technically
JF-Expert Member
- Jul 3, 2016
- 13,656
- 58,559
Kama ni kweli Rais wetu anamsikiliza Paul Kagame kama mshauri wa baadhi ya mambo hasa swala la kuifufua ATCL na Bandari naamini Kagame bado ni Tatizo na atakuwa na masilai binafsi na si vinginevyo!!
Kagame pamoja na kushinda kwenye Mijadala ya kimataifa akiongelea maswala ya uchumi kama " Global Economic Forum"
Lakini bado anashauri ushauri wa kizamani kabisa kujenga mfano swala la kujenga Reli (standard gauge) kwenda nchini kwake nchi ambayo ina watu kama 10milioni+
Baada tungefufua reli ya TAZARA ambayo ingeweza kuwafikia watu zaidi ya 150milion+ kutoka Zambia, Malawi, Zimbabwe na nchi zingine !!.
Hilo lingefanya bandari yetu iweze kuwa busy kuzihudumia nchi zaidi ya 10 Kusini mwa Jangwa la Sahara kuliko sasa!!
Ambapo hata Kongo imeanza kututilia shaka kutokana na Urafiki wetu na Kagame Kwa sababu wakongo wanajua kabisa huyu jamaa huwa anataka urafiki wa masilai kwa nchi yake !!
Sasa nikisema Kagame anaihujumu bandari yetu nitakuwa nakosea ? Kwani mkumbuke bandari yetu jamaa alishaitaka toka zamani Kwa kutoa maneno ya kejeli kwa Rais mstaafu?
Nikisema reli itakayojengwa itatumia garama kubwa kwa manufaa ya watu wachache nitakuwa nimekosea?
Nikisema uhusiano wetu na Congo umepungua baada ya kumkaribisha Kagame nitakuwa nimekosea?
Tuache unafiki Kagame anayajua haya yote na alikuwa na wivu sana enzi za Kikwete lakini sasa hivi atakuwa akijifungia anatuchekea sana!!
Na ukizingatia Rwanda imekuwa ikituhumiwa na USA na UN kufadhiri waasi walioko nchini Congo amabao wanapambana na Majeshi yetu pia je huu urafiki wetu na Rwanda amuoni kama unaongeza sintofahamu Kwa uhusiano wetu na Congo?
Na inaweza ikawa sababu moja wapo inayofanya mizigo ya kwenda Congo imepungua bandarini kipindi hiki?
Kwanini Rafiki yetu asiendelee kuwa Rais wa Kongo kuliko Kagame !!
Yaani unapoteza nchi yenye watu milioni 80+ na kuikumbatia nchi yenye 10milion+ alafu unategemea biashara?