Kwanini walimu hawazeeki mapema?

Kwanini walimu hawazeeki mapema?

Kweli aisee mkuu nakuunga mkono 💯% natoka familia ya walimu bibi yangu kastaafu 2012 ukimwona bado yupo fiti mbaka Kuna wanafunzi wake wa miaka ya 80 huko wanadhani Bado anafundisha mbaka now akiwaambia ana miaka 9 Toka astaafu wanabisha kabisa Yani!
 
Habari wanajukwaa,
Kuna ka usemi nilikua nakasikia tangu nikiwa shule O-level ila nilikua siamini eti walimu hawazeeki haraka. Kwa kweli nimekuja kushuhudia na kuchunguza juu ya hilo na kuona ni kweli kwa 100% maana juzi kama bahati nimekuta na mwalimu wangu ambaye alinifundisha vidudu(chekechea) sikuweza kuamini kwani haikunipa tabu kumtambua nilivyomuona mara moja niliweza kumfahamu.

Kiukweli yupo vilevile na bado anafundsha na ameweza kufungua center yake mwenyewe sio huyo tu na wengine wengi kuanzia primary mpaka secondary sijajua kiiman kwamba mwenyezi Mungu amewabarki ama vipi au niikwanini inakuwa hivyo.

NAWASILISHA
pia waalimu kipato chao ni kidogo lakini wanajitahidi kuwasomesha watoto shule nzuri za gharama.
 
Ukweli ni kwamba tunajua kuridhika, hakuna mashindano ya kijinga ofisini...Huyo Mkuu wa shule ana Boda Boda, mratibu Elimu ana baskeli...me nikakimbilie mkopo wa gari kisa cha kujitia stress nini? Akuu
Halafu hatuna stress za ntakula nini, tunakopesheka yani...nimeshuhudia huku nabebembelezwa kukopa nyama kiroho safi...tunaaminika sa we jaribu kukopa uone unavyopigwa cha mbavu.

Halafu hamna stress za kukutana na boss kila siku ofisini yani...unafanya kazi unavyopenda wakaguzi wanakuja Mara moja kwa mwakaaa...

Pia ni lifetime job, yani uumwe, uvunjike, upooze mshahara uko pale pale na kibarua hakipo mashakanii...

Kubwaa kuliko watoto wenu wanatupa raha, yani tukisahisha mitihani tunacheeeka hadi makunyanzi yanaondokaaa...wanajua kuandika pumba Wallahi.....

nimemaliza...
Aisee,we umeongea.,tunawakamata na vibarua vya mapenzi,tunawahoji wameyaona wapi haya,majibu yao sasa
 
Kubwaa kuliko watoto wenu wanatupa raha, yani tukisahisha mitihani tunacheeeka hadi makunyanzi yanaondokaaa...wanajua kuandika pumba Wallahi.....
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🙌
 
true juzi kati nimekutana na mwalimu wangu wa primary huwez amin tukapeana mambo tukagonga nikamkumbusha shule akajibu aaah nimehama niko shule nyingine akaniuliza ulikua unafanya kazi wap maeneo yale hakumbuki kua alinifundisha nikiwa darasa la 3 yy anadhan nilikua mkubwa nafanya kazi maeneo hayo nilishangaa sana!!! though kwa muonekano nikisimama nae unaona kabisa kama ni watu wa rika moja ndo mana salam ya mambo ilikua justifiable kabisa in the end wala sikumkumbusha kua alinifundisha!!!!
"Mkapeana mambo mkagonga" Samahani mkuu hii imekuwa sentensi tata kwangu

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
kuna moja yupo mtaani kwetu hapa anastaafu mwakani lakini ukimlinganisha na mimi ambao ndo na miaka 9 kazini.naonekana zee la mi mvi kichwani
 
Habari wanajukwaa,
Kuna ka usemi nilikua nakasikia tangu nikiwa shule O-level ila nilikua siamini eti walimu hawazeeki haraka. Kwa kweli nimekuja kushuhudia na kuchunguza juu ya hilo na kuona ni kweli kwa 100% maana juzi kama bahati nimekuta na mwalimu wangu ambaye alinifundisha vidudu(chekechea) sikuweza kuamini kwani haikunipa tabu kumtambua nilivyomuona mara moja niliweza kumfahamu.

Kiukweli yupo vilevile na bado anafundsha na ameweza kufungua center yake mwenyewe sio huyo tu na wengine wengi kuanzia primary mpaka secondary sijajua kiiman kwamba mwenyezi Mungu amewabarki ama vipi au niikwanini inakuwa hivyo.

NAWASILISHA
Hahahaha
 
Kwa Mtazamo wangu Wanamuziki ndiyo hawazeeki mapema kutokana na kuwa na furaha sana katika kazi yao ya muziki/burudani. Hawana stress

Juzi tu nimemwona mwanamuziki mkongwe mzee Zoro ametupia pensi kama sharo wa umri wa miaka 30 hivi.
Huyo anajifanyisha tu lakini kongoro kwisha anapenda ujana by kulazimisha mambo, lakini walimu hata avae vip utamuona bado ana umri umri wa kutokuzeeka
 
Kuna mwalimu alinifundisha kusoma na bado akaja kumfundisha mwanangu 1990's kusoma pia.

Shule ya msingi mtakuja,
 
Kwa fikra zangu nafikiri ni kwasababu ya pyschology.. kwasababu Walimu muda mwingi wanautumia wakiwa na Vijana na watoto.. basi hii inapelekea Pyschology na akili zao kujivika utoto ingali ni watu wazima.. Hivyo cells za mwili zinafanya adaptation kulingana na ubongo wao kukaa kwenye Mazingira ya watoto na vijana na watoto muda mrefu.. that's why hawazeeki.. Ila. Kwa mtu Mwingine utazeeka mapema kwasababu akili yako inakaa zaidi na watu wazima ofsini na vijana wasio kwenye Mazingira ya kishule hizo inazeeka mapema
 
Habari wanajukwaa,
Kuna ka usemi nilikua nakasikia tangu nikiwa shule O-level ila nilikua siamini eti walimu hawazeeki haraka. Kwa kweli nimekuja kushuhudia na kuchunguza juu ya hilo na kuona ni kweli kwa 100% maana juzi kama bahati nimekuta na mwalimu wangu ambaye alinifundisha vidudu(chekechea) sikuweza kuamini kwani haikunipa tabu kumtambua nilivyomuona mara moja niliweza kumfahamu.

Kiukweli yupo vilevile na bado anafundsha na ameweza kufungua center yake mwenyewe sio huyo tu na wengine wengi kuanzia primary mpaka secondary sijajua kiiman kwamba mwenyezi Mungu amewabarki ama vipi au niikwanini inakuwa hivyo.

NAWASILISHA
Watu wanao ongea sana hawazeeki harska
 
Kazi yao yenyewe ni mazoezi tosha, yaani kwa siku Mwalimu ana vipindi tuseme vinne na Kila kipindi anatumia dakika 45 maana yake kwa siku anasimama wima na kufanya movement za hapa na pale kwa muda wa masaa matatu

Hivyo basi afya yake lazima iwe vizuri na kuendelee kuwa kijana kila siku..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom