Kada maarufu wa CCM ambaye pia ni mbunge wa Kahama na mwenyekiti wa kamati ya Maliasili na utalii, Dr James Lembeli ametahadharisha kwamba kitendo cha Prof Muhongo kutowajibishwa au yeye mwenyewe kutoachia madaraka kwa hiyari, kitaiua CCM kabla hata uchaguzi wa mwaka huu haujatangazwa.
Kada huyo amemtaka rais kikwete kumfuta kazi muhongo ili kuinusuru CCM na chuki dhidi ya wananchi na hatimaye kufa kabisa baada ya kushindwa vibaya kwenye uchaguzi wa oktoba, 2015. Ametolea mfano wa Mwinyi na Lowasa waliowahi kuachia ngazi na hivyo kumshauri mhongo afuate mkondo huo endapo JK atagoma kumfuta kazi.
Chanzo: Nipashe
:israel:
Lembeli anamalizwa na maige anaepita kwa wapiga kura kuwaambia alichongewa na lembeli eti kaiba twiga, Maige anawauliza wananchi kuwa mnamfahamu twiga wanasema "ndio", unaweza kumswaga "hapana" sasa atamwibaje? wananchi wanaitikia hizo ni fitina.