Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Usitumie nguvu sana kumwelewesha mtu mzima had mmeo akaingilia. Kumbuka wanaume tuna huruma sana na vibinti vya umri huo ukivionea huruma ukajidai kuvitetea vinahisi umeisha vitaman vinazidisha majaribu.
Sasa chakukushauri japo kinaweza kuonekana cha kijinga kama haelewi nini unamfundisha mshonee sare special kwaajiri ya kufanyia kazi na umununulie nguo nyingne (ili kuonesha humkomoi) za kutokea, umwambie wakati wa kaz ni lazma awe kwenye hiyo sare yake ya kaz ila wakati hana kaz ni ruksa kuvaa nguo yoyote atakayo jisikia kuvaa.
 
Wewe ndio una makosa kumpangia muda au wakati wa kuvaa nguo ulizompa.
Mwache huru
Hapana kwa alivyonionyesheshea si anamshahara wake tu mkubwa atanunua huenda nikaepusha hizi dhambi ndogo ndogo nimefuta Mimi kumnunulia nje ya mshahara nikijua ataheshimu hata kidogo changu kwa kuniwazia kwamba kwa hiki kitu Cha thamani Nikichezea Dada atajisikiaje.Naacha Sasa nione Kama yeye akinunua nguo NZURI ataenda nayo bustanini
 
Habari waungwana.

Habari ipo hivi. Nyumbani tuna House gal ambaye Kama kawaida husaidia kazi za Nyumbani pamoja na kulea watoto .Sasa wkt anakuja nikagundua Hana nguo za kutokea kwa maana mfano kutokea tukienda mahali au akiumwa au akienda tembelea ndugu ZAKE weekend.

Nilichofanya nikampa nguo yangu moja NZURI ambayo hata Mimi ni zile za kanisani au kwenda sehemu special na pia nikamuongezea na za kushindia kwa maana za Nyumbani Kama anafanyafanya shughuli ndogo ndogo ,lakini wkt Nampa nilimfafanulia na Tena siku iyo nakumbuka alifurahi Sana na ni siku alikuwa anaenda kusalimia ndugu zake ilibidi avue Ile aliyokuwa ameivaa na kuvaa ile niliyompa akisema anashukuru Sana na ameipenda Sana .

Na alipovaa ni Kama alipimwa ilimpendeza Sana. Baada ya Kama wiki nikagundua Ile nguo ameigeuza ya kushindia na NDO anafanyia usafi.Nikamwita nikamwelekeza kwa Nini asivae zile zingine kwa maana Ile uwe Kama nilivyomuelezea.Akaelewa akaivua na kuifua.

Sasa Leo asubuhi naamka nikamkuta ameivaa anaifagilia nje na hata Jana yake aliivaa anamenyea nduzi(nikiongelea hivyo nduzi Zina utonvu na ni nyeupe) Nikamuuliza mbona umerudia kuifubaisha nguo NZURI na nilikuelezea? Nikamwambia vua ntampa hata ndugu yangu atakayeithamini.

Sasa Baba watoto akasema Kwanza Iyo nguo kumpangia masharti aivae vipi umekosea kwa kuwa wakati unampa hakukuomba ulimpa mwenyewe na kanuni ya kumpa mtu kitu chochote ukishampa umempa matumizi ni juu yake hata angeamua kudekia kufanyaje ni yeye maana imekuwa yake.

Kweli Kama mama nimeshangaa Sana kwa hizo kauli. Je Mimi makosa yangu ni yapi au ni kweli mtoto ndani ya nyumba hupaswi kumshauri(Huyo msichana Ana miaka 18 kwenda 19) Na ikumbukwe ni mista huyo huyo aliyenilalamikia kwamba huyo msichana tangia aje anavaa vinguo vyepesi na khanga tu akijua na yeye yupo kwa maana Kama Ana majaribu na akimfananisha na dada mwingine ambaye aliondoka ambavyo hakuwa na majaribu Kama ya huyu wa Sasa kwa maana kujipitisha Mara kajilaza ovyo Yaani Mambo Kama hayo.

(Kwa hayo malalamiko yake nikaongea na Dada nikamshauri jinsi ya kuvaa na hasa azingatie nguo za heshima.Walau akabadirika.
Sasa Leo NDO hayo.

Naombeni maoni na mista atawasoma Mana kajaa tele humu
Umefanya kosa kubwa kumpangia matumizi,kwa utaratibu wa kusaidia si vizuri ukapanga na msaada wa matumizi hasa hasa nguo.
Kama umempa muache atumie kwa utaratibu aupendao,nafikr kwa upande wake anaona inampendeza zaid akivaa wakat akidek kuliko kutokea.NI VIZUR UKAHESHIMU MAAMUZI YAKE.
 
Kwanza mtag huyo mista tumsikie na yeye..
 
Ushampa ni yake usimpangie

Anyway nenda kariakoo mnunulie madira kama 5 mpe avae
 
Dada naona mada yako inakupa stress tena maana watu wameelewa tofauti na ulivyokusudia, pole.

Nafikiri kama umemchukulia huyo msaidizi wako kama mtoto au mdogo wako, una wajibu wa kumuelekeza tena mkiwa wawili.

Unapokosea ni kutaka kulazimisha na mr. Ahusike kwenye kumfundisha hapo unafeli pakubwa sana na wanaume tuna utaratibu wa kuchukulia vitu kawaida sana unaweza ona jambo ni kubwa sana ila hata halitushitui kabisa.

Muelekeze vizuri tu kuwa nguo hiyo aitumie kwa mtoko, yawezekana hata namna unamuelekeza sio nzuri ndo maana binti hakuelewi.
Nashukuru Sana.Bahati NZURI Nina miaka Kama 10 na zaidi humu JF KUNA watu wengi wema Sana na waelewa na pia KUNA wavutq bangi vilevile NDO Mana huwa nawachukulia hivyohivyo maana utabishana na mvuta bangi mbichi iliyosagwa utamuwezea wapi.Nilimwelekeza vizuri tu Tena tukiwa wawili.Ila pengine hakunielewa Mana ni mzito kidogo
 
Umefanya kosa kubwa kumpangia matumizi,kwa utaratibu wa kusaidia si vizuri ukapanga na msaada wa matumizi hasa hasa nguo.
Kama umempa muache atumie kwa utaratibu aupendao,nafikr kwa upande wake anaona inampendeza zaid akivaa wakat akidek kuliko kutokea.NI VIZUR UKAHESHIMU MAAMUZI YAKE.
Usikute dada wa watu anaichukulia poa nguo, kumbe maza mjengo anaiona classic sana.

Kwa kweli, aheshimu maamuzi ya mdada wake.
Maana anachokifanya ni makelele yasio na ulazima n mwishowe yatakuja kumjengea kiburi huyo mdada.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Nimechekaa maana dada ameona hiyo Nguo ni ya kushindia nyumbani wew unamwambia ya Kutokeaaa...!! Kiufupii bora usingempaa kuliko Kumpa alafu uanze kumpangia Masharti aivaee wapii na asiivae wapii...
 
Haina haja ya kumpangia mazingira ya kuvaa nguo uliyompa, kama hujapenda anavyoitumia ichukue tu nguo yako aendelee kuvaa nguo zake alizonazo. Ila usimwache avae vikanga wakati mista wako anashinda nyumbani maana ndo mitego pekee inayotumiwa na dada wa kazi kuwamiliki baba wenye nyumba.
Maisha ya sisi wanawawake tunaotoka asubuhi na kurudi jioni na wadada kushinda Nyumbani wkt mwingine Mista anaweza akawahi kurudi eti yeye kavaa khanga nyepesi.Sasa na hii ningeilalamikia Mimi wangesema Nina gubu au namuonea wivu.Bht NZURI alilalamikia yeye mwenyewe.Point ni kwamba si Nyumbani mwangu tu nimeona familia nyingi zikilia na mbwembwe na vituko vya wadada.Mfano inaweza tokea Mama wa nyumba hayupo Baba akawa amewahi Sasa msichana naye NDO kajiachia kwenye Sofa na sio kukaa kwa heshima Bali amejilaza miguu kule.Kama mtu amewahi ishi na Dada ataelewa KUNA muda wadada wa kazi ndio hutega maboss wa kiume .Sasa matokeo yake NDO hayo tunasikia radioni matukio ya kushtusha
 
Wamama sometimes mnapendaga vita visivyoisha aiseeee, Jamaa Yuko very right. Uliitoa kama sadaka, so kwanini umpangie? Umeshauri mara ya kwanza, hajabadilika, si ukae kimya? Why fighting over such petty issues?
Elli.
Sawa nimekuelewa Ila kujiepusha na hata sitampa au kumnunulia atajinunulia yeye mwenyewe kwa pesa zake.
 
Wamama wa kisasa mnapenda ligi sana hapo ujue ugomvi wote huo analengwa Mshkaji, Huyo HG ni kama chambo tu! Jamaa alikua anasubiriwa ajipendekeze abebeshwe lawama, nae kajichanganya kweli, zitaibuliwa shutuma na kesi kibao Hadi za tangu wa uchumba
Wala issue haipo hivyo.Kuna mtu hapo juu amesema aliwahi mpa nduguye jens kiroho Safi kesho yake akakuta kaikata pensi.Aliumia anyway walioelewa wameelewa na wasiolewa hawataelewa
 
Kuna wanawake ni Wagomvi tu kwa asili, sasa unaamka asubuhi unawaza vile siku itaenda, Kuna ada, Kuna mlo, Kuna ujenzi, Kuna Kodi pengine Kuna na mchepuko, kazini kwa moto halafu ghafla unadondoshewa Kesi Ya Housegirl, hahahaa jioni unaweza usirudi kwako
Haaaa haaaa haaaaa jamani
 
Lazma ifike mahari na sisi wabongo tubadirike. Tunapo ona wenzetu wafanyakaz wao wa ndan wana sare tusichukulie kuwa wao ni wajinga wanafanya vile kukwepa mambo kama aya.
 
Mi nilinunua jeans kali 25000 enzi hizo ikanibana kiuno ikiwa mpya kabisa nikampa ndugu yangu mtoto wa ba mdogo kesho yake akaikata pensi,
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23] dah sio ya kucheka ila
 
Bro samahani sana..ile jeans ilikuwa lonyalonya sana nikaiona niikate pensi..Nitakununulia nyingine basi.

Kidding.
Haaa haaaa unajua hii issue kwa wengine Haina maana na wanaweza ona ni issue na sisi kina mama but in real life ande sense sisi wamama tuna Ile nature yetu ya kitu chetu kizuri unatamani Sana na mwingine ule uthamani wake sijui ni kwa Nini hata mfano KUNA T shirt moja NZURI Sana nilimnunulia mista alivyovaa mwenyewe akasema hii umenipatia tofauti na zingine Ila Ina rangi rangi za Simba ye Yanga Damu.Siku zikapita nikamkuta nayo Shambani anakatia migomba(nguo nyingi havai sababu Zina madoa hayo hayo ya ndizi utonvu.Niliumua why nilipenda AKITOKA avae sio kwenye kazi za hivyo Point NDO iyo jamani
 
Lazma ifike mahari na sisi wabongo tubadirike. Tunapo ona wenzetu wafanyakaz wao wa ndan wana sare tusichukulie kuwa wao ni wajinga wanafanya vile kukwepa mambo kama aya.
Thanks a lot.Said it all.
 
Back
Top Bottom