Laana inavyomtesa mteule na rafiki wa Rais. Asante mama kwa simulizi, hii ewe mtumishi jifunze jambo

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
Nikiwa nimeshika zangu Mswaki, huku huku Mama mzaa Chema akiwa amejiinamia anakosha vyombo, mara gafla chema, Akaanza stori zake na mama yake!

Chema ;Ma hivi wajua yule mkurugenzi hajawai tuandikia hata barua za kututambua sisi kama watoa huduma wake kwenye wilaya yake?''

Ma:'' mmmh mpaka leo hajawai na watu mmeanza kufanya kazi mpaka vyombo vya habari vinawatambua jamani?"

Chema;" huwezi amini Ma Bado na hatumwelewi Huyu mkurugenzi,yaani anajioma huyu mtu jamani basi tu"

Mimi; hahahaa acheni hiyo kazi huyo ni shoga yake na Mama hamkumbuki madiwani wote walikataa kufanya nae kazi na bado hakutumbuliwa yaani nasikia ni chawa wa mama mbaya mno!

Chema; Weeeee sifi Leo unachekesha yaani tuache kazi wakati wizara imetuletea pesa Milioni 150,000,000/= tumeambiwa tubuni mradi fasta na tutarejesha hizo fedha."?mkurugenzi Huyu ana wivu na tumepata taarifa ya kuwa hizo fedha anataka zikiingia azipige akishirikiana na Maafisa maendeleo ya jamii sisi tunawacheki tu we ngojea hata kama ni chawa Ili litamuondoa."

Ahahaha hahahahaha hahahah gafla mama chema anachekaaaaaaaa kicheko Cha mtu mwenye jambo kichwani baada ya kicheko inakuka simulizi nzito.

Mama chema:" nyinyi hamumjui huyo bwana,mwenzenu Nina miaka miwili imebakia ya kusitaafu ila nawambieni huyo mkurugenzi hafai ingawa ni mteule wa Mama nawaasa ogopeni mtu mwenye Rahana iliyomtafuna kizazi!

Ebooooooooooo! Kidume nikashutuka gafla nikahoji yaani Ma,una maana Huyu jamaa Hana mtoto?(ghafla ilibakia kidgo nihoji au ni punga?).

Kiburi chote kile kweli Hana mtoto,kulinga kote uko Hana mtoto,hahahaha naisi atakuwa amejitoa kafara Huyu Ili Ikulu zimuone na kumteua!ahahahahah tunacheka wote ila Ma anaonesha yeye ana analo lijua hacheki kama Mimi na chema!

Ila umbea mbaya jamani huwezi amini sijui hata Mswaki niliuweka wapi kidume nimenogewa na umbea wa mama chema kudadeki na chema mwenyewe. Ghafla Ma anaanza vizuri

Ma;''wanangu katika utumishi wenu msiwaonee watumishi wenzenu kamwe, Huyu mkurugenzi alimuonea mtumishi mwenzetu, aliyekuwa anamuuguza mwanae

"Heheee,Tena,?"ndio Kuna mtumishi mwenzetu alipata dharula ya kuuguliwa na mtoto wake ikabidi aende kumuuguza sjui Nini kilijili ila yule mtumishi alimpoteza yule mtoto wake huki Huyu bwana mkubwa akimkalia KOHONI paspo kujali yakuwa mwenzake amepoteza mtoto Tena mtoto wake wa pekee.

Kutokana na zile stress yule mtumishi alimnenea maneno mabaya Huyu. Chawa wa Mama mpaka mnavyoona Leo Hana mtoto, na hatokaa apate mtoto labda amtafute yule Mama na kumwomba radhi Ili mama yule ambae Kwa Sasa ni mstaafu avunje Ile rahana la sivyo hata liteuliwe kuwa nani halitokaa lipate mtoto maisha!(ma kamaliza usia).

WITO; ewe mtumishi,au usie mtumishi usinyanyase wenzako maisha na hii Dunia tunapita rahana nyingine ni za kutafta ona sasa mteule wa Rais anavyo haha kutafta hata wa kusingiziwa yaani Huyu hata aweje hawezi toboa Dunia Isha mpindua.
 
IMG_0622.jpg

chawa wako wengi sana sijui ni yupi
 
Fafanua beans, kuanza Mambo ya mafumbo tena, Mara mama mzaa chema, Mara Mimi .NDIO NINI
 
Back
Top Bottom