Utingo
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 10,270
- 8,031
Rafiki yangu mmoja kanijia jana akiwa mwingi wa mawazo na majonzi tele
Kisa nini..Ni mwaka wa tatu sasa ameolewa hana mtoto ,Mama mkwe kapiga simu saa tano usiku kwa mwanae wakiwa wamelala
anauliza mkeo yuko hapo ? jamaa kasema ndio ..basi akaambiwa weka loud spika ili huyo anayejiita mkeo apate vidonge vyake
Mama mkwe bila haya kaanza kuporomosha mvua ya maneno akilalamika kama hajaolewa kuja kumchuna mtoto wao wamemsomesha ili awatunze wao na sisi yeye mke mgumba ..
Mbaya zaidi anamwambia ..hajaolewa ili awe sanamu ndani ya nyumba ..la sivyo wangenunua sanamu wakaweka ndani wanachotaka amzalie watoto kama hawezi njia iko wazi aondoke ..!
Mke kulalamika kwa mmewe ..
Mme anamjibu hii ni message send ..
Wanaume kwa nn mnaruhusu ndoa iingliwe na ndugu mke anyanyaswe kiivyo ?
kwa nini msitoe suport ili mke awe na uwezo wa kujitetea?
shock!!!!
FL
FL1 mshauri huyo rafiki yako akapime peke yake kama kweni ni tasa au la. Ikiwa si tasa ambembeleze mumewe wakapime wote. ili wajue pia hali zao. unajua siku hizi wanaume wengi wana matatizo ya uzazi sana. Mpaka hapo ndio ushauri wangu kwao.
Nimekutana na kisa kama hiki last two weeks, lakini baada ya kuwashauri hivyo walipokwenda kupima imeonekana mwanaume ana issue-mbegu zake ziko na shida-no mikia(whatever that means).
As a result ndugu wa mwanaume wamefyata mikia wamekuwa wadogo kama piriton. na man ameanza kuchukua hatua kuona kama anaweza kuremedy hali yake hiyo.
Please advice her that.
Ikiwa majibu kwake yatathibitisha kuwa yeye ni tasa mwanzoni kabisa, them by God's grace tutamshauri kwa hekima tulizojaaliwa.