina maana unajua kuwa unaongea pumba
 
Yani ovyo kweli! Unajitapa sasa au? Badala ya kuleta uzi wenye tija unaleta mambo ya kuzomewa! Rubbish kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…