Wajameni,
Ni muda mrefu umepita kuushuhudia umati mkubwa kama huu."There are currently 3660 users browsing this thread. (1140 members and 2520 guests)"
Ukiangalia idadi ya members na wasio members, wasio members ni mara mbili ya members, hii inamaanisha jf, inatembelewa zaidi na wasio members kuliko hata members, hivyo this jf is very powerful media!.
Asante kwa hukumu hii ya Lema, leo imetuunganisha na long lost friends tuliopotezana nao kipindi kirefu nyuma!. Kwa maoni yangu, kile kidole Lissu alichounyooshea mhimili huu wa mahakama pia itakuwa imechangia angalau kwa mahakama kuu ya rufani kuwathibishia Watanzania kuwa kuna wakati, wanaweza kutoa uamuzi wa haki!. Sijui kwenye ile kesi ya mgombea binafsi, walishikwa na kigugumizi cha nini!