Lema kuwatoa wafungwa gerezani

Lema kuwatoa wafungwa gerezani

ngurati

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
221
Reaction score
240
Natokea kisongo saa hii kumuona Lema, nimemkuta akinyoa nywele na still ana furaha utadhani yupo uraiani. Miongoni mwa mambo aliyoyakuta ni idadi kubwa ya wafungwa waliopo ndani eti kwa sababu walishindwa kulipa faini kesi zao, faini hizi sio kubwa na pia zimepungua kwa sababu tayari wameshatumikia miaka kadhaa ndani.

Lema ameandija barua tayari na imeshapokelewa na mkuu wa gereza, mahesabu yanapigwa na kesho hesabu itafika ili walipiwe hizo faini na watoke.

Hizi ni faini Kama za laki 1, 2, elfu 50, laki tano, etc. Lakini wana Kama miaka Tisa, 5, 6, 11 etc.

Kuna mzee Ana miaka 85 kapewa kesi ya kubaka kafungwa miaka 30 na anasema hakuwahi kubaka, na kamwambia Lema Hana hata uwezo wa nguvu za kiume, Ila alisingizuwa kesi kwa sababu ya mgogoro wa ardhi.

Kuna kesi nyingi zenye utata lakini watu wamo gerezani. This week watatoka over 40 kwa msaada wa Lema.
 
Maelezo mengine yanasema Mh. Lema amewekwa kwenye chumba cha peke yake; hayo unayoyaandika ameyapataje?
 
Rais anaweza kuzuia mfugwa yeyote asitoke gelezani --- sheria / katiba yetu inamruhusu.
 
Siyo siri kwamba una haki ama hauna, bongo anayeamuwa hilo ni polisi na wanasiasa walioko madarakani.Haki yako haitokani na katiba na sheria za nchi,haki ya mtanzania inategemeana na utashi wa watawala!

Hili suala la kubambikiziwa kesi mbona tulishazoea kabisa?

Kuna watu wenye pesa ambao walishawahi kuhukumiwa miaka mingi kutokana na makosa yao,lakini amini usiamini.polisi huwa wanaenda mtaani kukamata mtu,anapewa hiyo kesi na anatumukia miaka ya huyo aliyehonga amabye anaachiwa.

Amabalo silijui ni hapo kwenye majina na document kutoka mahakamani kuwa kama ni kweli aliyeshitakiwa ndiye anatumukia kifungo hicho.

Pia kama kuna ujambazi ambao askari wameshiriki ama mkuu wao kahongwa,basi hiyo kesi ili iweze kufungwa,lazima apatikane mtu wa kubambikiziwa hiyo kesi na kuhukumiwa ili tu wafunge faili.

Nina uhakika kabisa kuwa wengi wasiokuwa na makosa wako ndani jela na wale wenye makosa wako nje.Wenye pesa hawakai ndani,na wenye connection na polisi ama wanasiasa pia hawakai ndani.

Na hata kama wakipata kesi,polisi wanaenda tu mtaani kuokoteza raia,na kuwapa hizo kesi ili kufunga mafaili na kuwafumba macho wananchi.

Na mara nyingi kwasababu polisi huwa wanaonekana wamefanya kazi nzuri mara baada ya kusolve kesi na kufunga jalada,basi huwa wanafanya hivyo kwa kwenda kuokoteza watuhumiwa na kuwapa kesi zilizoko kwenye makabrasha huko polisi na wanawapelekea watu mahakamani kwa kesi ambazo siyo zao.

Hili ni la kawaida kabisa bongo,nashangazwa kama kuna ambao hawajui!

Haya yote yanayotokea ni mambo amabyo ni ya kawaida sana bongo,na wengine yalishatuchosha kabisa na ni rahisi sana kujutia kuzaliwa Tanzania!

Sioni ni kwa njia gani tunaweza kumove forward bila mapinduzi,mfumo mzima ni hovyo bongo,na kupigia kelele Arusha peke yake siyo solution bali ni mwanzo tu,ni wananchi wachache sana wanojuwa haki zao na hata wale wenye kuzijua,ni wachache sana wanaamini kuwa zitakaa zipatikane bila rushwa nk....ni maoni tu.
 
Rais anaweza kuzuia mfugwa yeyote asitoke gelezani --- sheria / katiba yetu inamruhusu.
MJOMBA RAIS HANA MAMLAKA YA KUMFUNGA MTU SHERIA NDO INAMAMLAKA NA VILE VILE RAIS HANA MAMLAKA YA KUMZUIA MFUNGWA YYT ASITOKE GEREZANI SHERIA NDIO ITAZUIA lkn kwa serikali legelege na yakifisadi ya Tz yote yanawezekana ht kuua ruksa! Binafsi nampongeza sn mh.

G.Lema kwa ushujaa na uzalendo aliofanya na kama pesa zitampungukia asisite kurudi kwa wananch kutueleza, tutachangishana fasta kuwakomboa watanzania wenzetu. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MBARIKI LEMA, MUNGU IBARIKI CHADEMA,
 
Maelezo mengine yanasema Mh. Lema amewekwa kwenye chumba cha peke yake; hayo unayoyaandika ameyapataje?

Leo ni jumatano, ni siku ya kuwaona maabusu . Nimetoka kumuona na Mimi na viongozi wengine wa chama. Na maabusu sio Kama lock up. Tena tuliwekwa kwenye chumba tukazungumza kwa muda, sio kwenye wavu.
 
Rais anaweza kuzuia mfugwa yeyote asitoke gelezani --- sheria / katiba yetu inamruhusu.

Hapo kwenye red; you're right. Lakini unadhani ni sahihi? Well, utasema sheria zetu na Katiba vinamruhusu lakini bado ni sahihi kwa mtu mmoja kurundikiwa mamlaka na uwezo kama huo?

Mh. J. M. Kikwete ni rais lakini rais si Kikwete! Siku akiibuka mwendawazimu Ikulu hizo sheria tunazoshabikia leo kwa kuwa tu tuko madarakani au chama chetu ndicho chenye dola kuna siku zitatugeuka. Tume ya Jaji Mkuu Mtaafu Mh. Nyalali ilipendekeza sheria za aina hiyo zifutwe lakini kutokana viburi vya watawala wetu hadi leo hakuna kilichofanyika.

Taifa litadumu lakini sisi na vyama vyetu ni wa kupita - Tujenge mazingira bora kwa ajili ya Taifa letu na siyo kwa ajili ya makundi yetu.
 
Rais anaweza kuzuia mfugwa yeyote asitoke gelezani --- sheria / katiba yetu inamruhusu.
Ni kweli,na ndiyo maana tunataka mabadiliko ya katiba....Na pia ndiyo maana atakuwa responsible and accountable for almost everything.
 
Maelezo mengine yanasema Mh. Lema amewekwa kwenye chumba cha peke yake; hayo unayoyaandika ameyapataje?

Na wewe hayo maelezo /taarifa umeipata wapi? Huko ulikopata wewe ndo alikopata hizi taarifa
 
Sipati Picha Hiyo Siku Kamanda Anatoka؛....
 
Hivi wewe unaijua bongo au unaisikia redioni. Kama yule fisadi dagaa wa BOT ameweza kuwa na simu Ukonga na kumtwangia fisadi mkuu, leo hii hata akiwa chumba maalum unadhani hawezi kukutana na wafungwa wengine ? Magereza kama ilivyo polisi, askari wadogo njaa zinawaua na wapo hoi bin taaban. I can see walio zamu usiku wakisaidia kuandaa mikutano, na hata kusaidia kufanya surveys gerezani ili mradi wanaona kuwa huyu ni mtu anayejali...!!

This boy licha ya kupakwa kuwa hana elimu, has really impressed me, na muvu zake ni za kuchungwa sana kwa anatengeneza kitu ambayo itaingia ktk historia duniani. Kuelimika sio darasani tu bana, ona huyu maamuzi yake vs yale ya yule anayelazimisha kupewa PhD za dezo dezo wakati kila miezi 3 inabidi akapimwe akili nje ya nchi !!

...Ndiyo maana hao askrai wa chini hata kati wanampa siri za muvu zote polisi wanazopanga maana bila hivyo wangeshammaliza siku nyingi. Watanzania wameanza kuamka.......magamba chunga sana siku ikifika nyie tutawafyeka kwa nyengo ktk masaburi yenu, mpaka mrudishe mali zetu zote mlizokwiba... !!
Maelezo mengine yanasema Mh. Lema amewekwa kwenye chumba cha peke yake; hayo unayoyaandika ameyapataje?
 
Safi Lema wewe ni mpiganaji wa ukweli na hakika ukombozi umefika Tanzania ,tupo na wewe muda wote kupinga dhuruma hii ya CCM.
 
Sijaelewa kitu kimoja..........hao unaosema atawalipia faini zao walizoshindwa kulipa wameshahukumiwa au ni mahabusu?
Kama ni mahabusu, amejuaje hukumu itakuwa faini?
Kama hukumu ilishatolewa.......1)Faini 100k 2) au kwenda gerezani 3months..............kama walishindwa kulipa, maana yake option ya pili inakuwa excuted kama adhabu sahihi...........na huwezi kufikia half way ukasema sasa nalipa faini nusu ili nitoke gerezani. Haipo hiyo.
 
Habari njema kwa watanzania wote wapenda haki na amani.
 
Back
Top Bottom