Kwanini watu wanapenda kuvaa milegezo?

Kwanini watu wanapenda kuvaa milegezo?

Miongoni ya fasheni za hovyo kabisa kuvaliwa na vijana wa kizazi hiki, basi ni hii staili ya vijana wa sasa wanayoiita mlegezo aka kata K.

Huwa najaribu kuimagine hivi inawezekanaje kijana wa kiume avae huo mlegezo, halafu anapita mbele ya mama yake mzazi au mama mkwe wake bila wasiwasi wowote!

Huo ni mmomonyoko wa maadili uliopitiliza.

Vijana wetu waTz watambue kuwa siyo kila kitu kinachofanyika Marekani ni cha kuiga.

Nadhani umefika wakati, kama ambavyo imewahi kufanyika wakati fulani kwa wananchi kuwazomea waxiwazi wadada waliokuwa wanakatiza mitaani na vimini vya kutisha, hadi sasa wadada wengi wameacha kabisa kuvaa vimini vifupi sana, nadhani imefika wakati kwa watanzania wote tunaopenda Taifa letu liwe na maadili mema, tuanze sasa kuwazomea waziwazi vijana wote kila watakapokuwa wanapita, wakiwa wamevaa hayo mavazi yso ya kishenzi ya mlegezo.

Naamini ni kwa njia hiyo peke yake, tutaweza kulirejesha Taifa letu kwenye mstari, badala ya kuliacha liendelee kuangamia na mmonyoko huo wa maadili uliopitiliza.
We nawe maadili maadili, hayo maadili yanakuongezea msosi mezani?? kila mtu aachwe aishi maisha yake aliyoyachagua as long as havunji sheria wala kumbugudhi mwenzake.
 
We nawe maadili maadili, hayo maadili yanakuongezea msosi mezani?? kila mtu aachwe aishi maisha yake aliyoyachagua as long as havunji sheria wala kumbugudhi mwenzake.
Acha kutetea vitu visivyofaa, inawezekana nawe ukawa miongoni ya hao wavaaji wa hiyo milegezo.

Hivi hao vijana kutuonyesha maboxer yao, wengine hawajayafua hadi wiki moja, kwako unaona imekaa sawa tu?!
 
Ingekua vyema kwa watanzania kuanzisha OPERESHENI KOMESHA UVAAJI WA MILEGEZO.

Kama ambavyo watanzania siku za nyuma walivyoweza kuanzisha Operesheni Komesha Uvaaji wa Vimini, na hatimaye uvaaji huo wa vimini kwa mabinti zetu umepungua kwa kiasi kikubwa sana.

Ipo haja kwa sasa kila kijana mvaa mlegezo anapopita mtaani, azomewe kwa nguvu na kuitwa BWABWA HILO LINAPITA,

Naamini hiyo yaweza kuwa dawa ya kutokemeza hiyo fasheni ya milegezo, ambayo mimi naweza kuiita kuwa ni fasheni mbovu kuvaliwa na vijana, katika historia ya tangu Tanganyika yetu ipate uhuru wake toka kwa mkoloni mwaka 1961.
 
Ingekua vyema kwa watanzania kuanzisha OPERESHENI KOMESHA UVAAJI WA MILEGEZO.

Kama ambavyo watanzania siku za nyuma walivyoweza kuanzisha Operesheni Komesha Uvaaji wa Vimini, na hatimaye uvaaji huo wa vimini kwa mabinti zetu umepungua kwa kiasi kikubwa sana.

Ipo haja kwa sasa kila kijana mvaa mlegezo anapopita mtaani, azomewe kwa nguvu na kuitwa BWABWA HILO LINAPITA,

Naamini hiyo yaweza kuwa dawa ya kutokemeza hiyo fasheni ya milegezo, ambayo mimi naweza kuiita kuwa ni fasheni mbovu kuvaliwa na vijana, katika historia ya tangu Tanganyika yetu ipate uhuru wake toka kwa mkoloni mwaka 1961.
. Kipindi cha Awamu ya kwanza kulikuwa na maadili hadi kwenye Uvaaji nguo, Lakini awamu ya Nne ya JK wapo busy na yao hawataki kuangalia maadili yanavyoharibika ndiyo maana Vijana wengi wametumia Udhaifu huo kujivalia hovyo hovyo na hakuna Kiongozi ataweza kuthubutu kuhoji hilo.
 
Acha kutetea vitu visivyofaa, inawezekana nawe ukawa miongoni ya hao wavaaji wa hiyo milegezo.

Hivi hao vijana kutuonyesha maboxer yao, wengine hawajayafua hadi wiki moja, kwako unaona imekaa sawa tu?!

Huyo Matumbo ni Muumini number one wa Uvaaji wa Hovyoo a.k.a kata K ( Mlegezo) anataka kulazimisha watu wa-copy mitabia yao ya kijinga jinga pasipo kujua kuwa kizazi kinazidi kuharibika kwa wavaa Milegezo wa leo huenda wakawa viongozi wa kesho, sasa unategemea nini Mvaa Mlegezo akiwa kiongozi?
 
Mmmh! Kumbe ngoja niache kupiga mlegezo maana maneno yenu yamenigusa kumbe kuna mijitu inakuona shoga!!!! ,, too bad
 
Hiyo ni Genesis kwa Ulaya na Marekani ya 2000 s to above ....hasa Baada ya uvutaji wa Madawa ya kulevya kuzidi pia ....Kama nilivoelezea hapo Juu ....caught downing means "he" is ready kuvuliwa suruali anytime

Ila kabla gangs waliokuwa wanatoka jela ilikua kielelezo cha kuonesha Jamii kuwa they are hardened ..and hardcores ..Ndio maana ukikumbuka wale hardcore rappers Kama Easy E, Dr Dre ,Snoop Dogg, doggy Pound , Big Small Na junia mafia ...2pac..etc wote walivaa milegezo na minyororo in reminence of Jail ....na lazima wakiimba wa dedicate all the niggers who still rotting in the jail cells ....Sioni Siku hizi wakivaa tena ...

America kuna Baadhi ya majimbo wamepiga marufuku kabsa Uvaaji Suruali chini ya kiuno, hata America airline wana mabango kwenye ndege zao yanayowataka wateja wao kutovaa Mlegezo kwenye ndege zao, pata Picha kuwa Mlegezo ulianzia marekani lakini sasa hao hao wamarekani hawaitaki tena Lakin sisi Watanzania bado tunang'ang'ania huo Ujinga na Viongozi wapo busy kuwaza Uchunguzi nk hawataki kukemea hizo Tabia mbovu.
 
Aisee mi nimevaa sana 'milege' kipindi niko sekondari, but sikuwah kufikiria swala la ushoga, sahivi umri umesogea nimejikuta tu nimeacha
 
America kuna Baadhi ya majimbo wamepiga marufuku kabsa Uvaaji Suruali chini ya kiuno, hata America airline wana mabango kwenye ndege zao yanayowataka wateja wao kutovaa Mlegezo kwenye ndege zao, pata Picha kuwa Mlegezo ulianzia marekani lakini sasa hao hao wamarekani hawaitaki tena Lakin sisi Watanzania bado tunang'ang'ania huo Ujinga na Viongozi wapo busy kuwaza Uchunguzi nk hawataki kukemea hizo Tabia mbovu.

Labda kama huwaangaliagi wakina Lil Wayne
 
Dash unazidi kupambanua how big ushuzi are you

Hawazi pambana na hewa ambayo hutoka mda wowote na popote hachagui hapa kuna nani hata akiwepo Obama Rais wa Duniani ikiamua kutoka inatoka tu, tupige vita Mlegezo, Ruge wa Clouds upo Wapi? Fursa Hiyo tafuta wadhamani watoe pesa Kampeni piga vita Mlegezo ianze kama ilivyo hii kampeni ya kupiga vita Michepuko.
 
Vijana wengi wapenda Milegezo ukiwachunguza tabia zao kwa kweli idadi kubwa hawapendi kufanya kazi, wanapenda kulelewa, wizi, kuuza Unga, Bangi na mda mwingi ni kushinda bar vijiweni na Disco, Kijana Mchapa kazi mwenye mawazo ya kimaendeleo hawezi kukaa akawaza na kukariri kuwa kuvaa kata K ni Ujanja na Ufahari ! Kwa bahati mbaya Tanzania huwa ni Nchi ambayo ni jalala la Tabia Mbovu mbovu kwa sasa Serikali wapo busy kuwathibiti wapinzani juu ya maandamano hawana time na watanzania kuvaa nguo za Ajabu Ajabu, hata ukivaa nguo ya Usiku hakuna wa kukuhoji, Uganda wao wapo makini waligundua mapema Athali za kuachia kila Tabia Mbovu kupenya kwenye jamii Rais Mseveni kapiga marufuku Uvaaji wote wa kijinga jinga.
 
Wavaa Milegezo Tanzania ni Watemi na wababe pia ndiyo wapiga kura wakuu, ndiyo Maana Waziri wa Utamaduni, waziri wa Utawala bora, IGP na Waziri wa mambo ya Ndani wanawaogopa sana, hatathubutu kukemea hilo na haitakaa itokee labda Chadema wakivaa Mlegezo hapo utawasikia wanatoa Amri na Sheria za kudhibiti maadili zitazingatiwa, Hata Viongozi wa Upinzani akina Lipumba, mbowe, slaa, mbatia nk , hawana Sauti mbele ya Wavaa Milegezo na vimini na vinguo vya hovyo. Chezea Mseveni.... Kule Uganda hukuti watu wanavaa Milegezo kama Tz.

Mpwa uko sawa?
 
Aisee mi nimevaa sana 'milege' kipindi niko sekondari, but sikuwah kufikiria swala la ushoga, sahivi umri umesogea nimejikuta tu nimeacha

Milege ni Sumu ya miguu Kwani ukivaa Mlegezo hata Mwendo, utembeaji hubadilika wengine hutembea kama Vilema, wengine huburuza miguu na kwenda upande Upande, hata likitokea tukio la kukimbia wavaa Mlegezo hukamatwa haraka kwani si rahisi uvae Mlegezo kisha iwe Rahisi kutoka nduki faster, tupige vita Mlege kama tunavyopiga vita Tabia zingine mbovu Mbovu.
 
Mpwa uko sawa?

Kuna msemo kuwa hakuna aliye juu ya sheria, Lakini huo msemo haupo kwa Wavaaji Mlegezo, wao wanajua kuwa wapo juu ya Sheria ndiyo maana IGP awawaogopa sana hata mwanasheria mkuu pia hathubutu kuwagusa na kwa sasa hakuna Kiongozi anaweza kulisemea hili si wa Upinzani wala CCM hata Kinana mwenyewe anagwaya Sembuse nape.
 
Nadhani kusema kwanini watu wanapenda kuvaa milegezo unakosea. Unge sema kwanini wahuni hupenda kuvaa milegezo.
 
Back
Top Bottom