Toka Turkey mwaka 2015 namba 106 kiuchumi katika nchi masikini za ulimwengu wa tatu hadi nchi za G20 bora kiuchumi duniani chini ya chama cha AKP chini ya uongozi wa Rais Recep Tayyip Erdoğan.
Turkey imetoka kuwa nchi iliyoyokuwa imeelemewa na deni la taifa la kiasi cha dola 50 bilioni na sasa kuwa taifa lililojinasua kutoka mzigo huo na kuifanya sasa kuwa nchi tajiri kutoka hapo mwanzo ilipokuwa duni kiuchumi miaka 20 iliyopita .
Turkey inazalisha bidhaa nyingi za kiviwanda za kibinadamu pia viwanda vya kijeshi vya kutengeneza silaha nchini Turkey za kisasa ikiwemo drones zilizoipaisha hadi silaha zilizotengenezwa Turkey kuonekana katika viwanja vya vita mfano nchini za Syria, Azerbaijan na hadi ktk vita vya Ukraine na Russia
Ugunduzi wa nishati katika Bahari Nyeusi /Black Sea kumegunduliwa gesi nyingi 2023.
Dola ya Ottoman ilianguka miaka 100 iliyopita 1923 lakini sasa dola ya Ottomania inaonekana kuweza kurejea.
Duniya ya kiIslamu inategemea na kufuatilia uchaguzi huu wa jumapili tarehe 14 mwezi Mei 2023 na kuweka matumaini ya dola ya KiIslamu kunyanyuka tena baada ya kuanguka mwaka 1923 na dola zisizo za kiIslamu kunyanyuka zaidi kuwa ndizo pekee zenye nguvu kubwa duniani .
Mchambuzi wa chaneli ya mtandaoni wa Sunkar Islamic anaendelea kuelezea mafanikio ya serikali ya chama cha AKParty
Rais Recep Tayyip Erdoğan uchaguzi huu amepata upinzani mkali kutoka kwa Kemal Kilicdaroglu wa chama cha Republican People's Party na historia mpya inaweza kuandikwa.
Uchaguzi huu unafuatiliwa kwa mapana, marefu na kwa kina na mataifa mengi maana matokeo yake yataandika historia mpya kwa dunia yetu ya leo.
HISTORIA
Mchambuzi wa chaneli hii ya Sunkar Islamic Channel anaturejesha katika Surah Al-Qasas Ayat 5 kuwa katika kipindi kigumu kutoka udhalilifu na kuibuka washindi kwa waumini wa kiIslamu duniani nzima iliyoanza mwaka 1423 hadi 1923 na kwa miaka 600 ilitapakaa ulaya, Mashariki ya kati na bara Afrika kabla ya kudhoofishwa mwaka 1923 kwa kusalimu amri.
Mkataba wa Laussanne uliasisi Republic of Turkey ikimaanisha mwisho rasmi wa dola ya Ottoman kwa kuikata vipande vipande ikaishia kutoka dola kubwa hadi kipande cha nchi ya Turkey ya sasa.
Wahafidhina walibanwa kuoonesha aina yoyote ya uIslamu ikuwemo kupiga marufuku hata adhana kwa lugha ya kiarabu toka 1923 hadi 1959 ilipofanikiwa kurudishwa utamadumi wa lakini serikali ya wakati huu iliyopigania kurudisha tamaduni hizo za KiIslamu jeshi likaingilia na kupindua serikali mwaka 1959.
1994 Instabul mji mchafu kupita yote ulaya hadi kuwa mji msafi unaonukia manukato kupitia chama cha Uadilifu na Maendeleo cha AKParty
2023 uchaguzi wa Turkey unaotizamwa na duniya nzima kwa ukaribu kutokana na historia ya mivutano ya kambi tofauti duniani zinazotafuta kupenyeza ushawishi wao wa kidola, kitamaduni na kijeshi.
Source : Sunkar Islamic Channel