Video: Wakili Boniface Mwambukusi akifafanua kisheria na kikatiba ni kwanini uteuzi wa Naibu Waziri Mkuu ni uvunjaji wa katiba ya JMT ya 1977

Uzima Tele

JF-Expert Member
Jan 20, 2023
1,104
2,349
NB: JF Moderators, naomba hii thread ijitegemee. Najua imeshajadiliwa lakini naona huyu wakili kaja kivingine. Tuwape watu nafasi wajadili hoja yake..

Back to the topic;

✍️Ni kweli Rais Ally Hassan Mwinyi aliwahi kuunda ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na kumteua Dr Salim A. Salimu kushika wadhifa huo..

✍️Vivyo hivyo Rais ally Hassan Mwinyi aliwahi kufanya kosa la namna hii na nafasi hiyo kushikwa na Hayati Augustine L. Mrema wakati kikatiba PM akiwa John Malecela..

✍️Sasa Rais Samia Suluhu Hassan naye kafanya makosa hayahaya.

Je, makosa ya mwingine yanaweza kuhalalisha jambo?

✍️Msikilize Wakili Msomi Boniface Mwambukusi akitolea ufafanuzi wa kisheria na kikatiba wa makosa haya..👇👇👇👇


Aliyoyasema kwa ufupi (quotes):

".....Ni kweli Rais kikatiba ana mamlaka na haki (right) ya ku - constitute na ku - abolish any office at anytime. Lakini haki na wajibu huu hau - extend kwenye office ambazo zimeanzishwa na katiba....."

".....Kwa mfano; ofisi ya PM, DPP, AG, Bunge au CAG ni ofisi za umma zilizoundwa na kuwekewa utaratibu na masharti maalumu kikatiba kuanzia katika uteuzi, utendaji na uwajibikaji wa watu wanaoteuliwa na kushika ofisi hizi..."

"....Mfano, Waziri Mkuu anapoteuliwa ni lazima athibitishwe na wananchi kupitia Bunge lao. Kwa maana hiyo, ni makosa na kwa kweli haiwezekani Rais atafute mtu mwingine kwa mlango wa nyuma (au wa uani) na amkasimishe majukumu ya kikatiba ya Waziri Mkuu. Hizo zitakuwa vurugu na ni kukiuka katiba.."


Ndugu Petro E. Mselewa, Pascal Mayalla JokaKuu denooJ Mag3 na wengine mna maoni yoyote?
 
Nasubiria wenye ujuzi wa Sheria waje....
Wapo watakuja tu na nimemwita Kwa makusudi ndugu Petro E. Mselewa na Pascal Mayalla kwa sababu ni wanasheria ingalau Kwa sbb pia hujitambilisha hivyo hapa jukwaani..

Lakini kikubwa zaidi ni kwa sababu Wakili Boniface Mwambukusi katika wote waliolisemea jambo hili (niliowasikia mimi), jamaa huyu yeye kaja kitofauti kidogo na kufungua koki moja ya ufahamu wangu ambayo ilikuwa imefunga na ndiyo maana nikaleta hoja hii hapa jukwaani..
 
Wapo watakuja tu na nimemwita Kwa makusudi ndugu Petro E. Mselewa na Pascal Mayalla kwa sababu ni wanasheria ingalau Kwa sbb pia hujitambilisha hivyo hapa jukwaani..

Lakini kikubwa zaidi ni kwa sababu Wakili Boniface Mwambukusi katika wote waliolisemea jambo hili (niliowasikia mimi), jamaa huyu yeye kaja kitofauti kidogo na kufungua koki moja ya ufahamu wangu ambayo ilikuwa imefunga na ndiyo maana nikaleta hoja hii hapa jukwaani..

Sioni kipya alichosema.
 
Mkuu Uzima Tele I beg to differ with my learned senior Counsel. Naendelea na msimamo na maoni yangu kuwa Mhe. Rais yuko sahihi kikatiba kuanzisha na kumteua wa kushika Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu.

Nimeitaja ( na hata Wakili Mwabukusi ameitaja) ibara ya 36 (1). Inatoa mamlaka kwa Rais kuanzisha nafasi/ofisi za kimadaraka.

Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu haipo/haikutajwa kwenye Katiba. Jana ndiyo imeanzishwa. Majukumu yake yataainishwa kwenye Hati ya Kuanzishwa kwake.

Kuanzishwa kwa Ofisi hiyo hakumaanishi kuivunja, kuivuruga, kuiingilia au kuibadili Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni Ofisi mpya inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (Ibara ya 36(1)).
 
Huyu mwabukusi aligombea ubunge akakosa nadhani amejifunza kuwa wabongo bila kupinga Domo hupati nafasi kwahivyo tumuache anaweza jijengea Kuna akapata hata ubunge/udiwani
Kuna tofauti ya "kupiga domo hovyo" na "kuusema ukweli kwa kutumia mdomo" . Boniface Mwambukusi ni msema ukweli anayetumia mdomo wake vizuri. Nyie wengine ndo wapiga domo tu...

Kuwa "diwani" au "mbunge", nafasi hizi zote zinahitaji watu wazungumzaji (wajenga hoja) wazuri ambako wewe umekuita "kupiga domo"
 
Mimi hapa naona Katiba yetu yenyewe ndio inajichanganya, hii Katiba imempa Rais mamlaka makubwa mpaka unafika wakati huwa naiona Katiba yenyewe imejiweka chini ya Rais.

Nikitazama hiyo hoja ya Adv. Mwabukusi, alipotolea mfano Rais anapoteua jina la PM lazima kwanza likathibitishwe na bunge la wananchi, hapa ni sawa na kusema wananchi kupitia wawakilishi wao bungeni ndio hutoa ridhaa kwa either kupitisha jina la PM, au kulikataa, endapo tukiwa na bunge lenye akili, sio hilo kibogoyo la Spika Tulia.

Lakini kwa upande wa pili, kwenye hoja hiyo hiyo ya Adv. Mwabukusi, utaona inapinduliwa tena na Katiba ile ile, iliyompa Rais uwezo/mamlaka ya kuteua yeyote kwenye nafasi yoyote, au niseme kuanzisha ofisi mpya, tena bila kujali kama Rais kwa kufanya hivyo, ataweza kuingilia maamuzi ya wananchi kupitia wawakilishi wao bungeni.

Hapa kwa upande wangu, ningeiona hoja ya Adv. Mwabukusi iko valid, endapo Katiba hiyo hiyo ingemuwekea Rais exception, kwamba, ni ofisi zipi anazotakiwa kuziunda kwa mamlaka yake, na zipi hatakiwi kuziunda.

Ili ijulikane wazi mipaka ya Rais kwenye kuunda ofisi mpya inaanzia wapi na kuishia wapi, lakini bahati mbaya Katiba yetu ya 1977 iliyojaa viraka haijafanya hivyo, ndio maana unaona Rais amepewa mamlaka makubwa mpaka ya kuwazunguka wananchi kwa kuteua NWM.

Kwangu hilo ni kosa la Katiba ku undermine nguvu ya maamuzi ya wananchi, sio kosa la Rais aliyeachwa atengeneze ofisi mpya bila mipaka.
 
Mkuu Uzima Tele I beg to differ with my learned senior Counsel. Naendelea na msimamo na maoni yangu kuwa Mhe. Rais yuko sahihi kikatiba kuanzisha na kumteua wa kushika Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu.

Nimeitaja ( na hata Wakili Mwabukusi ameitaja) ibara ya 36 (1). Inatoa mamlaka kwa Rais kuanzisha nafasi/ofisi za kimadaraka.

Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu haipo/haikutajwa kwenye Katiba. Jana ndiyo imeanzishwa. Majukumu yake yataainishwa kwenye Hati ya Kuanzishwa kwake.

Kuanzishwa kwa Ofisi hiyo hakumaanishi kuivunja, kuivuruga, kuiingilia au kuibadili Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni Ofisi mpya inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (Ibara ya 36(1)).
Sawa, lakini mimi bado naendelea kukubaliana na mwanasheria mwenzako huyu based on the fact kwamba;

1. Ofisi zilizoanzishwa kikatiba zinapaswa kuwa intact vilevile. Haipaswi Rais kuitumia ibara ya 36 kimakosa kwa kuingiza mtu mwingine kwa mlango wa nyuma Kwa nafasi ileile na Kwa jina la cheo kilekile. Hizi ni vurugu..!

2. Kama Rais ameona kuwa PM anahitaji mtu wa kumsaidia, na aitwe "Naibu Waziri Mkuu", apeleke amendment ya katiba..

3. La anaona shida, na ameona ktk serikali yake kuna mambo yanahitaji kuundiwa wizara, hilo liko ndani ya mamlaka yake kikatiba kuanzisha wizara na kumteua waziri ashughulikie hayo LAKINI SIO KUM - SABOTAGE PM ambaye yupo pale kikatiba...!!

Nakubaliana na Boniface Mwambukusi..
 
Mimi hapa naona Katiba yetu yenyewe ndio inajichanganya, hii Katiba imempa Rais mamlaka makubwa mpaka unafika wakati huwa naiona Katiba yenyewe imejiweka chini ya Rais.

Nikitazama hiyo hoja ya Adv. Mwabukusi, alipotolea mfano Rais anapoteua jina la PM lazima kwanza likathibitishwe na bunge la wananchi, hapa ni sawa na kusema wananchi kupitia wawakilishi wao bungeni ndio hutoa ridhaa kwa either kupitisha jina la PM, au kulikataa, endapo tukiwa na bunge lenye akili, sio hilo kibogoyo la Spika Tulia.

Lakini kwa upande wa pili, kwenye hoja hiyo hiyo ya Adv. Mwabukusi, utaona inapinduliwa tena na Katiba ile ile, iliyompa Rais uwezo/mamlaka ya kuteua yeyote kwenye nafasi yoyote, au niseme kuanzisha ofisi mpya, tena bila kujali kama Rais kwa kufanya hivyo, ataweza kuingilia maamuzi ya wananchi kupitia wawakilishi wao bungeni.

Hapa kwa upande wangu, ningeiona hoja ya Adv. Mwabukusi iko valid, endapo Katiba hiyo hiyo ingemuwekea Rais exception, kwamba, ni ofisi zipi anazotakiwa kuziunda kwa mamlaka yake, na zipi hatakiwi kuziunda.

Ili ijulikane wazi mipaka ya Rais kwenye kuunda ofisi mpya inaanzia wapi na kuishia wapi, lakini bahati mbaya Katiba yetu ya 1977 iliyojaa viraka haijafanya hivyo, ndio maana unaona Rais amepewa mamlaka makubwa mpaka ya kuwazunguka wananchi kwa kuteua NWM.
Uko sawa ndugu yangu denooJ

Kwa maelezo zaidi naomba usome post yangu #16 hapo juu nikijibu hoja ya wakili Petro E. Mselewa..

Lakini nikuulize tena swali hili;

kwamba, unadhani inawezekana Rais wa JMT akaamka kesho na kuanzisha ofisi na cheo cha Makamu wa pili wa Rais wa JMT na Kisha akateua Kwa sababu tu katiba inampa mamlaka ya kuanzisha ofisi na kumteua mtu kushika wadhifa wa ofisi hiyo?
 
Uko sawa ndugu yangu denooJ

Kwa maelezo zaidi naomba usome post yangu #16 hapo juu nikijibu hoja ya wakili Petro E. Mselewa..

Lakini nikuulize tena swali hili;

kwamba, unadhani inawezekana Rais wa JMT akaamka kesho na kuanzisha ofisi na cheo cha Makamu wa pili wa Rais wa JMT na Kisha akateua Kwa sababu tu katiba inampa mamlaka ya kuanzisha ofisi na kumteua mtu kushika wadhifa wa ofisi hiyo?
Your answer is very short and simple; YES. Tena sio kuanzisha na kuteua tu, anaweza hata kumpa hicho cheo kipya shangazi au mjomba wake.

Hii Katiba yetu imempa Rais mamlaka makubwa, mpaka unafika wakati Rais mwenyewe kwa hekima zake, anaamua kujipunguzia nguvu alizopewa, ndio maana Nyerere aliwahi kusema hii Katiba inaweza kumfanya Rais wetu akawa dikteta.

Naona umetumia neno "vurugu" kwenye maelezo yako, sawa na aliyotumia Adv. Mwabukusi, lakini lazima mtambue huo uwezo wa Rais kufanya hizo vurugu amepewa na hii Katiba mbovu inayompa mamlaka ya kutengeneza ofisi mpya bila mipaka, Rais wa JMT kwa hii Katiba tuliyonayo anaweza kufanya chochote.

Haya mambo ya kisheria, hasa argument za kisheria, mara nyingi lazima ziambatane na authorities either kuzipinga, au kuzikubali, lakini unapotaka kuzipinga tu kwa kutengeneza hoja ya kufikirika (opinion zetu), inakuwa ngumu sana.

Hapa kwa mtazamo wangu, Katiba yenyewe ndio ingetakiwa kuja na majibu ituoneshe mipaka ya majukumu ya Rais, lakini unapoona ibara hiyo ya 36 (1) ilivyompa uhuru usio na mipaka Rais, inabidi kutulia tu.

Hata hicho unachoita makosa ya Rais kutuzunguka, ingetakiwa Katiba ndio itoe majibu kama Rais ametuzunguka au yuko sawa, lakini kusema tu makosa kwa mtazamo wako inaweza kuwa sawa, hasa ukiwa na uwezo wa kujenga hoja mahakamani.

Lakini kama Katiba yenyewe ipo kimya, haijaonesha hilo unaloita kosa, naona mambo ndio yanazidi kuwa magumu kabisa kwasababu unatumia mawazo yako binafsi.
 
Back
Top Bottom