mwandiga
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 1,506
- 661
Takwimu za kijinga sana hizi. Waseme ngapi zimenunuliwa. Itakuwa mara mbili ya hizo. Ukifungiwa leo hapo hapo unanunua nne mpya. Waeleze wangapi wamekamatwa na kufungwa kwa utapeli wa kutumia simu. Kufungia tu haina tija yoyoteNimesoma kuwa line millioni 18 zimehusika kwenye uhalifu, sasa wahalifu wenyewe wako wangapi? kama kila mhalifu alikuwa na line mbili maana yake watanzania milioni kumi ni majambazi, yaani kila watu watano mmoja ni jambazi. kama ni kweli basi nchi yetu sio salama kabisa, kama jeshi letu lingekuwa imara maana yake hawa wote wangekuwa jela, je jela zetu zinao uwezo wa kuweka hawa wote, au tuje na mpango wa kujenga jela mpya, kwahili tunaomba ufafanuzi zaidi isijekuwa hii habari imetiwa chumvi
18, 000 SIM cards blocked in Tanzania
The government has blocked 18,622 subscriber identification module (SIM) phones that were found to have been involved in criminal incidents in the country.www.thecitizen.co.tz