Kwanini Watanzania wamuachie Mungu?

Kwanini Watanzania wamuachie Mungu?

upupu

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2008
Posts
614
Reaction score
198
Jamani naomba mnisaidie, hivi hii ni hulka au tatizo au kukata tamaa? Imekuwa tabia ya watanzania wengi kupenda kumuachia Mwenyezi Mungu hata katika mambo ambayo yalikuwa ndani ya uwezo wao, nao ndo walitakiwa kuchukulia hatua;

Mfano:
1. Mtu anatapeliwa pesa, utasikia anasema namuachia Mungu, atanilipia (badala ya kukomaa na aliyemtapeli amrudishie, au nayeye amtapeli kitu kingine).

2. Mtu anaibiwa kitu, utasikia namuachia Mungu, ndiye atakayenilipia, (hachukui hatua yeyote)

3. Mtu anakuvunjia heshima, (hapa napo anamuachia Mungu, yaani hata kumlamba vibao viwili vitatu unashindwa hayo ni machache sana, ila kuna mengi ya namna hiyo, nadhani hata wewe ni mmoja ya wanaomuachia mwenyezi Mungu,

Tuache kumuachia Mungu mambo ambayo tunaweza kuyashughulikia wenyewe!! Tumuachie vile ambavyo vipo nje ya uwezo wetu, mfano mafuriko, kimbunga, ukame na mengine.
 
Watanzania huwa wanajidai ni washika neno(namwachia MUNGU), lakini ni wanafiki wakubwa(matendo yao hayafanani na Yule wanayesema wamemwachia) na wakitoka hapo ni break hadi Bagamoyo kwa Sangoma.

Anyway, 'mungu' ni relative naona!
 
Watanzania huwa wanajidai ni washika neno(namwachia MUNGU), lakini ni wanafiki wakubwa(matendo yao hayafanani na Yule wanayesema wamemwachia) na wakitoka hapo ni break hadi Bagamoyo kwa Sangoma.

Anyway, 'mungu' ni relative naona!

Ukiwemo na wewe pia .
 
Wala hatutaki shida ni mipango ya Mungu na tunamwachia mungu.
 
mungu wao hana kazi ndiyo maana wanambebesha hata ambavyo mtoto mdogo anaweza beba.
 
Mimi nilisubiri kwa hamu tuingie barabarani watu kimyaaaa,madai yao wamemuachia Mungu!
Inakera sana.
 
Tulianza na Mungu tutamaliza na Mungu. Kumbuka kuna imani inasema kuwa "Heri na shari vyote vinatoka kwa Mungu"
 
"Namuachia mungu" ni kauli ya watu wenye umasikini na ufukara wa mawazo.
 
Acha niendele kupata windhoek baridddd hehehe
 
Mimi nilisubiri kwa hamu tuingie barabarani watu kimyaaaa,madai yao wamemuachia Mungu!
Inakera sana.
Vp nifah! Pole na maumivu najua tulikuwa ktk boti moja! Lkn kwa upande wangu wilaya yangu ya kino Diwani katoka ukawa cdm, mbunge ndy vile....kuna wakati wananchi mnaweza anzisha figisufigisu na ikazaa matunda,etc biafra, kuhusu kuandamana hilo liko kwa viongozi wakuu walianzishe watu watamalizia
 
Kwa sababu moja tu: Ujinga.

Sasa hapa wale 'wajinga' wasiojua maana ya 'ujinga' wanaweza wakakasirika na kudhani labda nimewatukana kwa kuwaita 'wajinga'.

Adui 'ujinga' bado hatujamshinda kabisa.
 
Back
Top Bottom