Hii imenifikirisha sana!
Kwa kawaida mimi huwa si mtu wa kupiga mizinga, kwasababu nina kipato cha kujitosheleza na kubaki akiba kubwa tu.
But last week nikaona nijaribu kuomba watu kadhaa hela kama kuwajaribu tu. Huwezi kuamini, yaani bila hata wao kuwaza mara mbili mbili, wale watu wote 5 walituma hela kwenye simu yangu. Na kilikuwa ni kiasi kikubwa tu cha pesa kwa usawa huu wa Magu.
Swali ninalojiuliza: Inakuwaje katika nyakati hizi za ulimwengu wa mitandao ya kijamii, mtu anakuamini kirahisi rahisi tu na kukutumia pesa zaidi ya laki 1 bila hata ya kuwa anakufahamu? Je JF tuna ukarimu mkubwa kiasi hicho compared to other platforms?