CHAULA RICH
Umeuliza swali zuri. Tatizo ni kwamba vijana wa siku hizi wanadhani kila kitu kinachofanywa na vijana wenzao nje ya nchi - majuu - kinafaa kuigwa. Huo ni ulimbukeni.
Asili ya uvaaji "mlegezo" ni kwenye jela za nchi za nje, ambapo uvaaji huu ulianzia nchini Uingereza.
Kwa vijana wanaoingia magerezani, walijifunza kwamba ukiwa pale - mfungwa - unapaswa kuwa na "bwana" wa kukulinda ili usiwe unapigwa na kuumizwa na wafungwa wenzako. Kwa hiyo ili upate "ulinzi" huo unapaswa kukubali kujihusisha na matendo ya usodoma. "Bwana" wako anakuwa ni mtu mzima, jabali, mwenye wafuasi wengi, ambao baada ya wewe kuwa "kundini" hakuna atakayekugusa mpaka akuchoke au ugombane naye na aamue kwamba huna faida naye tena.
"Ukishatemwa" kwenye kundi la "Bwana" hiyo inakubidi uvae "mlegezo" ili "bwana" mwingine ajue kwamba sasa "uko huru" na yeye anaweza "kukuchukua".
Mtindo huu ulienea kwa kasi sana kwenye magereza ya Uingereza hadi Marekani, na unaonekana kuwa jambo la kawaida.
Hivyo basi, uvaaji huu unahusika kabisa na vitendo vya kishoga, na mashoga wengi wa kiume ambao hawako jela huvaa suruali zao kwa namna hiyo ili kujitambulisha kwa mashoga wengine, haswa kwa vijana.
Swali ni, je, hawa WAJINGA wanaovaa mlegezo wanajua maana yake?
Jaribuni kuwaambia kwamba uvaaji huo ni wa kishoga, muone kitakachotokea.
Nimemaliza.