Kwanini tunampoteza Kabila Kwa sababu ya Kagame?

Kwanini tunampoteza Kabila Kwa sababu ya Kagame?

Hoja hafifu inayojengwa juu ya proposition kwamba kuwa rafiki na Rwanda ni kujenga uadiui na Congo. Naona wote wanaweza kuwa rafiki zetu.
Rafiki zako kihivi wewe unamsahidia Jirani yako mmoja kumwathibu mtoto wa Jirani mwingine alafu unaanzisha urafiki na Jirani yako ambaye nawewe uwa unausika kuwapiga watoto wake wakiwa Kwa Jirani yako mwingine?
 
Kweli education for riberation yaani siamini kama hili ndilo mlilo liona tatizo sasa mnatakaje nyie mbna kila kitu kwenu ni tatizo
 
Mtoa mada hajui hata umuhimu wa standard gauge rail
Hii ni hatari sana
 
Hii analysis sijaielewa na kwanza kwa kuonyesha tu mtoa mada ni mtu asiye makini angalia hiyo population ya Rwanda. Ameshindwa hata kwenda Google kujiridhisha. Hapo tayari una question uwezo wake wa kujenga hoja vizuriii....
Whatever the population figure he wrote still Congo has much more to Rwanda
 
ni kweli atakuwa amekosea kwenye population lakini ana hoja kwanin tuache soko la watu karibia milion 80 la congo na tukae karibu na watu 10m wa rwanda
Soko linaachwa vipi? Chukua muda kidogo uangalie ramani. Kuna njia nne kwenda DRC kutokea Dar

1)SGR itakayojengwa - branch ya Rwanda - DRC
2)SGR itakayojengwa - branch ya Burundi - DRC
3)SGR itakayojemngwa - Kigoma-Ziwani-KalemieDRC
4)Tazara - Zambia pandisha copperbeltDRC

Wanaachwa wapi?
 
Lakini VAT imeanza mwezi wa saba..Upungufu wa mizigo umeanza kuonekana mwezi February.. Mbona sioni correlation hapo?????
Kwani ukiona moshi unafuka utasubiri nyumba ishike moto ndo ukimbie? dalili za mvu ni mawingu na panapofuka moshi chini panamoto; wafanya biashara wanafanya risk analysis na since election na mkemia alipoanza kutoa miongozo majukwaani smart guyz wakaplay smart from january on ward na hiki ndo tunakiona sasa.
 
Kwa hiyo kwa kufanya biashara na Rwanda maana yake tunajitenga na Congo? Nilijua kwamba kwamba hizi nchi zote zipo kwenye jumuia ya EAC na lengo ni wote baadaye tuje kufanya biashara pamoja.. Lakini kinachotokea sasa hivi wale members wa hii block walio tayari wanaunganisha nguvu wakati members wengine wanajipanga. Congo ataendelea kuwa mshirika wetu na pia tungependa na wengine wawe washirika wetu. Haya mambo ya kuzodoana zodoana na kutoaminiana ndo yanarudisha nyuma Africa. Congo bado haipo vizuri kimiundo mbinu kwa hiyo ni bora kuanza kushirikiana na wale walio tayari. Congo ni future potential ally bado ni sleeping giant..
Nimekuelewaa
 
Labda nikuulize tu swali dogo sana hivi kwa mfano kusingekuwepo hiyo nchi ya Congo inamaana Tanzania ingekuwa masikini na isinge songa mbele kimaendeleo? Yaani " Jitu " kabisa kama Wewe unakuja humu kulia lia kwa Rasilimali za nchi za Wenzako wakati Wewe hapa hata tu nusu ya Rasilimali zako ambazo pengine kama ungezitumia vyema na kuwa na usimamizi nazo mzuri leo hii Tanzania ingeshindana na South Africa, Egypt na hata nchi baadhi za huko Ulaya na Wewe kuondokana na kumpa lawama Rais wangu mpendwa Paul Kagame wa nchi yangu ya maziwa na asali ya Rwanda.

Huwa sipendi kuwadharau baadhi yenu humu lakini kwa aina hii ya uwezo wenu mdogo sana wa kufikiri mliona hakika sitoacha kuwadharau na mtanisamehe kwa hili tafadhali. Najua argument yako juu ya hili ni too geographical than strategical. Umeona kuwa pengine Tanzania ingefaidika sana na Congo ya Kabila kwakuwa tu nchi yenyewe ni kubwa na ina Watu wengi lakini ukasahau kwamba inawezekana hawa Rwanda wakawa wadogo Kijiografia na kiidadi ya Watu lakini kimkakati wakawa na faida kubwa sana Kibiashara na Tanzania hata kuliko hao Congo.

Siku nyingine ukija humu na Mada zako jitahidi kwanza kufanya utafiti ili ueleweke vizuri na Watu ambao Mwenyezi Mungu alitubariki upeo mkubwa na akili nyingi tokea tukiwa hatujazaliwa. Kwa kukusaidia tu na nakuomba nenda pale Bandarini au maeneo mengi ambapo kuna Wafanyabiashara wa kutoka Congo ndipo utajua kuwa hawa Watu ni " mikosi ". Wakongo naturally ni Matapeli na Wasanii sana na hupenda mno " kitonga " a.k.a dezo dezo katika mambo yao mengi na hili halina ubishi kwamba katika Wafanyabiashara ambao waliichafua Bandari yetu ya Dar ni hawa wa Congo kutokana na Utapeli na Ujanja Ujanja waliokuwa wakiufanya hadi Mkombozi wetu Rais Dkt. Magufuli alipokuja na kuwadhibiti.

Rwanda inaweza kuwa ndogo na ukaidharau lakini kwa kukusadia tu na hili hata Watu wa TRA watakusaidia ni kwamba hakuna Wafanyabiashara ambao ni wakweli na wana nidhamu ya Kibiashara kama wa kutoka nchini kwetu Rwanda na labda badala ya kutudharau na kutudhihaki hivi kupitia Rais wetu Paul Kagame nadhani ungetuomba radhi na kutushukuru kwani Wanyarwanda hawajawahi kukwepa kulipa Kodi yoyote ile stahili katika Biashara zao wanazozifanya au kuzipitisha hapa Tanzania.

Hivi ni lini mtaishukuru Rwanda nyie? Rwanda tumewakosea nini? Mbona Mataifa mengine yanayowatieni Umasikini na bado mnayakumbatia tu hamuyasemi? Kuna chochote mnatudai Rwanda ili kama vipi tuwaombe Mkopo Wordl Bank na IFM ili tuwalipeni? Hivi ni kweli hakuna jema ambalo Rwanda tunalo na nyie Watanzania mnaweza kuliiga ili nanyi pia liwasaidieni? Rais Dkt. Magufuli kuonekana kumkubali Rais wetu Kagame ni dhambi? Nyie ni nani kumpangia Rais achague Marafiki? Mbona huyo " aliyestaafu " aliwakumbatia INTARAHAMWE na kuwa na ushikaji wa kupitiliza na Nkuruzinza lakini mlikuwa kimya hata pale tu nchi kubwa za Ulaya na Marekani zilipokuwa zinaishutumu Burundi na huyo Rais wake?

Please give us a break and mind your own business.
What is business?
 
Mtoa mada kuna kitu hakijui kuhusu reli ya kati. Reli ya kati inaanzia Dar-es-salaam mpaka Tabora inagawanyika moja inaenda Mwanza kupitia Isaka(bandari ya nchi kavu), nyingine inaenda Kigoma na nyingine inaenda Kasanga. Kwa mujibu wa mradi hii ya kwenda Mwanza itachepuka ambacho moja itaenda Rwanda na Burundi kupitia Kahama-Geita-Kagera(upembuzi yakinifu ushafanyika miaka mingi iliyopita toka enzi za Kikwete). Ile ya Kigoma inaishia bandari ya Kigoma ambapo Kigoma inaunganisha Kongo(uvira) na Burundi(Bujumbura) kibiashara. Hii ya kwenda Mpanda Rukwa inaishia Bandari ya Kasanga ambayo inaunganisha Tanzania na Kongo(Lubumbashi) kibiashara. Kwa hiyo wazo la raisi ni zuri kwa sababu ujenzi wa reli utaimarisha soko la usafirishaji mizigo wa ndani (Kigoma, Rukwa, Katavi, Tabora, Dodoma, Shinyanga, Kahama, Mwanza, Geita, Kagera), Pia tutaimarisha soko la nje Uganda, Rwanda,Burundi na DRC. Mpango wa ujenzi wa reli hii kwa standard gauge sio mpya ulikuwepo toka enzi za JK. My Take tusiwe watu wa kupinga kila kitu, wakati mwingine tufanye research kwanza. By Sammy
 
Mtoa mada kuna kitu hakijui kuhusu reli ya kati. Reli ya kati inaanzia Dar-es-salaam mpaka Tabora inagawanyika moja inaenda Mwanza kupitia Isaka(bandari ya nchi kavu), nyingine inaenda Kigoma na nyingine inaenda Kasanga. Kwa mujibu wa mradi hii ya kwenda Mwanza itachepuka ambacho moja itaenda Rwanda na Burundi kupitia Kahama-Geita-Kagera(upembuzi yakinifu ushafanyika miaka mingi iliyopita toka enzi za Kikwete). Ile ya Kigoma inaishia bandari ya Kigoma ambapo Kigoma inaunganisha Kongo(uvira) na Burundi(Bujumbura) kibiashara. Hii ya kwenda Mpanda Rukwa inaishia Bandari ya Kasanga ambayo inaunganisha Tanzania na Kongo(Lubumbashi) kibiashara. Kwa hiyo wazo la raisi ni zuri kwa sababu ujenzi wa reli utaimarisha soko la usafirishaji mizigo wa ndani (Kigoma, Rukwa, Katavi, Tabora, Dodoma, Shinyanga, Kahama, Mwanza, Geita, Kagera), Pia tutaimarisha soko la nje Uganda, Rwanda,Burundi na DRC. Mpango wa ujenzi wa reli hii kwa standard gauge sio mpya ulikuwepo toka enzi za JK. My Take tusiwe watu wa kupinga kila kitu, wakati mwingine tufanye research kwanza. By Sammy
Wewe ujanielewa na wewe ndio ujui kinachoendekea Rwanda inafadhiri waasi ambao wanasumbua serikari ya Rwanda kitendo tu cha sisi kushirikiana na Rwanda ni sawa na kusaport waasi ambao na sisi tulituma majeshi kwenda kuwadhibiti ndio maana unaona wafanya biashara wa Congo wameamia beila msumbiji
 
Kama ni kweli Rais wetu anamsikiliza Paul Kagame kama mshauri wa baadhi ya mambo hasa swala la kuifufua ATCL na Bandari naamini Kagame bado ni Tatizo na atakuwa na masilai binafsi na si vinginevyo!!
...Imani yako ni potofu. Kufufuka kwa ATC ni faida ya Tanzania. Kufanya vizuri kwa bandari ni faida kwa Tanzania. Ainisha hayo maslahi binafsi.

...Ukweli ulipo. Rwanda wanahitaji njia ya kupitisha mizigo mizito kwa gharama nafuu kuelekea bahari ya Hindi. Kama itakuwa Dar, sawa. Kama itakuwa Mombasa, haya.

Kagame pamoja na kushinda kwenye Mijadala ya kimataifa akiongelea maswala ya uchumi kama " Global Economic Forum"
Lakini bado anashauri ushauri wa kizamani kabisa kujenga mfano swala la kujenga Reli (standard gauge) kwenda nchini kwake nchi ambayo ina watu kama 10milioni+
...Mtu "akikushauri" ujenge reli -maana mpango wa kufufua reli ni wa muda mrefu- anakuwa katoa ushauri wa kizamani zamani?

...Unafahamu kwamba kiasi kikubwa cha hiyo reli kiko Tanzania. Kwani sie hatuna matumizi au mahitaji ya reli bora na ya kisasa?

Baada tungefufua reli ya TAZARA ambayo ingeweza kuwafikia watu zaidi ya 150milion+ kutoka Zambia, Malawi, Zimbabwe na nchi zingine !!.
...Hauna habari kuna mpango wa kuifufua Tazara, na waChina wanahusika moja kwa moja? Zimbambwe hana haja ya Tazara, labda kama kuna dharura, yeye anaijua Beira na Durban. Zambia na Congo Kinshasa ndio wadau wakubwa wa Tazara.

Hilo lingefanya bandari yetu iweze kuwa busy kuzihudumia nchi zaidi ya 10 Kusini mwa Jangwa la Sahara kuliko sasa!!
...Nchi kumi zipi, kuhudumiwa na Tazara? Can you list them?

Ambapo hata Kongo imeanza kututilia shaka kutokana na Urafiki wetu na Kagame Kwa sababu wakongo wanajua kabisa huyu jamaa huwa anataka urafiki wa masilai kwa nchi yake !!

Sasa nikisema Kagame anaihujumu bandari yetu nitakuwa nakosea ? Kwani mkumbuke bandari yetu jamaa alishaitaka toka zamani Kwa kutoa maneno ya kejeli kwa Rais mstaafu?
...Anaihujumu kivipi? Unahisi au una hoja yenye mantiki? Unaweza toa mfano wa hujuma mojawapo?

Nikisema reli itakayojengwa itatumia garama kubwa kwa manufaa ya watu wachache nitakuwa nimekosea?
...Reli ni yetu sie. Je, sisi tu wachache?

Nikisema uhusiano wetu na Congo umepungua baada ya kumkaribisha Kagame nitakuwa nimekosea?
...Unaweza toa ushahidi, hata wa kimazingira?

...Kipimo gani kimetumika kubaini kupungua kwa uhusiano?

Tuache unafiki Kagame anayajua haya yote na alikuwa na wivu sana enzi za Kikwete lakini sasa hivi atakuwa akijifungia anatuchekea sana!!
Kwanini Rafiki yetu asiendelee kuwa Rais wa Kongo kuliko Kagame !!
...Actually, wewe ndio mnafki.

...Vigezo gani vinatumika kuchagua "rafiki yetu"?

Yaani unapoteza nchi yenye watu milioni 80+ na kuikumbatia nchi yenye 10milion+ alafu unategemea biashara?
...Usichanganye mambo!
 
Alichosema mtoa mada kinaukweli kabisa,
...Mtoa mada amehusisha hoja ya mizigo kupungua bandarini na uhusiano wetu na Rwanda, kitu ambacho si sahihi.

Mimi ninauzoefu na baadhi ya miji ya Msumbiji ukiwepo mji wa Beira, na ni miezi 2 imepita nilikua huko, kwa hakika ukiona msongamano wa malori yenye plate namba za Congo, Zambia, Malawi na Zimbabwe yanayo ingia na kutoka bandari ya Beira basi utakubali kwamba Beira Porto wanafanya the Best
...Beira imekuwa ikitumiwa na hizo nchi kwa muda mrefu. Mizigo mingi ya Congo Kinshasa imekuwa ikipita huko zama na zama.

...We need to be competitive. Tusipokuwa, tutakimbiwa!

kwa sasa si sawa na miaka iliyopita, kutoka na hilo selikari ya msumbiji imeingia katika ujenzi wa utanuzi wa Barbara kutoka Beira mpaka njia panda inayokwenda boda ya Zimbabwe na Malawi/ Zambia takribani 600km. Hivyo makosa yetu yanaweza yakawa faida kwa wenzetu. TUJITAFAKARI.
...Ujenzi wa miundombinu kuelekea lango la bahari ni muhimu sana. The cost, should not scare us.

...Tuko pamoja!
 
Tuache chuki binafsi km vipi cdm mrudisheieni kagame pesa alizompa mbowe kule Nairobi mpk mkamtetea mbungeni
 
Hii analysis sijaielewa na kwanza kwa kuonyesha tu mtoa mada ni mtu asiye makini angalia hiyo population ya Rwanda. Ameshindwa hata kwenda Google kujiridhisha. Hapo tayari una question uwezo wake wa kujenga hoja vizuriii....
Hata kama takwimu zimekosewa kidogo ukweli ni kwamba ana hoja ya msingi sana
 
Kweli education for riberation yaani siamini kama hili ndilo mlilo liona tatizo sasa mnatakaje nyie mbna kila kitu kwenu ni tatizo
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hata urafiki wa Congo ulikua hauna maslahi zaidi kuwachosha wanajeshi wetu
 
Back
Top Bottom