adriz
JF-Expert Member
- Sep 2, 2017
- 15,479
- 33,509
Hakuna dini imeheshima watumwa na kufanya harakati za kuukomboa utumwa kama Uislamu na Qu'ran imewahurumia sana watumwa nenda upande wa pili Bible verses kuhusu utumwa na watumwa utasikitika na kushika kichwa.Kuuliza si ujinga:Kwa nini Quran inazungumzia watumwa/utumwa ndani ya jamii kwamba ulikuwepo/walikuwepo?Ukiwa muislam,unautafsiri vipi utumwa?Je,watumwa nao wanaruhusiwa kujinasibisha na kuiona Quran ni yao?
Utumwa ni tamaduni ambayo ilikuwepo toka zamani na ilikuwa imeenea na kawaida karibia pande zote Duniani . Watu kabla ya Uislamu Uarabuni watumwa walikuwa wanachukuliwa kama Wanyama hawana nafasi yeyote kwenye Jamii na anayemmiliki anaweza kumuamrusha na kufanya chochote bila Kuzingatia utu na mipaka yake.
Qur'an na Uislamu ukaja kuweka mambo mbalimbali na kuondoa Sheria kandamizi kuhusu watumwa mfano kufanyishwa biashara ya ukahaba