Usedcountrynewpipo
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,636
- 2,731
Skewed minds (fikra potofu)...
Mashoga hawavai mlegezo ata siku moja, wengine wanachomekea kabisa.
Mlegezo ni swagger tu za street, hii style ilianzia huko Marekani kwenye jela moja kuna mchiz nguo alizopewa baadae zilimpwaya akageuza style.
Wengine hadi mataulo wana shusha mlegezo...
Biashara matangazo Yaani imo
Hahahahahaha! Wengine nasikia hadi kanzu wanalegeza.
Acha kutetea vitu visivyofaa, inawezekana nawe ukawa miongoni ya hao wavaaji wa hiyo milegezo.
Hivi hao vijana kutuonyesha maboxer yao, wengine hawajayafua hadi wiki moja, kwako unaona imekaa sawa tu?!
Watanganyika tuamke sasa tusiishi kwa mazoea mambo ya kuishi kwa kukariri lifestyle ya mbele hayana nafasi kwa sasa, kilichobaki ni kuiga Tekinologia bora tu na maendeleo vingine si Lazima tuwaige yatupasa na sisi tubuni Mavazi mazuri ili na wao watuige sisi isiwe kila siku kuwaiga wao tu.
ili wakatike vizuri wakati wa kutembea,,
Huo ni utashi wa mtu isiwe ishu ya kulazimisha. Wewe iga technology mwenzio aige mlegezo maisha yanaendelea.
Shusha kidogo hiyo sarawili yako, tena, tena, bado kodogo, eeeeh hapo hapo, sasa anza kutembea mimi nipo nyuma yako teh teh, Miss Chagga angalia mwendo wa kijana
Watu wakiamua kuushi kivyao vyao pasipo kukanyana wala kukosoana ina maana Hayo ni maisha ya Hatari sana, Wavuta Bangi,vibaka wala unga na Wavaa Milegezo watafurika kama nzige, lazima tuishi kwa maadili kama wewe ulivyoamua kuacha Mlegezo baada ya kujua kuwa ni Aibu kuiacha Tigo wazi,wasihi waacha using'ang'anie Tamaduni zisizo na tija.Milegezo nimevaa sana sikatai, ila sasa umri hauniruhusu sivai tena wala hakuwai tokea mtu kunikataza .
Nachoshangaa wewe kuona kitu usichopenda basi liwe jambo la kitaifa, yani mlegezo kaweka mwingine we unakosa raha kwa nini. Angaika na mambo yako.