TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,514
- 11,277
Wewe ukiambiwa uuze Makoti msimu wa Joto hapa Dar utakubali?Shalom wapendwa, nataka kujua kuhusu hawa Wachungaji wa michongo inakuwaje wajikite kuhubiri mafanikio ya pesa na mali na sio mafanikio ya kiroho.
Leo hii vijana wengi wamekimbilia kuanzisha makanisa huku wakijiita mitume, manabii, maaskofu nk lakini nimejaribu kusikiliza mafundisho yao yapo kinyume na ukweli wa kibiblia yaani hawajui kuichambua Biblia kama neno la Mungu lisilo na ubaguzi ktk kumhudumia muhitaji.
kuna baadhi ya makanisa haya ya Wachungaji wa michongo ni wabaguzi wakubwa wanaotenga hadi viti maalum kwa watu maalum (VIP)
Hapo tusemeje kuhusu Mungu maana Mungu sio wa kubagua bali huwahudumia wote wenye mali na wasio na mali.
Kwanini Wachungaji wa michongo huhubiri pesa zaidi kuliko mafanikio ya kiroho?
View attachment 2079225
Wanasoma upepo unavumaje na wao wanajikitia humo humo.