Lembeli: Muhongo anaiangamiza CCM

Lembeli: Muhongo anaiangamiza CCM

CCM mnashangaza sana. Mtu anayesema ukweli mnamkejeli na kumuona hana maana. Ila wale mafisadi ndio mnawaona wana maana. Chama kinazidi kujifia.

Lembeli ni matehemu anayetembea mtakumbuka maneno yangu punde twendeni sawa atalia sana mwaka huu hata iweje hatoki.

hayo makapi ya kutoka CCM kama linataka kuja huko na lije tu , Muhongo ni mmoja wa watu ambao watanzania tulikuwa tunawahitaji muda mrefu sana, acheni wivu wenu.

Ni tusi kubwa sana mtu kudhani mimi ni ccm!
 
Dr. James Lembeli si nimemuona kwenye picha anaendesha Chopa aliyopanda Mwigulu Nchetemba
 
JK ni jembe maneno yote haya ni ya kumgwaya tu na si vinginevyo, mtamkumbuka sana baba wa demokrasia afrika nzima, enzi za Mkapa mlikuwa hambwabwaji hivi
Mkapa alikuwa dicteta ila si fisadi, sasa kikwete ni demokrasia lakini Fisadi, pia Ikulu ilikuwa inaheshimika sasa ikulu pango al wezi
 
Umeongea kweli Mh.Lembeli Lakini anayeiuwa ccm si Mhongo pekee yake, zaidi sana anayeiua ccm ni Rais wako, kama unavyoona hata wewe msema kweli hakupendi, ila anawapenda mafisadi
 
kabla ya Muhongo hao TANESCO hawakuwepo, mbona ilikuwa ni ndoto umeme kwenda huko vijijini
Jamani mbona hamwelewi Mhongo na Jk Ni wamoja katika Ulaji ndo maana jk hawezi kumtosa mwenzie abaki kwanza ili waendelee kuchukua kila kitu hujui wanamaliza kipindi
 
Kada maarufu wa CCM ambaye pia ni mbunge wa Kahama na mwenyekiti wa kamati ya Maliasili na utalii, Dr James Lembeli ametahadharisha kwamba kitendo cha Prof Muhongo kutowajibishwa au yeye mwenyewe kutoachia madaraka kwa hiyari, kitaiua CCM kabla hata uchaguzi wa mwaka huu haujatangazwa.

Kada huyo amemtaka rais kikwete kumfuta kazi muhongo ili kuinusuru CCM na chuki dhidi ya wananchi na hatimaye kufa kabisa baada ya kushindwa vibaya kwenye uchaguzi wa oktoba, 2015. Ametolea mfano wa Mwinyi na Lowasa waliowahi kuachia ngazi na hivyo kumshauri mhongo afuate mkondo huo endapo JK atagoma kumfuta kazi.

Chanzo: Nipashe

:israel:
Huku ndiyo kupishana kwa lugha kwa watawala Askofu wa FGBF alisha semaAlitamka.Tunayaona sas wanapishana wao kwa wao, dhambi inawatafuna wenyewe na bado muda unakaribia
 
kabla ya Muhongo hao TANESCO hawakuwepo, mbona ilikuwa ni ndoto umeme kwenda huko vijijini

Ndoto labda ya kwako. Ukweli habari ya REA ni ya kila MTanganyika kwa kuwa yako makato yanafanyika. Tatizo watu hawafahamu wajibu wa serikali kwao. Waziri mwenye dhamana akifanya kile anachopaswa kufanya watu wanadhani amewasaidia. Ndugu hiyo ni haki yako kama mwananchi na mlipa kodi na makato mengine. Mbona madaktari wanaopasua watu na wauguzi wanaozalisha hawasifiwi? Watanganyika yuache ushamba. Fahamuni hata kufuatilia kama watendaji kwenye mikoa na halmashauri wametekeleza majukumunyao huyo prof. Mwongo alitumia fedha ya serikali. Sasa hizi sifa ni za nini? Au kuna mgawo wa eacrow? Tuambizane ukweli.
 
Mwacheni Muhongo achape kazi.Lembeni akapumzike tangu amekuwa Mbunge amewafanyia nini watu wa Kahama?

usiwe mgumu wa kuelewa. kuchapa kazi kwa muhongo sio tatizo ila uchapa kazi una negative effects kwa CCM. sasa kama unaona hiyo effect ya ufisadi wa muhongo haina madhara kwa CCM, mwache aendelee kuchapa kazi.
 
Ni wazi Muhongo na JK hawakukutana barabarani........ Mbona wanapendana hivi,Yani JK yupo radhi CCM ife lkn sio kumtoa Muhongo............mahaba ya dhati.

jk na rugemalira pia hawajakutana barabarani. ndio maana wapokea rushwa wanafikishwa mahakamani wakati mtoa rushwa (ruge) anadunda mtaani. maCCM ni viumbe wa ajabu sana.
 
Tena liondoke saa nane za usiku ili liondoke na nuksi zake zote anadhani kuwa na nywele nyeupe ndiyo kupewa uwaziri jk haangalii nywele bali anaangalia uwezo.

tatizo maCCM hampendi mtu anayewasahihisha au anayewashauri muacha UFISADI. hili ndilo tatizo lenu kubwa.
 
usiwe mgumu wa kuelewa. kuchapa kazi kwa muhongo sio tatizo ila uchapa kazi una negative effects kwa CCM. sasa kama unaona hiyo effect ya ufisadi wa muhongo haina madhara kwa CCM, mwache aendelee kuchapa kazi.
Watu wamepmbqzwa akili na ccm
 
lembeli anasumbuliwa na frustrations, miaka yote ya ubunge hata nyumbani kwake hajafanya kitu achilia mbali kwa wananchi wake. Anatumiwa na Wapinzani ili kudhoofisha majembe ya JK ili CCM ionekane haijafanya kitu

mtu yeyote anayewapa ushauri CHANYA na kuwasihi muache UFISADI ametumwa na UKAWA? kweli nyie mmerogwa, sio bure!
 
Back
Top Bottom