Kweli leo nimekoma

Kweli leo nimekoma

Mkuu.. mlima Kilimanjaro unaonekana Asubuhi mda wa saa 11 mpaka saa moja. Baada ya hapo unafunikwa na mawingu. Unaweza pia kubahatisha kuuona mchana lakini ni mara chache na tena ni mda wa kiangazi tu. Ukifanikiwa kuuona unapendeza sana

IMG_1155.jpg


Hapa ni maeneo ya marangu.. Mda ilikua ni saa moja asubuhi
 
Wakuu salamu,

Ni hivi leo asubuhi baada kuwa off na kikazi ninachofanya hapa Arusha nikajisemea moyoni sasa ngoja niende Moshi nasikia ni fasta kutoka A Town ili nijionee Mlima Kilimanjaro kwa macho yangu.

Mzee mzima nikajikoki na ten yangu huyo kwenye coaster ili njia nzima mimi macho yangu yapo kodo kwenye madirisha nikijua tu nitaona mlima hola, mara KIA hapa nikasema sasa lazma itakuwa nakaribia kuuona mlima hadi moshi mjini Hola, nikazunguka zunguka bado sikubahatika mpka jioni.

Badala ya kuona mlima Kilimanjaro nimeambulia kula matunda tu na kurudi zangu Arusha.

Mpaka sasa sielewi kabisa mlima haonekani ukiwa Moshi Mjini sasa nitauonea wapi mie au mpka nirud kwenye atlas kweli.

Nipeni uzoefu niende maeneo gani tena niweze kuuona Mlima Kilimanjaro.
Nenda Kibosho maeneo ya Umbwe utauona vizuri hadi ufurahie
 
Nimekaa Moshi siku tatu lakini sikufanikiwa kuuona mlima, siku ya mwisho nikaambiwa natakiwa kuwahi kuamka saa 12 asubuh ndio naweza kuuona
 
Mkuu.. mlima Kilimanjaro unaonekana Asubuhi mda wa saa 11 mpaka saa moja. Baada ya hapo unafunikwa na mawingu. Unaweza pia kubahatisha kuuona mchana lakini ni mara chache na tena ni mda wa kiangazi tu. Ukifanikiwa kuuona unapendeza sana

View attachment 1613944

Hapa ni maeneo ya marangu.. Mda ilikua ni saa moja asubuhi
Kutoka malangu mpka moshi mjin ni sh ngapi hata mm napanga siku moja nitembelee huko nikaone mlima
 
Kabla ya kurudi Arusha Kunywa mbege kwanza mlima utauona
 
Mlima uko picha karibu zote, just google Mt. Kilimanjaro
 
Ukisimama pale KNCU unauona, Ukiwa Mweka pale Chuoni unauona, ukiwa TPC kule unauona, Ukiwa Mile Sita pale Weruweru unauona.
 
Njoo kesho shuka Tengeru saa 10 jioni yani unauona live kama vile upo hapo mbele tu
 
Hata ukiwa KIA mbona huwa unaonekana vizuri tu.
 
Back
Top Bottom