Kada maarufu wa CCM ambaye pia ni mbunge wa Kahama na mwenyekiti wa kamati ya Maliasili na utalii, Dr James Lembeli ametahadharisha kwamba kitendo cha Prof Muhongo kutowajibishwa au yeye mwenyewe kutoachia madaraka kwa hiyari, kitaiua CCM kabla hata uchaguzi wa mwaka huu haujatangazwa.
Kada huyo amemtaka rais kikwete kumfuta kazi muhongo ili kuinusuru CCM na chuki dhidi ya wananchi na hatimaye kufa kabisa baada ya kushindwa vibaya kwenye uchaguzi wa oktoba, 2015. Ametolea mfano wa Mwinyi na Lowasa waliowahi kuachia ngazi na hivyo kumshauri mhongo afuate mkondo huo endapo JK atagoma kumfuta kazi.
Chanzo: Nipashe
:israel:
Eti Limbeli Amemtaka Rais kutekeleza matakwa yake? Kwani Limbeli ni Amiri Jeshi mkuu na Rais wa Dunia? anamtaka Rais atekeleze Amri yake kama nani? Pesa alizopewa na Mengi zimemzuzua mpaka anaropoka pasipo kutafakari kama Mvuta Bangi Lema.