MTK
JF-Expert Member
- Apr 19, 2012
- 8,920
- 6,859
Wakuu salamaa?
Jana nimemsikikiza mh. Lema, akieleza juu ya sintofahamu ya kuvamiwa vituo vya police, kupigwa na kuporwa bunduki n.k
Kwa mshangao mkubwa akasema, Kamanda Changoja haamini kama rais kaishafanya uteuzi wa IGP na sasa anafanya sabotage to a new IGP ili aonekane anamapungufu kwa kuratibu matukio mbalimbali n.k
Ni kauli nzito sana, na matukio sasa ya aina hii ni mengi sana, tujadili pamoja kwa undani kama kuna kiukweli vile.
Mungu nibariki nifike December tu.
Kwa maoni yangu njia bora ni kutafuta audience na mtoa hoja; Mh. G J Lema ili atupe undani wa tamko lake; tunaweza kujadiliana lakini kimsingi tutakuwa tunajadiliana mitazamo na maoni yetu kuhusu swala husika; na kwa tabia ya baadhi ya wanaJF; mjadala huo utakwenda alijojo baada ya muda mfupi sana kwa watu kuanza kurushiana vijembe na mitusi na kujadili kwa misimamo ya vyama vyao nk nk; jambo ambalo halina tija hata kidogo!!
KYT: Baadhi yetu tunalifanyia kazi tayari; na itakapobidi tuta-share hicho tutakachokipata hapa jamvini; watch this space!!