LEO BUNGENI DODOMA - Bajeti ya Wizara ya Kilimo

LEO BUNGENI DODOMA - Bajeti ya Wizara ya Kilimo

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
3,119
Reaction score
1,428

LEO BUNGENI DODOMA - Bajeti ya Wizara ya Kilimo

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, ameelezea umuhimu wa uanzishwaji wa Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji ndani ya Bonde la Bugwema la Jimboni mwao.

Mbunge huyo ameeleza mengi, yakiwemo yafuatayo:

(i) Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kufufua Mradi huo uliodumu kwa miaka zaidi ya 50 bila kutekelezwa

(ii) Mazao makuu yatayolimwa kwa umwagiliaji ni: mpunga, mahindi, alizeti, choroko, kunde, mbaazi, maharage na pamba

(iii) Ziwa Victoria lina umri wa takribani miaka 400,000 na umri wa Mto Nile ni takribani miaka milioni 30. Kwa hiyo, kilimo cha umwagiliaji kiendelee kwani Mto Nile ni mkongwe umekuwepo kabla ya kuwepo kwa Ziwa Victoria

CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa:
Tafadhali sikiliza mchango wa leo Bungeni wa Prof Sospeter Muhongo

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Alhamisi, 22 May 2025
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2025-05-22 at 16.31.55.mp4
    15 MB
Back
Top Bottom