Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Kuna wanawake ni Wagomvi tu kwa asili, sasa unaamka asubuhi unawaza vile siku itaenda, Kuna ada, Kuna mlo, Kuna ujenzi, Kuna Kodi pengine Kuna na mchepuko, kazini kwa moto halafu ghafla unadondoshewa Kesi Ya Housegirl, hahahaa jioni unaweza usirudi kwako
 
Umesoma vizuri toka mwanzo?kwa Nini Kama ni hivyo huwa watoto wakitoka na nguo kanisani au na nguo special mahali husema vua Kwanza hiyo nguo Na Mimi sijamchukulia Kama mtu Bali au jirani au mtu nisiyekaa Naye na sijawahi mwambia asivae Ila asiifanyie kazi mfano wkt anafagia au wkt anamenya ndizi.Na wkt Nampa nilimwambia hii ya kutokea .

Na SIO hivyo tu nikamuongezea zingine za kufanyia kazi asubuhi kwa maana hata akivaa iyo nguo Nyumbani wkt hafanyi zile kazi za kuifubaza Haina shida.Nikisema kuifanyia kazinunaelewa NDO Mana hata shambani KUNA nguo zake usijifanye hujaelewa
Nimekuelewa vizuri sana

Miaka 18 huyo sio mtoto huyo ameshaanza kupevuka kitambo na Asha develop feminine character Kama kutaka kupendeza kama ameipenda nguo mwache aivae kwa nini umpangia kwani yeye hajui hana nguo za kutokea sana sana ataona unamnyanyasa na unamnyanyasa kweli

Wapangie watoto wako wadogo nguo ulizio wapa halafu mimi ninavyojua watoto wadogo ndio wanapangiwa nguo za kuvaa hasa wale wa chekechea au hata la kwanza

Hawa wengine wanavaa watakayoipenda kwa siku hiyo ili mradi wanafua wenyewe na nguo ni safi na zenye heshima
 
Mkuu acha ujuaji. Wewe unataka ushauri au umetaka kubishana?? Mumeo yupo sahihi. Ukizidi kumbugudhi na hoja zako hizi atakuwa haivai kabisa halafu utaanza kumuuliza mbona nguo niliyokupa huivai??
Point yangu asiivae wkt wa usafi wa asubuhi basi
 
Nimekuelewa vizuri sana

Miaka 18 huyo sio mtoto huyo ameshaanza kupevuka kitambo na Asha develop feminine character Kama kutaka kupendeza kama ameipenda nguo mwache aivae kwa nini umpangia kwani yeye hajui hana nguo za kutokea sana sana ataona unamnyanyasa na unamnyanyasa kweli

Wapangie watoto wako wadogo nguo ulizio wapa halafu mimi ninavyojua watoto wadogo ndio wanapangiwa nguo za kuvaa hasa wale wa chekechea au hata la kwanza

Hawa wengine wanavaa watakayoipenda kwa siku hiyo ili mradi wanafua wenyewe na nguo ni safi na zenye heshima

Mit 25:24 SUV​

Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
 
Naomba Soma maelezo vizuri.Hata angeivaa siku zote Haina neno NDO Mana hata Jana baada ya Mimi kutokea kazini aliivaa na Wala hakuwa na shida na ni Mimi nilimwambia SIO kwamba ukiwa Nyumbani NDO usipendeze hapana.Nina maana unapoamka Nyumbani KUNA kazi nyingi mfano sisi tuna mpaka Bustani garden ya maua Sasa zile kazi kazi za asubuhi Kama ni nguo NZURI lazima isidumu au inafubaa.Na.wkt Nampa nilimwambia na nikampa na hizo za kazi pia mwenyewe anazo.Sijasema asivae
Nasaha zangu zilibase kwa mumeo na stara, hilo la nguo kweli lazima awe na nguo ya kufanyia vishughuli vya hapa na pale na za kutokea au za kumfanya asiwe tofauti na wale wa humo ndani.
Ila stara muhimu ni mikao isiyoeleweka ni mwiko
 
Kwamba umempa nguo nyingi ila ya kutokea special ndo umempa hiyo moja tu?
Halafu ni mfanyakazi wako?
Hapana kuwa wazi dadangu ni hivo tu ndo umekuja fungulia uzi kisa nguo tu uliyompa?

Mie nasema kuna kingine labda.HAIINGI AKILINI KABISAAA labda uwe mchoyo .
Hapana kwanza Ana mwezi mmoja NDO kwanza nimempa mshahara wa kwanza.Na iyo moja nikawa tayari kumshonea kwa fundi zingine za kutokea hii nje ya mshahara.Ndo Mana nikasema KUNA wkt anaweza hata akaumwa Basi asivae zilezile za kushindia au za kufanyia usafi.Awe nazo NZURI hata 5 na haimaanishi zote kimuonekano ni mbaya hapana Ila nikisema special unaelewa
 
Mi nilinunua jeans kali 25000 enzi hizo ikanibana kiuno ikiwa mpya kabisa nikampa ndugu yangu mtoto wa ba mdogo kesho yake akaikata pensi,
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🙌
 
Nachukia sna mwanamke wangu kuanza makelele na HG
Kwa hiyo hata akikosea anyamamaze asimrekebishe?mbona mfano nyie wenyewe unaweza kuta Mista labda aliwahi kutoka kazini akakuta Dada akaacha tu maji yanachemka kwenye gesi au hajafunga bomba vizuri au katoka kaacha nyumba wazi anakushtakia why asinyamaze.Haya Mambo ya kurekebishana ni kawaida ili Mambo yakae sawa.Na si makelele na sidhani Kama mtu anaweza amka akaanza kupiga tu makelele.

Mfano mbali na mengine msichana wangu Mimi huyo ni msahaulifu Sana hawezi kwenda Dukani mpaka umwandikie hata Kama ni vitu vichache la sivyo atarudi bila vitu vilivyokamilika au unamwambia asubuhi pasha chakula NDO uendelee na kazi nasahau vyakula vinachacha mnamwaga .Kwa hiyo KUNA muda unaacha au unapasha mwenyewe Sasa Kama unawahi Sana kazini NDO inakuwa hivyo.
 
Nje ya box.

Ninavoona kwa umri wa 18yrs huyo ni mtu mzima. The fact kua hakua na nguo ni sawa, but nadhani the best approach ungetoa nguo zoote unazotaka kumpa alaf yeye achague ipi anataka au hataki. On top of that, ungemuuliza ipi anadhan inafaa kutokea na ipi ya kushindia, then hapo maybe umuongezee ushauri.

We differ in perspective, we unayoona ya kutokea, kwake anaeza hisi haimpendezi na huwez badilisha hilo. Women hua wana insecurities kibao about theor bodies. Hyo nguo yaeza kua nzuri but yeye anaona inamfanya maybe manyonyo yaonekane vbaya n.k.
Kuhusu huyo mista, hili suala usingehangaika nae maana sisi wanaume tunaamini wewe ndo waziri wa ndani so kuna vitu you solve them hasahasa mambo yanayohusu wanawake kama beki 3 aliepo.

Muhim mkazie beki 3 awache kukaa kihasarahasara mbele ya bwana ako. Kaa ukijua, HUEZI KUTUMIA MUWA KAMA FIMBO YA KUTEMBELEA, LAZMA UTAULA TU.
 
mpe na nguo za ndani halafu muulize mmeo kama anazivaa inavyotakiwa
Hawa NDO Aina ya watu tunaotegemea wawe wakuunwa wilayana akina Kasesela sawa nitampa Wala hakuna Shaka.Ushauri mzuri
 
Kumpa mtu kitu na kuendelea kumpangia matumizi nacho ni masimango,,. Umemwambia haelewi achana nae mumeo anaona unamsimanga binti wa kazi

18-19 Yuko kwenye foolish age,, ununda na ujinga mwingi,, akikukosesha amani sana mrudishe alikotoka,,
 
Mtoa mada mimi nimekuelewa.
Uliamua kumpa nguo ya kutokea baada ya kuona hana nguo za kutokea nzuri. Na wewe ulitaka akiwa anatoka apendeze.

Kuhusu kumpangia aivaaje ni sahihi pia, huyo ni kama mtoto wenu. Mkitoka pamoja yeye amevaa hovyo aibu ni yenu. Ni sawa mtoto wako umnunulie nguo za kutokea halafu ageuze za kushindia siku anaumwa bahati mbaya hana nguo inayotazamika ya kumpeleka hospital. Hiyo itakuwa ni aibu yako.

Binti wetu wa kazi nilimnunulia nguo za ndani 12 awe anabadilisha maana alikuja na moja. Lakini kila akioga sioni akianika nguo. Kila baada ya wiki utasikia dada nawashwa huku nawashwa huku. Mkienda hosp ana fungus na UTI.

Sasa siku nimeingia ndani kwake nakuta chupi 11 bado mpya hata label hazijatolewa maana yake hazijawahi valiwa. Sasa huyu shost kumbe yeye anavaa moja tu, akioga anaivaa hiyo hiyo ikichafuka anafua anaivas ikiwa mbichi. Halafu anaumwa mnasumbuka kutibu fungus zisizopona na uti sugu.

Sasa hapa mtasema tumeshamnunulia yeye akiamua abadilishe asibadilishe ni yeye?

Nikirudi kwako mtoa mada, upo sahihi sana huyo ni binti yako maana unaishi nae na unamlea. Akiwa hovyo wewe ndio utasemwa kwa hiyo una haki ya kumchagulia hii nguo ni ya kutokea hii ni ya kushindia. Maana akitoka out yupo hovyo mtaonekana hamumjali.

Na pia japo wengi wanasema ukimpa mtu kitu mpe usifuqtilie anatumiaje ila hamna kitu kinauma umempa mtu kitu unachokithamini halafu anakitumia ndivyo sivyo jamani. Roho lazima iume.
 
Back
Top Bottom