Kinoamiguu
JF-Expert Member
- Nov 29, 2018
- 10,526
- 13,015
Tabia hii inazidi kukua kila kukicha japo inaudhi. Hawa watu wanalipwa na nani na wanatoka wapi?
Lazima ifike mahali tukubaliane kwamba kila mtu ana imani yake kulingana na alivyolelewa na kwamba swala la imani ni binafsi na kuna maeneo mahususi ya kuabudu.
Makanisa ya kilokole kina Mwamposa na wenzake wanaoibuka kila siku kama uyoga. Hawa huwapata wale waliopoteza matumaini na dini zao za asili.
Hawa huamini kwamba wafuasi wao wanapatikana popote hata kwenye mabus na stand siijawahi kumuona padre wa RC wala askofu achilia mbali shemasi akihubiri barabarani. Nadiriki kusema na kuamini kwamba hawa wanaofanya mahubiri yao barabarani na kwenye mabasi ni walewale wenye asili ya kuhani musa na mzee wa upako.
Waislamu, hawa shughuli zao huishia misikitini na kwenye makusanyiko ya warming wao. Japo na wao wanatumia vipaza sauti ambazo mara nyingi huwa ni kero kwa wasiohusika lakini hutolewa kwenye maeneo maalum tu.
Wapagani na wasio na dini, hawa ni pamoja na wqnaoamini katika miungu ya kale (waliowengi hawajitanabahishi) lakini hukereka sana na wapo wengi.
Unakuta mtu mmepanda kwenye usafiri wa umma au mkiwa stand kila mtu akielekea kwenye mambo yake tena na mawazo tofauti mtu anawasha speaker yake ya mchina na kuanza kuhubiri dini? Aliyewambia mungu yupo kwenye daladala au standi ni nani?
Ni kweli kuna uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa sheria lakini kila uhuru unamipaka yake. Kwa kutambua hilo ndo maana serikali imetenga maeneo maalumu ya kufanyia ibada ambako warming hukutana huko na kumuomba huyo mungu.
Utaratibu wa kuhubiri kwenye mabasi ya umma na vituo vya mabasi ni utaratibu holela na unakiuka haki za watu wengine wasiopenda kusikia habari za Mungu kwa wakati huo.
Wale mnaowapa pesa watu hawa pia mngezielekeza pesa zenu kwa wahitaji moja kwa moja ili zimfikie huyo mungu na mupate baraka muwe na mafanikio zaidi hata kama wengi wenu ni wezi wa mali za umma, waongo, wazinzi, waasherati na wasengenyaji (baada ya kutoka kwenye nyumba za ibada).
Uhuru wako uishie mwisho wa pua yako, vinginevyo ni vurugu!
Nawasilisha.
Lazima ifike mahali tukubaliane kwamba kila mtu ana imani yake kulingana na alivyolelewa na kwamba swala la imani ni binafsi na kuna maeneo mahususi ya kuabudu.
Makanisa ya kilokole kina Mwamposa na wenzake wanaoibuka kila siku kama uyoga. Hawa huwapata wale waliopoteza matumaini na dini zao za asili.
Hawa huamini kwamba wafuasi wao wanapatikana popote hata kwenye mabus na stand siijawahi kumuona padre wa RC wala askofu achilia mbali shemasi akihubiri barabarani. Nadiriki kusema na kuamini kwamba hawa wanaofanya mahubiri yao barabarani na kwenye mabasi ni walewale wenye asili ya kuhani musa na mzee wa upako.
Waislamu, hawa shughuli zao huishia misikitini na kwenye makusanyiko ya warming wao. Japo na wao wanatumia vipaza sauti ambazo mara nyingi huwa ni kero kwa wasiohusika lakini hutolewa kwenye maeneo maalum tu.
Wapagani na wasio na dini, hawa ni pamoja na wqnaoamini katika miungu ya kale (waliowengi hawajitanabahishi) lakini hukereka sana na wapo wengi.
Unakuta mtu mmepanda kwenye usafiri wa umma au mkiwa stand kila mtu akielekea kwenye mambo yake tena na mawazo tofauti mtu anawasha speaker yake ya mchina na kuanza kuhubiri dini? Aliyewambia mungu yupo kwenye daladala au standi ni nani?
Ni kweli kuna uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa sheria lakini kila uhuru unamipaka yake. Kwa kutambua hilo ndo maana serikali imetenga maeneo maalumu ya kufanyia ibada ambako warming hukutana huko na kumuomba huyo mungu.
Utaratibu wa kuhubiri kwenye mabasi ya umma na vituo vya mabasi ni utaratibu holela na unakiuka haki za watu wengine wasiopenda kusikia habari za Mungu kwa wakati huo.
Wale mnaowapa pesa watu hawa pia mngezielekeza pesa zenu kwa wahitaji moja kwa moja ili zimfikie huyo mungu na mupate baraka muwe na mafanikio zaidi hata kama wengi wenu ni wezi wa mali za umma, waongo, wazinzi, waasherati na wasengenyaji (baada ya kutoka kwenye nyumba za ibada).
Uhuru wako uishie mwisho wa pua yako, vinginevyo ni vurugu!
Nawasilisha.