Kwenu wanaume ...Hii imekaaje ?

Rafiki yangu mmoja kanijia jana akiwa mwingi wa mawazo na majonzi tele
Kisa nini..Ni mwaka wa tatu sasa ameolewa hana mtoto ,Mama mkwe kapiga simu saa tano usiku kwa mwanae wakiwa wamelala
anauliza mkeo yuko hapo ? jamaa kasema ndio ..basi akaambiwa weka loud spika ili huyo anayejiita mkeo apate vidonge vyake
Mama mkwe bila haya kaanza kuporomosha mvua ya maneno akilalamika kama hajaolewa kuja kumchuna mtoto wao wamemsomesha ili awatunze wao na sisi yeye mke mgumba ..
Mbaya zaidi anamwambia ..hajaolewa ili awe sanamu ndani ya nyumba ..la sivyo wangenunua sanamu wakaweka ndani wanachotaka amzalie watoto kama hawezi njia iko wazi aondoke ..!
Mke kulalamika kwa mmewe ..
Mme anamjibu hii ni message send ..
Wanaume kwa nn mnaruhusu ndoa iingliwe na ndugu mke anyanyaswe kiivyo ?
kwa nini msitoe suport ili mke awe na uwezo wa kujitetea?
shock!!!!
FL


FL1,

Wengine ni suruali tuu...kuruhusu ndoa kuingilkiwa kiasi hiki...hamna mme hapo.
 
FL1,

Wengine ni suruali tuu...kuruhusu ndoa kuingilkiwa kiasi hiki...hamna mme hapo.

Huyu Binti anavyodai anampenda sana mme wake na amemkalisha chini jana wameongea kajaribu kumuomba na yeye akapime .ila jamaa kang'ang'ania mwanamke ndio mgumba ?
swali la dharau binti anaulizwa na mmewe hivi wewe kabla sijakuoa umewahi hata kushika mimba mbona sioni dalili ??naona hapo kama si pa kukaa vile !!
 
Hapa bi mkubwa kachemsha!! Kwa kawaida wenye maneno huwa ni mawifi angalau inaleta maana, sasa mama mzima badala ya kumsaidia mkwewe kama ana matatizo yeye anaishia kutoa maneno makali kwenye loud speaker ya simu, mashaka matupu kwa busara ya huyo mama mkwe.

Haya ni mambo ya kitaalamu sio lazima tatizo liwe kwa mwanamke unless walikwenda kupima na kuthibitisha kwamba tatizo lipo kwa mwanamke, kina mama wengine hasara tupu.
 
Back
Top Bottom