Hoja ya kumhusisha Rais Kagame na kupungua kwa mizigo ya DRC bandarini Dar haina msingi. Waagizaji wa DRC wameikimbia bandari yetu kwa sababu mbili kuu ambazo zimetokana na maamuzi mabovu na yasiyojali maslahi ya taifa yaliyofanywa na watawala wa hii nchi. Moja ni kutoza VAT kwenye huduma za mizigo iendayo nchi jirani (ancillary transit cargo handling services) ambazo ni kupakua, kupakia, storage (bandarini), warehousing (bandari kavu) na kusafirisha mizigo. Hapo awali VAT kwenye hizi huduma haikuwepo. Pili ni makubaliano ya serikali za Tanzania na DRC kuanzisha single customs territory regime ambapo kodi zote zote za bidhaa za DRC bandarini zinakusanywa na TRA badala ya kukusanywa katika kituo cha mpakani DRC. Hii hatua haikuwafurahisha waagizaji wa DRC kwa sababu ina urasimu na usumbufu mkubwa. Sababu zote hizi mbili hazi-apply katika bandari shindani za nchi jirani. Kumbuka biashara ni mashindano na mfanyabiashara atakwenda penye huduma nafuu.