Kwanini tunapenda kutuma pesa (kwa njia ya simu) kuliko benki ambazo huwa na gharama nafuu?

Mi sipendi kabisa kutuma pesa kwa simu
Wezi sana mitandao
Kitu kizuri umeweka na kiasi,

Imagine unatoa elfu kumi wanakata 1000, ambayo ni 10% Hii si ni balaa kabisa na bado wadau wanakomaa huko huko
Mimi ukiona nimekutumia pesa kwenye simu ujue:
1. Gharama ya mimi kuja na kukupatia plus gharama ya muda ntakaotumia kuja ni kubwa kuliko gharama ya mimi kutuma na wewe kuitoa.
Au labda wewe huko uliko hakuna namna nyingine ya kupata huduma.
 
Hili la kusema watu wengi hudhani kuwa benki ni kwa ajili ya watu fulani ni sahihi kabisa. Ndio maana watu wengi hawana account za bank. Lakini watu hao wengi wasio na bank accounts wana miliki simu na wanapokea na kutuma fedha kupitia accounts za simu.

Iko hivi, watu wengi hawana taarifa sahihi juu ya matumizi ya accounts za bank. Kuna rafiki zangu siku moja walikua wanang'ang'ania kuwa wataendelea kutumia CRDB kwa sababu ipo kila mahali...mimi nikawaambia sitaitumia sababu muda mwingi naishi Dar es Salaam. Je, ukienda mkoani? Nikawajibu, ni mara ngapi kwa mwaka naenda mikoani? Na nikienda hata robo mwaka haifiki narudi hapa hapa. Zaidi ntakaa week 2 tena za likizo. Kuna bank kuhamisha pesa toka bank kupeleka Tigo/voda ni bure ila kila mwisho wa mwezi unakatwa sh 250/- hata kama wamepandisha siku hizi, basi tuseme 500/- bado ni nafuu sana.

Lakini kwa nini utumie simu? Wakati kuna visa?
Kuna bank kutoa kwa visa unakatwa sh 3,000 bila kujali kiasi unachotoa. Wakati tigo kutoa laki 2 ni elfu 5. Kuna kipindi mzee alikua anaumwa kalazwa hospitali, na mimi ndio nilikua caretaker. Kuna gharama kule hospitali haziko kwenye bima, sasa ndugu na jamaa wakawa wanataka wanitumie pesa kwa simu, haki nakwambia niliwapa account yangu ya bank. Mtu akihoji niende kwa bank muda huu sijui bla bla namwambia nenda kwa wakala niwekee juat like unavyoenda kuweka tigopesa.
Ilisave sana gharama za kutolea pesa. Maana nikienda ATM navuta laki 2 mpaka 4 kwa buku wakati tigopesa ningetakiwa niwaachie elfu 10 hapo.

Cha msingi ni taarifa.
Nimejifunza kitu...sisi watu weusi hatuna hesabu za hela.
 
Bank na makampuni ya simu wanakosea kuweka Gharama Kubwa kutoka kwenye simu kwenda benki....wakiweka rate ndogo itavutia hata watu wa kipato cha chini kuweka PESA benki tena Mara kwa Mara, ndio itavutia watu kutumia Benki zaidi...mi niliacha kutumia simu kwenda bank baada ya kuona natumia pesa nyingi zaidi. ...yaan nikituma hata elfu 20,000 nakatwa 2400...
 
Hii sio hypothesis, imeshakuwa proven kwa tafiti zilizofanywa na wengine wanaotafiti kuhusu poor economics.

Iko hivi ni rahisi kujua kuwa gharama za kutuma na kutoa fedha kwa kutumia simu, iwe M-pesa, Tigo pesa nk ni gharama zaidi kuliko kutumia benki i.e ATM ambazo zimetapakaa nchini.

Kwa maeneo kama Dar, ATM zimetapakaa maeneo mbalimbali na zaidi benki nyingi zinatumia mitandao mikubwa kama VISA, MASTARCARD, MAESTRO nk ambayo haikupi ulazima wa wewe kutafuta benki yako ili kutoa fehda.

Mbali na hayo bado watu wamekuwa wakitumia zaidi mitandao ya simu ambayo ina gharama kubwa za huduma zao kuliko benki, Je shida iko wapi.

Wewe kama mdau unayetumia simu kufanya miamala, Je unadhani ni kipi kinakufanya ukae humo ukizingatia gharama ni kubwa?

Nadhani watu wa benki wanaotengeneza mifumo ya masoko wanaweza kuwa na njia nzuri ya kuweza kujua namna gani ya kuwanasa watu ambao wanatumia simu badala ya benki ambazo zina gharama nafuu.

Hypothesis: Watu hawatumii benki kwa kuwa benki zinaonekana kama ni za watu fulani wenye hadhi na fedha nyingi (It can be tested)

Au ni kuwa watu huwa hawana muda wa kujua kuhusu gharama za masuala ya kifedha.

Signed

Oedipus

Benki na ATM zao hawaaminiki.
  • ATM hazijatapakaa kama mawakala kila sehemu kama unavyosema
  • Changamoto ya kutafuta usafiri kuzifikia hizo ATM zilipo ni kubwa
  • Kutotabirika kwa uwepo wa huduma kwenye ATM ni jambo jingine, unatoka mbali unafika ATM mbovu gharama kutafuta nyingine ni kubwa
  • Ni rahisi kushikana shati na wakala kama fedha haijaenda kuliko ATM
 
Kitu kizuri umeweka na kiasi,

Imagine unatoa elfu kumi wanakata 1000, ambayo ni 10% Hii si ni balaa kabisa na bado wadau wanakomaa huko huko
Hoyo 1000 ni sawa na nauli ya kwenda kuitafuta ATM ilipo
 
Wezi sana mitandao

Mimi ukiona nimekutumia pesa kwenye simu ujue:
1. Gharama ya mimi kuja na kukupatia plus gharama ya muda ntakaotumia kuja ni kubwa kuliko gharama ya mimi kutuma na wewe kuitoa.
Au labda wewe huko uliko hakuna namna nyingine ya kupata huduma.
Hapa ndio jibu la mada lilipo. "Convenience"

Na si watu wengi wenye bank account. Kuna shughuli nilishafanya na watu 20 mikoani huko. Kati yao waliokuwa na account bank ni wawili tu lakini kila mmoja ana mzunguko wa pesa wa kuzidi sh. 300,000 kwa mwezi.
 
Kwa Dar ni usumbufu ulioje kusafiri hadi benki au kwenye ATM.
Ila hata ughaibuni, kama kuna uwezekano wa kufanya malipo mitandaoni, hakuna anayesumbuka kwenda benki na gharama, iwe benki au mitandaoni ni bure kwa mlio ndani ya nchi moja, ya kimataifa unaweza kuchajiwa.
 
Benki na ATM zao hawaaminiki.
  • ATM hazijatapakaa kama mawakala kila sehemu kama unavyosema
  • Changamoto ya kutafuta usafiri kuzifikia hizo ATM zilipo ni kubwa
  • Kutotabirika kwa uwepo wa huduma kwenye ATM ni jambo jingine, unatoka mbali unafika ATM mbovu gharama kutafuta nyingine ni kubwa
  • Ni rahisi kushikana shati na wakala kama fedha haijaenda kuliko ATM
Yaani mara mtandao uko chini,
Mara hakuna salio,
Mara kadi imemezwa shida zote hizi za nn??
Mara foleni ukifika teller kafunga dirisha anaenda lunch...

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Niwe mkweli tu kwa sasa nimeacha kabisa kutuma pesa kutoka bank kwenda mpesa na kutoka mpesa kwenda bank hebu fikiria kutuma 1million kutoka bank kwenda mpesa ni 12k. na hapo mpesa hujaitoa. Wakati kutoa cash kwenye atm 400k max ni 1200 +vat jumla 1800, for 1m ni sh 5.2k,
 
Hapa ndio jibu la mada lilipo. "Convenience"

Na si watu wengi wenye bank account. Kuna shughuli nilishafanya na watu 20 mikoani huko. Kati yao waliokuwa na account bank ni wawili tu lakini kila mmoja ana mzunguko wa pesa wa kuzidi sh. 300,000 kwa mwezi.
Convenience kwa hapa Dar hujaniambia bado. Wakala wa banks wapo kila kona. Hivi unadhani kwanini banks ziliweka mawakala? Convenience
 
Bank bado zina utaratibu wa utoaji huduma wa karne 19 na hii ni karne ya 21. Accounts yako ukaifungulia dar alaf ikaja kufungwa na ukitaka kuifungua kama upo arusha itakuchukua muda mwingi hadi ije kuanza kutumika.
 
Convenience kwa hapa Dar hujaniambia bado. Wakala wa banks wapo kila kona. Hivi unadhani kwanini banks ziliweka mawakala? Convenience
Tozo za kutoa pesa kwa wakala wa benki sidhani kama zinatofautiana sana na hizi za makampuni ya simu. Wacha nilifuatilie hili kwanza.
 
Zina
Tozo za kutoa pesa kwa wakala wa benki sidhani kama zinatofautiana sana na hizi za makampuni ya simu. Wacha nilifuatilie hili kwanza.
Tofautiana sana. Tena sana. Kutoa laki 2 ni elfu 5 kwa simu. Wakati ATM au wakala wa bank haizidi elfu 2.
 
Kiongozi, Chukulia mazingira ya Dar, Jinsi ambavyo ATM ziko maeneo mengi tofauti tofauti, plus unaweza kutoa hela kwa mawakala wa huduma za kifedha kama fahari Huduma na Nmb wakala
Hivi ulishajiuliza ni waTZ wangapi wana bank akaunti na ni wangapi wana simu?

Hivi unajua waTZ wengi hawana hela ya kukaa kwenye bank akaunt? Wana hela kiasi tu na iko kwenye mzunguko daily

Pia kwa hicho hicho kidogo tunasaidiana shida zetu za hapa na pale. Mfano hela ya kula, hela ya vocha, nauli, hela ya bia n.k

Halafu mlichobugi zaidi nyie watu wa bank, kwa mawakala mmeweka chaji kubwa kuliko ndani. Tena hao Fahari huduma ndo sitaki hata kuwasikia. Yaan nyie badala muweke gharama kiduchu huku kwa mawakala ili tukimbilie huko, nyie mnatukomesha.

Na migharama yenu ya ajabu ajabu inafanya watu wachukie bank. Yaan hela zangu halafu eti kuangalia salio tu unanikata, nikitaka statement tu hata ya miamala 5 tu napo mnakata looh!!

Kwa wajanja benk zimebaki za kupokelea tu mshahara kisha natoa zote nahifadhi mahala au natumia mdogo mdogo kwenye simu.
 
Back
Top Bottom