Wana wa Nchi,
Nimshukuru sana Mwenyezi Mungu, Hatimaye Haki imependeka, mwaka 2010 nikiwa Mwenyekiti wa CHADEMA Arusha mjini chama changu kilinipa dhamana ya kuwa Meneja Kampeni wa Kamanda Lema, kazi ambayo niliapa kufanya kwa Moyo wangu wote, hali kadhalika nilipewa jukumu la kusimamia madiwani katika kata 18 ambapo nilishinda kata 8 na kupata madiwani 8.
Mwaka 2010 sikuwa na fedha za kupambana na CCM, waliotuchangia fedha ni machinga, mama ntilie na washikaji waliopigika kimaisha, hatimaye walipiga kura na kulinda ushindi hadi Lema akawa mbunge, kitendo cha Lema kuvuliwa ubunge kilikuwa ni dhulma kwa wanyonge wa taifa letu, baada ya mwenende mzima wa kesi na hatimaye rufaa Kamanda Lema amerudishiwa ubunge wake, nadhindwa kuzuia furaha yangu kwa kuwa kazi ya mikono yangu imezaa tunda jipya, hongera kamanda Lema, hongera Arusha, Hongera Chadema...
"KWA KUWA MUNGU YUPO UPANDE WETU HAKUNA WA KUMUOGOPA DAIMA"
AMNDLAA!!!!!!! AMANDLAAA
Kamanda Magoma Jr Magoma
M/Kiti Mstaafu Chadema Arusha.
Kampeni Meneja Arusha Mjini.