Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
Umechangi vizuri sana especial mwisho!
Kuhusu kutokupanga uzazi na maswala ya kuoa wake zaidi ya mmoja.... mfano mimi wale tuliomaliza nao Dodoma Sec miaka zaidi ya 12 iliyopita marafiki zangu "wakristo" wengi wao hawajaoa/olewa na walio oa/olewa hawana mtoto zaidi ya mmoja! Lakini rafiki zangu wa kiislam wake kwa waume nikiwamo mimi tuna watoto zaidi ya mmoja! Madhalan mimi nina wake wawili in ten years siwezi kuwa sawa na Rafiki yangu ambae hana mke wala mtoto maana mimi dini yangu hainiruhusu kufunga uzazi kwa njia yoyote ile! that means nitakuwa na watoto wa kutosha tu!
Take from me then zidisha kwa hao waislam wachache uwajuao wewe.
Mkuu kwanza hongera kwa kuwa na wake wawili. Lakini kwanini unaona wawili? kwa sababu dini inakuruhusu? uchumi unakuruhusu? na hao wake waili unaweza kuwatunza vipi? au ndio wanaishi maisha magumu kila kukicha? Do you real think this is smart? Unadhani kwanini wenzako uliomaliza nao sekondari hawajaoa, wana matatizo ya kibaiolojia au?
Ukiangalia kwa undani suala hili unaweza kukuta kuwa ndio linachangia kwa baadhi ya watu kukosa elimu. kuna watu wana wake wanne na watoto 12 lakini hana uwezo wa kumpa chakula bora mtoto mmoja kwa mwaka mzima, au kumsomesha mtoto hata mmoja hadi chuo kikuu cha maana, matokeo yake wanasema eti mtoto anakuja na riziki yake. Kuna wengine mtoto akifika darasa la saba anasema sasa umekua jitafutie maisha. Vicious circle.