Mimi nimeingia kwenye site yao na nimeona kuwa kwa sasa wapo na safari moja ambapo ndege inaondoka dar 17:00 na kuwasili Mwanza 18:45, kuanzia mwezi December watakuwa na flight itayotoka Dar saa 06:00 na kuwasili Mwanza 07:45, kwa maoni yangu sio mbaya kwa kuanzia na huku ukipima upepo wa biashara, hata nauli yao ya 199,000 sio mbaya sana kwa kuazia ukichukulia kuwa tunaenda katika pick season. Ninachowashauri 1. wawe na maamuzi ya haraka wanapoamua jambo (waziri husika awape nafasi board wafanye kazi) bila ya maamuzi ya haraka kwenye airline business siku zote utaachwa nyuma. 2. waboreshe sana website. i.e najua archive yao ipo very rich kwenye information ya mambo ya ndege na culture za miji tofauti lakini wajue biashara kwanza na waache kuweka kila kitu pale front page. 3. kuna root zingine ni hot cake kwa mfano mwanza/Bukoba, ama Znz/Pemba maeneo haya kijiografia yametengwa na mikondo ya maji na hivyo kuwa vigumu kufikika kwa meli waende huko haraka. 4. Waingie kwenye biashara ya kuruhusu kununua tiketi kwa njia ya mitandao ya simu haraka sana.