Ni mahubiri ya Utajiri, Mafanikio na Miujiza, Watu wanamtegemea Mchungaji Eliona Kimaro na kusahau injili ni Shida na Mateso

Huliza

JF-Expert Member
May 5, 2017
392
982
Ni utamaduni mpya kabisa wa mahubiri ya Utajiri, Mafanikio na uponyaji tu na Miujiza unaopingana na Imani ya Msalaba,

Eliona Kimaro na baadhi ya watu waliojipa utume na unabii wamelenga kwenye mahubiri ya uponyaji, utajiri, Miujiza na Mafanikio hivyo kuwaaminisha wafuasi wao kuwa njia ya Msalaba na msingi wa imani yetu ni kitu rahisi sana

Imani ya kikristo sio rahisi, Manabii na Mitume walipitia Mateso na shida,

1. Mtazame Ayubu maisha aliyoishi
2. Mtazame Stefano alipigwa mawe, 3.Mtazame Yohana alikatwa kichwa
4. Mtazame Masihi mwenyewe alisurubiwa

Imani ya kikristu inajengwa na Msalaba yaani njia ya Mateso, Njia ya kujitoa sadaka kwa ajili ya Wengine, Ni njia ya maumivu kuelekea ukombozi wa mwanadamu

Hutasikia hawa wachungaji wa kisasa wakienda hospitali ya Muhimbili, Mlongazila au Taasisi ya mifupa Moi kwenda kufanya miujiza na uponyaji wanayowadanganya wafuasi wao wakiwa kanisani

Kama kweli imani ya kikristu inajengwa na utajiri, Mafanikio, miujiza na uponyaji wachague siku moja waende pale Taasisi ya mifupa Moi au pale Muhimbili wakafanye miujiza watu wote wapate uponyaji na kutembea

Tangu enzi za kale manabii waliteuliwa na hawakujiteua wenyewe, Manabii walitumwa kwa kazi maalum na wala hawakujisifia wao

Yohana Mbatizaji au John the Baptist alifanya kazi kubwa ya kumuandalia masihi njia na alikuwa na wafuasi wengi sana lakini hata siku moja hakujisifu kuwa Yeye ndio Yeye mbele ya wafuasi wake, Alibatiza mamia kwa maelfu ya watu

Umaarufu wa Yohana mbatizaji haukumfanya ajione yupo juu ya watu wake na hata wanafunzi wake na wafuasi wake walipohamia kwa masihi hakukasirika

Yohana mbatizaji hata alipofuatwa Kuulizwa wewe Unafanya mambo makubwa hivi, Je wewe ni masihi au tumsubiri mwingine, Yohana mbatizaji alijibu kwa unyenyekevu na kujishusha kabisa kuwa Mimi sio yule, Aliye nyuma yangu ndio aliye mkuu kuliko mimi

Watu wanapoamua kubeba mabango ili mchungaji asiondolewe inafikirisha sana kwenye Misingi ya imani ya kikristo inayojengwa kwenye Msalaba yaani imani yetu tunapitia shida na Mateso kuelekea ukombozi na hata masihi alipitia njia hiyo hiyo ya shida na mateso

Kabla ya huyo mchungaji kulikuwepo watu wengi wamepita na kuondoka na hata Ukitaka abaki atazeeka na kustaafu ataiacha imani ya Msalaba

Wakristo hatuwezi kukwepa njia ya Msalaba, Njia ya Mateso, Kifo na ufufuo

Cha kushangaza na kuchekesha
Mtu anakurupuka alikotoka anajiita mimi ni Nabii alfa na Omega, Yaani Yeye ni nabii mwanzo na mwisho hakuna Wengine zaidi yake

Wakristo tuache kuwaamini wanadamu, Imani ya kikristu haijengwi kwa kupitia Mchungaji au Padri, Imani ya kikristo inajengwa kupitia msalaba

Padri na mchungaji ni njia tu ya kusaidia watu kuelekea ukombozi lakini wao wasitake kutengeneza Umaarufu nje ya Misingi ya imani ya Msalaba yaani shida, Mateso, Kifo na ufufuo
 
Walioko vijijini wanahamia mjini. Unabii/Uchungaji huo uwazao ulikuwa zamani ipo miji iliyojengeka Tanzania kutokana na wamisionari kufika kule miaka hiyo.

Maeneo hayo yalikuwa mapori sana na ya kutisha (mfano Ifakara - Kilombero / Ndanda - Kusini / Peramiho - Kusini / Singida / Tabora etc leo hii ni miji mikubwaa kutokana na kukaa kwao.

Zama zabadilika yabidi nao wabadilike
 
Walioko vijijini wanahamia mjini. Unabii/Uchungaji huo uwazao ulikuwa zamani
Ipo miji iliyojengeka Tanzania kutokana na wamisionari kufika kule miaka hiyo. Maeneo hayo yalikuwa mapori sana na ya kutisha (mfano Ifakara - Kilombero / Ndanda - Kusini / Peramiho - Kusini / Singida / Tabora etc leo hii ni miji mikubwaa kutokana na kukaa kwao.

Zama zabadilika yabidi nao wabadilike
Kwani Missionary ya Peramiho haipo si bado ipo na wazungu waanzilisha walishakufa na kuondoka

Kwani missionary ya Ndanda haipo si bado ipo

Lengo la Mission lina maana kufikisha ujumbe kule ambako haujafika

Imani inaendelea kwa kuwa watu hawakuwafuata wale wazungu huko Peramiho na Ndanda bali walifundishwa msingi wa imani ya msalaba

Peramiho na Ndanda Leo inaongozwa na watu weusi mfano Ndanda kuna Abate mweusi na Imani yao inasonga mbele

Usijaribu kutegemea mwanadamu kiimani

Hilo lengo lipo mpaka Leo kwenye kanisa la Wakatoliki, Kuna sadaka maalum kabisa na siku maalum kabisa Katika litrujia ya imani yao Katika mwaka ambapo wanakusanya michango kwa ajili ya umisioni yaani kupeleka injili sehemu zisizofikika

Hao Wakatoliki unaowaongelea kwa kutaja Ndanda na Peramiho chini ya Benedictine mission bado umisioni haujakoma

Ujenzi wa makanisa kwa kupitia wazawa wanaufanya Wakatoliki kila siku na wanajitahidi kuweka kanisa kila mahala kuwapunguzia umbali waumini wao

Kila siku wanaletewa mapadri wapya hata padre ukimpenda sana na hata akafanya muujiza, Siku yake ya kuhama Ikifika anahamishwa tu huko katoliki, Padri aliletwa pale sio kutafuta umaarufu

Sasa hizi imani mpya za kumlilia mchungaji au Padri asiondoke ni imani mpya kinyume na Imani ya kikristo
 
Kwanza si kweli kuwa Injili ni mateso, hii ndio lugha ambayo mzungu alituletea mwanzo,
Baada ya watu kuelimika na kuisoma Biblia wenyewe ndio walipopata ufahamu kuwa Injili ni ya furaha, utajiri na umaskini ni laana kuu!
 
Kwanza si kweli kuwa Injili ni mateso, hii ndio lugha ambayo mzungu alituletea mwanzo,
Baada ya watu kuelimika na kuisoma Biblia wenyewe ndio walipopata ufahamu kuwa Injili ni ya furaha, utajiri na umaskini ni laana kuu!
Yesu alikataza watu kua matajiri, yupo aliyeambiwa auze mali zake zote, pia alisema tajiri ni ngumu kurithi uzima wa milele etc
 
Kwanza si kweli kuwa Injili ni mateso, hii ndio lugha ambayo mzungu alituletea mwanzo,
Baada ya watu kuelimika na kuisoma Biblia wenyewe ndio walipopata ufahamu kuwa Injili ni ya furaha, utajiri na umaskini ni laana kuu!
Injili Ni furaha
Si furaha ya kufurahia Mali zilizokuzunguka
Furaha ya kuishi kwa amani na upendo na waliokuzunguka
Furaha ya Rohoni sio ya mwilini

Maisha ya upendo kwa wote Ni maisha yasiyo na furaha ya mwili, Ni mateso!
Kujitoa kusaidia watu Ni mateso,
Hakuna utajiri utakaa kuumiliki kwa maisha ya kujitoa kusaidia watu

-Ukiwa waziri hutaiba mabilioni ya serikali, utayaachilia yakahudumie watu

-Ukiwa mwanasheria hutadai milioni kumi kutetea watu kesi zao za haki, na hutapokea hata shilingi kutetea watu waovu
-Ukiwa Dactari utatibu bila kudai pesa za ziada
-Ukiwa Askari barabarani hutachukua pesa yoyote kwa raia
-Ukiwa mchungaji utaishi kipadre, hutadai sadaka za kukutajirisha kwa kuwadanganya waumini kuwa wewe Ni nabii na unaponya na kufufua watu
-Ukiwa mfanyabiashara utauza bidhaa kwa Bei nafuu, utalipa Kodi bila kukwepa, hautauza bidhaa feki, bidhaa zenye kuleta Kansa, madawa ya kulevya, pombe Kali, sigara, bunduki na mabomu visingeuzwa
Viwanda vingeunda bidhaa zenye tija kwa binadamu wote, bidhaa imara zenye kudumu

-Injili inaelekeza kuwasaidia wenye shida

-Ili upate utajiri lazima uwakwepe wenye shida!
Leo hii ombaomba anapewa sh. 200 akiingia kwenye duka la hardware pale kariakoo my

Mwenye kuifuata injili, lazima afe maskini lazima ateseke
Injili haina ubinafsi Bali Ni kujali wengine

Injili ingefanikiwa kushikwa na walimwengu wote, Kama lengo la Yesu alivyotaka, dunia ingekuwa yenye furaha ajabu
Shetani amevuruga ameshinda
Leo hata wahubiri wa injili wameweka mbele Mali na si utu
Wanatangaza enjili imekuja ili watu wawe matajiri
Utawezaje kuwa tajiri bila kukusanya Mali za wenzako?
Watu wote duniani wanaweza kuishi kwa furaha ya pamoja, Ila watu hawawezi kuishi kwa utajiri wa pamoja



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom