Kwanini walimu hawazeeki mapema?

Kwanini walimu hawazeeki mapema?

Mh kumbe now wanaohitaji kuchelewa kuzeeka ni mwendo wa kuwashauri kuwa walimu! but nadhani uwalimu ni mazoezi tosha, (naunga mkono hoja)
 
Tutazeekaje wakati kila siku tunatembea ya mguu kwenda kazini???
Ni lazima niamke saa kumi na moja na nusu kwenda kuwasimamia watoto usafi shuleni na kuwakimbiza mchaka mchaka.

Na kila siku ni lazima niwaangalie wanavyosoma wakiwa Prep. Nakula chakula cha dona na mboga za majani za shule.

Huku hata kumbi za starehe sizijui sasa nitazeekeaje? Mimi nakutana sana na watu niliowahi kusoma nao Miaka mingi nyuma wananiambia sizeeki.
Kweli ni mazoezi ya kila siku tu.

Sent from my BlackBerry 9720 using JamiiForums
 
Sio kwamba hawazeeki, Ila mategemeo yetu kuona wakizeeka mapema kutokana na kazi yao ndo kunafanya tuwaone hawazeeki. Ila ukifika umri wa kuzeeka wanazeeka tu mbona
 
Habari wanajukwaa,
Kuna ka usemi nilikua nakasikia tangu nikiwa shule O-level ila nilikua siamini eti walimu hawazeeki haraka. Kwa kweli nimekuja kushuhudia na kuchunguza juu ya hilo na kuona ni kweli kwa 100% maana juzi kama bahati nimekuta na mwalimu wangu ambaye alinifundisha vidudu(chekechea) sikuweza kuamini kwani haikunipa tabu kumtambua nilivyomuona mara moja niliweza kumfahamu.

Kiukweli yupo vilevile na bado anafundsha na ameweza kufungua center yake mwenyewe sio huyo tu na wengine wengi kuanzia primary mpaka secondary sijajua kiiman kwamba mwenyezi Mungu amewabarki ama vipi au niikwanini inakuwa hivyo.

NAWASILISHA
MIKOPO NA MAISHA MAGUMU
 
Mfumo wa maisha pia unachangia hawana hela za anasa na wanatumia muda mwingi kwenye kuandaa madesa na tuitions etc.

Anyway walimu wangu walevi wa gongo nishawazika sana tu pamoja na wale vicheche.
Wanapoenda chuma mboga nimemkumbuka mwl. Wile
 
Nikweli kabisa walimu hawazeeki mapema,,nimeanza shule nina mwaka 1994 nikamkuta mwalimu tumbo ni mkuu shule ya msingi nyanza na hadi leo ni mwalimu mkuu pale nyanza na bado anadundika tu.
Hahahahha wanaishi maisha halisi sana bila ma anasa ya ma bia
 
Kumbe starehe zinazeesha mapema kuliko maisha magumu? Mbona kama hii kitu ina-contradict aisee?
Ina contradict vipi mzee unless uwe upo kwenye maisha ya kula majalalani😅!!!
Walimu wanakula maisha ya mboga na madagaa chukuchuku tofauti na manyama na mavyakula ya mafuta mafuta (healthy foods). Wanalima lima bustani zao (Mazoezi) wanaenda shule kwa mguu ama baiskeli (mazoezi). Wanasimama most of the school hours wakifundisha (mazoezi). Wanakokotoa mahesabu na kusahihisha madaftari na mitihani (mazoezi). Hayo ni machache tu kwa hao walimu!

Tukiangalia kwa wenye unafuu wa maisha hapa nawagusa maboss boss! Asubuhi chai nzito kisha kazini ni kwa gari, 8 hours yupo kakalia kiti ni kupiga simu na kuchezea laptop! Muda pekee anatembea ni kwenda toilet na kutoka ofisini kwenda lunch! Hapo utaona ni kushindilia supu mchana ma vyakula yenye mafuta au manyama choma na ugali! Kisha jioni ndani ya gari tena mpaka bar ya jirani na home kugida mabia kisha home kula mawali ya mke na kualala.

Hii aina ya lifestyle inakuhakikishia kisukari na BP ya mapema sana
 
Ina contradict vipi mzee unless uwe upo kwenye maisha ya kula majalalani!!!
Walimu wanakula maisha ya mboga na madagaa chukuchuku tofauti na manyama na mavyakula ya mafuta mafuta (healthy foods). Wanalima lima bustani zao (Mazoezi) wanaenda shule kwa mguu ama baiskeli (mazoezi). Wanasimama most of the school hours wakifundisha (mazoezi). Wanakokotoa mahesabu na kusahihisha madaftari na mitihani (mazoezi). Hayo ni machache tu kwa hao walimu!

Tukiangalia kwa wenye unafuu wa maisha hapa nawagusa maboss boss! Asubuhi chai nzito kisha kazini ni kwa gari, 8 hours yupo kakalia kiti ni kupiga simu na kuchezea laptop! Muda pekee anatembea ni kwenda toilet na kutoka ofisini kwenda lunch! Hapo utaona ni kushindilia supu mchana ma vyakula yenye mafuta au manyama choma na ugali! Kisha jioni ndani ya gari tena mpaka bar ya jirani na home kugida mabia kisha home kula mawali ya mke na kualala.

Hii aina ya lifestyle inakuhakikishia kisukari na BP ya mapema sana
Mtuache na dagaa wetu chuku chuku.
Ila umetunanga na kutusifia humo humo kenge wewe
 
Mie huwa ninafanya balance of trade wabejah sana maticha wote
Hapo ulisahau vituko vya wanafunzi, ukiacha maujinga yao ila most of the times wanafurahisha sana. Yaani kikitoka kituko kimoja kinakuja kingine basi ni muda mwingi ni kufurahi tu.

Lakini pia sisi hatujifungii kila mtu ofisini kwake na stress zake, tunakaa ofisi moja karibia walimu wote, basi hapo ni story za hapa na pale za kuelekezana jinsi ya kuunga dagaa wetu huku unasahihisha madaftari. Na kushirikishana vituko vya watoto basi ni kucheka tuu muda wote.

Lakini pia walimu wengi tunaishi maisha yetu halisi, hakuna kufake sijui ninunue wigi la milioni sijui. Nikisuka nywele za elfu 5 nimejiridhikiaa na kitenge changu mpauko
 
Habari wanajukwaa,
Kuna ka usemi nilikua nakasikia tangu nikiwa shule O-level ila nilikua siamini eti walimu hawazeeki haraka. Kwa kweli nimekuja kushuhudia na kuchunguza juu ya hilo na kuona ni kweli kwa 100% maana juzi kama bahati nimekuta na mwalimu wangu ambaye alinifundisha vidudu(chekechea) sikuweza kuamini kwani haikunipa tabu kumtambua nilivyomuona mara moja niliweza kumfahamu.

Kiukweli yupo vilevile na bado anafundsha na ameweza kufungua center yake mwenyewe sio huyo tu na wengine wengi kuanzia primary mpaka secondary sijajua kiiman kwamba mwenyezi Mungu amewabarki ama vipi au niikwanini inakuwa hivyo.

NAWASILISHA
Huwezi kukutana na walimu wachache kati ya walimu wote waliokufundisha ukaishia kufanya conclusion kuwa walimu wote hawazeeki?
Kwani walimu wana kitu gani special zaidi ya binadamu wengine kinachofanya wasizeeke?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom