Van persie
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,099
- 719
Nimesikitishwa na kufedheheshwa na kitendo cha Televisheni ya Taifa[TBC 1] kukatisha matangazo ya mubashara wakati mama Samia Suluhu, Makamu wa Rais, alipokuwa akielezea mkanganyiko na kilichotokea Foreign siku za hivi karibuni na kupelekea Naibu Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashiriki kufutwa kazi.
Ghafla wakati Mama Samia anazungumzia kiini cha nini kimetokea, TBC 1 wakakata matangazo ya mubashara bila kueleza tatizo. Inaonesha ni makusudi tu. Baada ya hapo wakarudisha haraka mkulu alipoenda kwenye podium.
Hii censoring imenishangaza na kuniuzunisha. Kweli tumerudi kwenye nyakati za giza aisee!
Ghafla wakati Mama Samia anazungumzia kiini cha nini kimetokea, TBC 1 wakakata matangazo ya mubashara bila kueleza tatizo. Inaonesha ni makusudi tu. Baada ya hapo wakarudisha haraka mkulu alipoenda kwenye podium.
Hii censoring imenishangaza na kuniuzunisha. Kweli tumerudi kwenye nyakati za giza aisee!