Diva Beyonce
JF-Expert Member
- Mar 6, 2014
- 12,913
- 11,295
Sio kumwachia mungu nchi hii wasio jielewa ni wengi hata mafuriko badala ya kuya control wanamwachia Mungu hata kipindu pindu wanamwachia Mungu. Ignorance ni janga kwa hili taifa
Jamani naomba mnisaidie, hivi hii ni hulka au tatizo au kukata tamaa? Imekuwa tabia ya watanzania wengi kupenda kumuachia Mwenyezi Mungu hata katika mambo ambayo yalikuwa ndani ya uwezo wao, nao ndo walitakiwa kuchukulia hatua;
Mfano:
1. Mtu anatapeliwa pesa, utasikia anasema namuachia Mungu, atanilipia (badala ya kukomaa na aliyemtapeli amrudishie, au nayeye amtapeli kitu kingine).
2. Mtu anaibiwa kitu, utasikia namuachia Mungu, ndiye atakayenilipia, (hachukui hatua yeyote)
3. Mtu anakuvunjia heshima, (hapa napo anamuachia Mungu, yaani hata kumlamba vibao viwili vitatu unashindwa hayo ni machache sana, ila kuna mengi ya namna hiyo, nadhani hata wewe ni mmoja ya wanaomuachia mwenyezi Mungu,
Tuache kumuachia Mungu mambo ambayo tunaweza kuyashughulikia wenyewe!! Tumuachie vile ambavyo vipo nje ya uwezo wetu, mfano mafuriko, kimbunga, ukame na mengine.
"Namuachia mungu" ni kauli ya watu wenye umasikini na ufukara wa mawazo.
uwe unatumia na choya:A S shade:mie nakunywa vya asili, udo.
uwe unatumia na choya
Hata Hi Post Tuna Mwachia Mungu T Maana Yey Ndie Ajuay