Kwanini si muumini wa Serikali Tatu...

Kwanini si muumini wa Serikali Tatu...

Zanzibar huwa kuna "Waziri wa Nchi" ........ Hapo kwenye "nchi" wanakuwa wanamaanisha nchi gani?

Kwa mfano, kuhusiana na Zanzibar, nitakuwa sahihi kama nikisema

Waziri wa Tanzania, Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora.
Waziri wa Tanzania, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum
Waziri wa Tanzania, Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi wa Umma
Waziri wa Tanzania, Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar

EMT

Tanzania ni Muungano wa nini? Nchi, majimbo, wilaya, vijiji?
Tanzania ina wanachama wangapi?

Kama hadhi ya nchi zilizoungana zilibadilika, zilichukua hadhi ipi? Majimbo? Mikoa? Wilaya au?

Tunajaribu kuhalalisha ukiini macho lakini huwa hatufiki mbali.

Serikali ya Muungano inafanya kazi za mamlaka mbili, mamlaka ya mambo ya muungano na mamlaka ya mambo yasiyo ya muungano ya Tanganyika(kama ni mshabiki wa mazingaombwe, Tanganyika isomeke Tanzania bara)

Tafuta mambo ambayo si ya muungano kwa upande wa Tanganyika baadae jaribu kuuhakiki mchango wako, mfano Uwe Tanganyika aka (Tanzania bara) badala ya Zanzibar ndio utaelewa kuwa wadanganyika tuna matatizo. Tunajifanya mbuni kuzika kichwa ardhini wakati mwili wote unaonekana. Wanaona wale tu wenye macho!
 
Mfumo wa sasa wa muungano ni wa Chama tawala kinachoongoza Serikali iliyoshindwa kutawala. Katika zama hizi, hHakuna taifa linaloweza kutawaliwa na chama na serikali kwa wakati mmoja. Ni wale tu wasioelewa ukweli huu ndio watapinga mfumo wa muungano kufanyiwa marekebisho.
China inatawaliwa na chama na serikali kwa wakati mmoja.
 
Tata mchango mzuri lakini.. Kwanza mimi ni mwamini wa Serikali moja ua mbili kamailivyo sasa au kuvunjika kwa muungano.
Kwa nini sitaki kusikia kitu kinaitwa serikali tatu?? Sababu kubwa siwezi shabikia kitu ambacho is bond to collapse in NO TIME. Kuwa na serikari tatu sio suluhu ya matatzo ya muungano hata kidogo mimi na fikiri ni kuongeza matatzo. Kwanza kutakua na dhana ya serikal ya Muungano ambayo kwa ilivyo itakua omba omba ikisubiria michango kutoka kwa nchi shirikishi pili itakua haina nguvu yoyote katika maamuzi ya dhidi ya wananchi wake hata ukiangalia vizuri utagundua kuwa rais wa tanzania ukiwa unaomba kura utatoa sera gani?? Rasilimali,Elimu,Miundo mbinu au nini?? Kwa vile mambo ya muungano ni 7 tu..ambayo yote hayana mashiko kwa uendeshaj wa nchi.ie katiba,jeshi,fedha,mambo ya nje,tume ya uchaguz,...

Hivyo ni dhairi kwamba hichi chombo kinachotengenezwa ni chombo dhaifu sana ambacho akisusa tu hata kiongoz wa nchi moja shirikish linakufa.na viongozi wa tanzania watakua wakiwa kwa vile hawana chochote zaidi ya jina. Sasa ndugu zangu kwanin tukubaliana kwenye kitu ambacho hakina nguvu ya kutusaidia au kuvunjika kwake ni raisi sana. Itakua mali ya viongozi ugomvi wao inakula kwa tanzania wakati inatakiwa kuwa other way round.inatakiwa kuwe na tanzania ambayo inaweza take control of its destiny sio kuongozwa na nchi shirikishia.

Kwa ilivyo sasa serikali tatu za Jaji Warioba is a time bomb. Sasa ni kheri tukae chin tutengeneze kitu ambacho kitadumu for ages sio kusolve immediate problems,hivyo its either we move towards kuungana vizuri zaidi kwa serikali moja au tubakie na huu mfumo wa sasa tuuboreshe kwenda kwende serikal mmoja au worse case scenario tuuvunje tuunde nchi zetu vizuri. Hizi solution tatu atleast zinaweza dumu hata kwa decade mbili.
Na mwisho naungana na MKK na nguruvi kwamba kabla ya wote lazma wananchi wapige kura. Yote ni maamuzi magumu ambayo yanaitajika kufanywa ili we cut the cost na we move on sio kutuhairishia matatizo kwa serikali tatu.
 
Last edited by a moderator:
Hoja yaMwalimu kwamba serikali moja ingeliimeza Zanzibar naona hii ni hoja potufu iliona dhamira ya kuwakaanga watu kwa mafuta yao wenyewe. Wakati ule kulikuwa nawazanzibar laki 3, na Tanganyika watu milioni tisa, ration ya 1:30, hivi sasani milioni moja Zanzibar na milioni 40 bara, sawa na ration 1:40, ardhi ndioile ile, kwa ufupi kama hoja ilikuwa valid wakati ule sioni kwa nini isiwevalid kwa sasa? Jengine kama hoja ya Mwalimu ilikuwa imejengwa kuilinda dhamirakutopoteza utamaduni na utaifa wake kwa nini hakukekemea sera ya CCM yaserikali mbili kwenda moja? Au khofu yake hii ilikuwa ya muda tu? Kama ilikuwaya muda, kitu gani alichokuwa akikisubiri mpaka hii khofu ya kuonekana serikalimoja haitoimeza Zanzibar iondoke? Jee kwa sasa hio khofu ya sayidna Mwalim,imeshakuwa neutralised na kwamba kuna mabadiliko hata hii khofu iwe haipo?


Kuhusu gharama kwa serikali ya muungano kuwa kubwa, iweje mambo saba yamuungano yawe na gharama zaidi kuliko 22 ya sasa? Kama uchangiaji Zanzibaritatakiwa ichangie nusu kwa nusu katika shughuli za uendashaji wa muungano, jeemgawo wa mapato nayo Zanzibar itafaidika kwa kupewa nusu ya mapato? Turudikwenye logic, ni vipi gharama za nchi yenye watu milioni arobaini iwe sawa nanchi ya watu milioni moja? Jee nafasi za serikali ya muungano ikiwa Zanzibaritatakiwa kuchangia nusu kwa nusu, vipi na nafasi za wafanyakazi wa serikali yamuungano zowe nusu kwa nusu? Vipi bunge la muungano nalo liwe nusu kwa nusu?Turudi tena kwenye gharama, kwa mfano uendeshaji wa jeshi la muungano, ni nanihasa atakaetumia facility za jeshi zaidi kati ya ukubwa wa karibu kilomita zamraba laki tisa na ile ya kilomita za mraba 2000? Kinachoshangaza ni malalamikomakubwa juu ya Zanzibar kuchangia nusu katika bajeti ya serikali ya muungano,lakini mgawo ni wa asilimia 4% kwa Zanzibar, hii haikubaliki kwa logic yoyote.


Maneno mengi yamezungumzwa kuhusu Mwalimu kama ndie alieamua tuwe na serikalimbili, na kwa jinsi Mwanakijiji anavyoeleza inaonekana Mzee karume ndiealietaka serikali moja lakini Mwalimu alikataa kwa sababu ya khofu yake yakuimeza Zanzibar. Hii hai make sence kabisa, tuangalia circumstantial evidencekwa upande wa Mzee Karume hasa kwa vile nae ndie mdau mkuu kama ilivyo kwaNyerere katika muungano wake alisemaje juu ya serikali moja. Kwanza hakunadocumentation yoyote inayomueleza Mzee Karume kama ni muumin wa serikali moja,au contraire zipo evidence zinazoenyesha hakuuamini hata muungano wenyewe.Azimio la Arusha, Kwa kauli ya Mzee karume ni kwamba mwisho chumbe, kauli yakeya muungano kama koti likikubana ulivue, inaonyesha imebase katika serikalimoja? Alipowarejesha wanajeshi kutoka Zanzibar kwa kuwa hakukubaliana naMwalimu katika azma yake ya kusaidia ukombozi wa nchi jirani tutasema kwambaalikuwa ni mpenzi wa serikali moja? Hata kupitia marais wote waliopita baada yaMzee Karume hakuna aliekubaliana na hoja ya serikali moja. Huwezi kulazimishaumoja kwa kudharau maoni ya wananchi, jee kuna utabiri wowote uliofanywa wakitaaluma unaofavour serikali moja hususan kwa ukuswanyaji wa maoni kutokaZanzibar?


Twende katika sehemu ya mwisho ambayo naiona ni muhimu zaidi, jee TRA, BOT,financial institutes, fiscal institutes, World Bank, IFM na taasisizilizoindependent zimewahi kufanya research ya argument ya gharama za serikalitatu na zikawafavour wanaosema uuendeshwaji wa serikali tatu ni gharama? Huwezikubase ideology ya gharama kwa kutumia mantiki matupu, kunatakiwa kuwe na backup ya hoja hasa zinazojengwa na gharama kupitia studies independent sio logicya hesabu za trilioni ngapi zitatumika wapi bila ya mchanganuo wa kisomi.
 
China inatawaliwa na chama na serikali kwa wakati mmoja.
Mkuu, Kobello,In today’s world, ‘Political Power Follows Money’; Nikuulize:• Isnt Hong Kong Part of China? • Is Communism practiced in Hong Kong? Nikianza na hoja yangu hapo juu kwamba political power follows money katika dunia ya leo, this is evident if you look at the evolution of china’s de facto federalism; Since hoja yetu ya msingi hapa ni federalism vis as vis unitary system, tutazame China kwa undani zaidi:China imegeuka kuwa a de facto federalism baada ya kutoa autonomy kwa majimbo yake na pia to guarantee Hong Kong semi independent status as an autonomous region. Nikitoka nje kidogo ya mada, nadhani utakubaliana nami kwamba, kama ilivyo kwa Hong Kong kuto practice ukomunisti ingawa ni sehemu ya China, Ujamaa haukuwa practiced in the semi autonomus island of Tanzania (Zanzibar), licha ya kwamba Katiba ya JMT (1977) katika kipindi chote cha miaka karibia 50 ya muungano, inalitambulisha Taifa la Tanzania (TANGANYIKA + ZANZIBAR) kwamba linafuata sera ya Ujamaa na kujitegemea ; Mkuu Kobello, china emerged as an economic power on a global scale only after it became a de facto federation kwa kuhamishia wide economic policy making powers kwa majimbo yake. Vinginevyo kabla ya hapo, china ilikuwa handicapped kiuchumi kwa muda mrefu by centralism (ambayo wewe na Mzee Mwanakijiji mnaipendelea Tanzania), na vile vile kutokana na unitary system that prevailed chini ya utawala wa kifalme.Kwa maana hii, Utawala wa Chama na Serikali kwa Wakati mmoja in China in only an illusion if not a fiction, kwani its not a fact;cc MTAZAMO
 
Last edited by a moderator:
Hivi kukiwa na serikali tatu mipaka ya baharini inakuaje. Pia nasikia zipo ducuments zinazoonesha Tanganyika haina Pwani, Pwani ya zenjibar ni mpaka Somalia na wengine wameenda mbali kusema watanganyika wataishia kibaha and that the union was born under such conditions hivi ni kweli?
 
hawa watu wanaoitaka Tanganika kwa sababu zao binafsi inabidi tujue idadi yao, kwani tayari tushajua watu karibi ishirini elfu walipendekeza serikali tatu kwenye tume ya katiba.vingenevyo watu watakuja na hoja zao wakitumia "watu" "watanzania" kupotosha kama inavyotokea
 
Mkuu, Kobello,In today's world, ‘Political Power Follows Money'; Nikuulize:• Isnt Hong Kong Part of China? • Is Communism practiced in Hong Kong? Nikianza na hoja yangu hapo juu kwamba political power follows money katika dunia ya leo, this is evident if you look at the evolution of china's de facto federalism; Since hoja yetu ya msingi hapa ni federalism vis as vis unitary system, tutazame China kwa undani zaidi:China imegeuka kuwa a de facto federalism baada ya kutoa autonomy kwa majimbo yake na pia to guarantee Hong Kong semi independent status as an autonomous region. Nikitoka nje kidogo ya mada, nadhani utakubaliana nami kwamba, kama ilivyo kwa Hong Kong kuto practice ukomunisti ingawa ni sehemu ya China, Ujamaa haukuwa practiced in the semi autonomus island of Tanzania (Zanzibar), licha ya kwamba Katiba ya JMT (1977) katika kipindi chote cha miaka karibia 50 ya muungano, inalitambulisha Taifa la Tanzania (TANGANYIKA + ZANZIBAR) kwamba linafuata sera ya Ujamaa na kujitegemea ; Mkuu Kobello, china emerged as an economic power on a global scale only after it became a de facto federation kwa kuhamishia wide economic policy making powers kwa majimbo yake. Vinginevyo kabla ya hapo, china ilikuwa handicapped kiuchumi kwa muda mrefu by centralism (ambayo wewe na Mzee Mwanakijiji mnaipendelea Tanzania), na vile vile kutokana na unitary system that prevailed chini ya utawala wa kifalme.Kwa maana hii, Utawala wa Chama na Serikali kwa Wakati mmoja in China in only an illusion if not a fiction, kwani its not a fact;cc MTAZAMO
MKUU Mchambuzi,
Kilichoiendeleza China wala siyo federalism, hapo utakuwa unalazimisha.

Hong kong, Macau ni sehemu ya China iliyokuwa ikitawaliwa na waingereza na wareno na hazikukombolewa 1949, kwa hiyo incorporation yake ilipotokea China ilikuwa na Market system already'

Kama hoja yako ni federalism vs. unitarism, I can debate you on that, bearing in mind that there are strong unitary economies in this world too.Kwa hiyo economic development haihusiani na federalism kwani kuna studies nyingi zinazoonyesha strengths za unitary system. Hii inategemea mambo mengi sana and not a merely constitutional Federalism.

Within a unitary system, you can have administrative federalism. Constitutional unitarism can delegate administration and come up with a better government than a constitutional federalism. The only difference here is, one system deegates power while the other makes power inherent.

Now, you need to be careful of what you are wishing for. Because Accountabilty, veto points, competition among governments,fiscal federalism and size of the government have been shown to be one of the weakest arguments for good governance.

Kama hutaanza na serikali bora, mfumo bora wa maisha unaokuwa supported by a competrent and patriotic bureaucracy, the type of federalism unayoipigania siyo tu kwamba haitakuwa bora zaidi ya unitary government, haitakuwa na maana yeyote ya kuwepo.

Sioni maana, haja wala ubora wa serikali tatu katika jambo lolote.
 
Nilichojifunza ni kuwa wengi wa wanaopiga kelele kuhusu serikali 1,2 & 3,hawaelewi wanachoongea.Ukiwauliza economic,political na social impacts ya mfumo wa serikali wanaoutaka na mapungufu ya mfumo uliopo,wengi wao wanatoa majibu ya juu juu tena ambayo waliyasikia kwa mtu fulani,wanafuata mkumbo tu.UMAKINI WA HALI YA JUU unahitajika ktk haya masuala.Tusibipu majanga,tukumbuke kuwa 'in ignorance a farmer breaks an egg to prove if an embryo is alive'
 
MKUU Mchambuzi,Kilichoiendeleza China wala siyo federalism, hapo utakuwa unalazimisha.Hong kong, Macau ni sehemu ya China iliyokuwa ikitawaliwa na waingereza na wareno na hazikukombolewa 1949, kwa hiyo incorporation yake ilipotokea China ilikuwa na Market system already'Kama hoja yako ni federalism vs. unitarism, I can debate you on that, bearing in mind that there are strong unitary economies in this world too.Kwa hiyo economic development haihusiani na federalism kwani kuna studies nyingi zinazoonyesha strengths za unitary system. Hii inategemea mambo mengi sana and not a merely constitutional Federalism.Within a unitary system, you can have administrative federalism. Constitutional unitarism can delegate administration and come up with a better government than a constitutional federalism. The only difference here is, one system deegates power while the other makes power inherent.Now, you need to be careful of what you are wishing for. Because Accountabilty, veto points, competition among governments,fiscal federalism and size of the government have been shown to be one of the weakest arguments for good governance.Kama hutaanza na serikali bora, mfumo bora wa maisha unaokuwa supported by a competrent and patriotic bureaucracy, the type of federalism unayoipigania siyo tu kwamba haitakuwa bora zaidi ya unitary government, haitakuwa na maana yeyote ya kuwepo.Sioni maana, haja wala ubora wa serikali tatu katika jambo lolote.
Kwanza, nadhani nimejibu hoja yako kuhusiana na chama na serikali kutawala kwa wakati mmoja kisiasa na kiuchumi katika dunia ya sasa, na ulichofanya hapo juu haikuwa kujibu hoja zaidi ya kuzunguka zunguka;Pili, ni muhimu ufanye utafiti kidogo juu ya federalism elements zilizopo china; Nadhani hauna taarifa za kutosha juu ya federalism in China; Tatu, kuhusiana na federalism vs unitary system na efficiencies zilizopo kisiasa na kiuchumi, sio tu kwamba I can debate you on that as well, bali pia I already did;nimejadili sana hili kwenye uzi mwingine ambao nilikualika rasmi lakini hujashiriki kuja na counter arguments; Nikipata muda, nitazijadili katika uzi huu ingawa itakuwa ni kama kujirudia kwako;Nne, wewe kusema hauoni maana na umuhimu wa serikali tatu katika muungano wa nchi mbili, kwa kweli inatia shaka juu ya uelewa wako kuhusiana mfumo wa utawala katika mahusiano ya kimataifa katika muktadha wa muungano baina ya nchi husika; pia inaonyesha kwako serikali tatu is synonymous to marais watatu, na hili ndio linawasumbua zaidi, am I right? Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
pia inaonyesha kwako serikali tatu is synonymous to marais watatu, na hili ndio linawasumbua zaidi, am I right?
Hili ndilo tatizo kubwa watu wanapoufikiria mfumo wa serikali 3. Wapotoshaji kama akina Nape Nnauye wanalitumia vema sana kuhadaa umma.

Tunaweza kuwa na rais mmoja na mawaziri wakuu wawili kwa nchi washirika.
Tatizo ambalo tume ya Warioba imekutana nalo ni kutoka upande wa ZNZ.
Wao wanataka kiongozi wao aitwe rais wakiwa wamesahau kuwa walikuwa na Sultan na waziri mkuu ambaye alikuwa kiongozi wa serikali.

Kinachowasumbua tume ni 'nationalism'' ambayo znz inayo. Znz inasema yenyewe ni nchi na lazima iwe na rais hata kama hayo ni majina tu. Hili limelazimisha tume kutumia neno hilo hilo kwa Tanganyika.

Znz inahisi itakapokuwa na waziri mkuu ile 'nationalism' ya nchi, bendera na wimbo wa taifa itaondoka.
Ndiyo maana nasisitiza kuhusu kura ya maoni, hiyo itawaondoa 'nationalism' za ajabu ajabu kwasababu wakikubali kura ya maoni lazima wakubali na yatokanayo.Hawataki kura ya maoni wanataka njia za mkato za kugawana vyeo na si gharama

Nasisitiza kurejea kwa Tanganyika kwasababu hii nationalism ni kwasababu hakuna upande wa pili. Tanganyika ingekuwepo znz ingefikiria mara mbili wana nini cha kudhani nationalism yao ni kubwa kuliko Tanganyika?

Lakini muhimu ni kuwa kama hatuwezi kuondoa tofauti ndogo kama hizi tutarithisha vizazi vyetu matatizo.
Kwanini tusipeane nafasi ya kupumua kila mmoja akienda kivyake?
Kuna haja kweli ya kuwa na muungano kwa ugomvi wa majina ya rais na si masilahi mapana ya wananchi.
Nadhani waasisi wa muungano walikuwa na akili sana bahati mbaya wameacha vizazi vya majuha, to be honest!
 
Hivi kukiwa na serikali tatu mipaka ya baharini inakuaje. Pia nasikia zipo ducuments zinazoonesha Tanganyika haina Pwani, Pwani ya zenjibar ni mpaka Somalia na wengine wameenda mbali kusema watanganyika wataishia kibaha and that the union was born under such conditions hivi ni kweli?

Kuna ukweli fulani; kwani kihistoria unaposema "Zanzibar" haumaanishi Unguja na Pemba kama wahafidhina wa Zanzibar wanataka watu tuamini. Zanzibar kama dola ilikuwa na mipaka iliyohusisha hadi pwani ya bara - maili kumi. Ndio maana wakati mwingine nimeuliza wanaoitaka Zanzibar "kwanza" wanaitaka Zanzibar ipi? maana kama wanataka Unguja na Pemba kwanza ni vizuri waseme hivyo...
 
Hili ndilo tatizo kubwa watu wanapoufikiria mfumo wa serikali 3. Wapotoshaji kama akina Nape Nnauye wanalitumia vema sana kuhadaa umma.

Tunaweza kuwa na rais mmoja na mawaziri wakuu wawili kwa nchi washirika.
Tatizo ambalo tume ya Warioba imekutana nalo ni kutoka upande wa ZNZ.
Wao wanataka kiongozi wao aitwe rais wakiwa wamesahau kuwa walikuwa na Sultan na waziri mkuu ambaye alikuwa kiongozi wa serikali.

Kinachowasumbua tume ni 'nationalism'' ambayo znz inayo. Znz inasema yenyewe ni nchi na lazima iwe na rais hata kama hayo ni majina tu. Hili limelazimisha tume kutumia neno hilo hilo kwa Tanganyika...

Nguruvi; sijui kama naweza kuita kinachoendelea Zanzibar ni "nationalism" yaani "utaifa". Hii ni kwa sababu Zanzibar haijawahi kuwa na "utaifa" wenye kuwavuta watu wote katika umoja. Hata tukiuita utaifa kwa kweli ni utaifa unaotokana na kuipinga Tanganyika zaidi kuliko kuipenda Zanzibar zaidi. Ni kwa sababu "taifa la Zanzibar" lilikuwa lina maana tofauti kabisa kwa makundi mengi ya watu visiwani humo kiasi kwamba tofauti ambazo zinaonekana zimezikwa sasa zitajitokeza wazi tena kwa nguvu zaidi baada ya taifa Zanzibar kuwa nchi nje ya Muungano.

Chukulia mfano wa Misri; wakati wa mwamko wa mapinduzi uliomuondoa Hosni Mubarak kulikuwa na imani kuwa Wamisri wote au wengi wao walikuwa kinyume na Mubarak; kwamba watu walikuwa wanapigania "Misri" na hivyo walipepea bendera za Misri na kushirikiana pamoja kuonesha "umoja wao" against the object of hatred - Hosni Mubarak. Maelfu ya watu walisimama na kushikiana mikono kuonesha umoja wao. Sasa mtu anaweza kusema kuwa walikuwa wanaonesha "utaifa" wao kwa kudai Mubarak aondoke na utawala wake uporomoke!

Well, haikuchuuka muda tukaja kugundua kuwa kumbe ndani ya waliotaka Mubarak ang'oke walikuwa Muslim Brotherhood, Wasalafi, Waliberali na hata Wasekula. Walipojaribu kuishi pamoja na kutumia ule "utaifa" wakagundua kuwa kumbe siyo wamoja! Ushindi wa MB ndio ukathibitisha hili kabisa na sasa tofauti zimekuwa kamili.

Wazanzibari ni hivyo hivyo. I would call what is happening in Zanzibar as a "Political Opportunism" veiled as "nationalism" brought by a collective sense of hatred against the Union and more categorical, against the Mainland, Tanganyika.
 
Serikali moja au serikali tatu hapo ndipo tutaweza kurekebisha kero zilizpo sasa. Lakini kama ulivyohitimisha MMM, sio lazima tuungane.

Ukweli mchungu hapa ni kuwa Waafrika kwa hulka, tabia, uwezo na desturi hatuwezi kuungana. Mara nyingi njaa (hasa umaskini) na ujinga (hasa kwa njia ya tamaa) hutufanya tuwe na maono ya kuku.

Pia kingine ni unafiki na kutokuwajibika kwetu mmoja mmoja, kama jamii na hatimaye kama mataifa huru ....ndio maana mara nyingi jumuiya/muungano/mashirikisho ya kiafrika huwa kama ngoma za kitoto. Mfano mdogo EAC iliundwa ikafa,, kisha ikaundwa tena na huenda ikafa karibuni.

Yaani kuhujumiana ni kwingi sana na ubinafsi ni vitu vilivyo ktk DNA zetu, sadly.

Mwisho ni vema kura ya maoni (bila kuchakachua) iamue hatma ya nchi hizi na mustakabali ujao na sio vikundi vya watu wachache kutumualia.
 
Nguruvi; sijui kama naweza kuita kinachoendelea Zanzibar ni "nationalism" yaani "utaifa". Hii ni kwa sababu Zanzibar haijawahi kuwa na "utaifa" wenye kuwavuta watu wote katika umoja. Hata tukiuita utaifa kwa kweli ni utaifa unaotokana na kuipinga Tanganyika zaidi kuliko kuipenda Zanzibar zaidi. Ni kwa sababu "taifa la Zanzibar" lilikuwa lina maana tofauti kabisa kwa makundi mengi ya watu visiwani humo kiasi kwamba tofauti ambazo zinaonekana zimezikwa sasa zitajitokeza wazi tena kwa nguvu zaidi baada ya taifa Zanzibar kuwa nchi nje ya Muungano.

Wazanzibari ni hivyo hivyo. I would call what is happening in Zanzibar as a "Political Opportunism" veiled as "nationalism" brought by a collective sense of hatred against the Union and more categorical, against the Mainland, Tanganyika.
well said, na hapa ndipo nasema rejeo la Tanganyika litawaacha na 'utaifa' wao huku Watanganyika wakiepuka matatizo yanayotokana na nationalism iliyojengwa katika msingi wa hatred.

Pili, tuwe na kura ya moni ili wajipime kwanza kama nje ya muungano 'nationalism' itafanya kazi.
Tanganyika nao wajitahmini kama kuna sababu za kujitoa kwa malipo ya hatred

Wakiamua kuwa nationalism itafanya wpewe fursa hiyo.
Wakisema wanashaka tutawaambia,kwanza waweke nationalism pembeni tukae tuongee tunawezaje kufanya kazi katika utaifa wenye maana lakini kila mmoja akiwa na akiba ya utaifa wake(Tanganyika au Zanzibar).
Kama hawataki basi tuvunje jahazi

Hii nationalism ya kutuletea matatizo sasa basi. Hii nationalisma ya kuvizia nafasi, vyeo na kukwepa gharama Watanganyika tumechoka. Tupewe nafasi ya kuamua mustakabali wetu tuwaache na nationalism yao.
 
well said, na hapa ndipo nasema rejeo la Tanganyika litawaacha na 'utaifa' wao huku Watanganyika wakiepuka matatizo yanayotokana na nationalism iliyojengwa katika msingi wa hatred.

Pili, tuwe na kura ya moni ili wajipime kwanza kama nje ya muungano 'nationalism' itafanya kazi.
Tanganyika nao wajitahmini kama kuna sababu za kujitoa kwa malipo ya hatred

Wakiamua kuwa nationalism itafanya wpewe fursa hiyo.
Wakisema wanashaka tutawaambia,kwanza waweke nationalism pembeni tukae tuongee tunawezaje kufanya kazi katika utaifa wenye maana lakini kila mmoja akiwa na akiba ya utaifa wake(Tanganyika au Zanzibar).
Kama hawataki basi tuvunje jahazi

Hii nationalism ya kutuletea matatizo sasa basi. Hii nationalisma ya kuvizia nafasi, vyeo na kukwepa gharama Watanganyika tumechoka. Tupewe nafasi ya kuamua mustakabali wetu tuwaache na nationalism yao.

Kama mliuzika hai utaifa wenu basi msitarajie zbr kuuzika utaifa wake,aliye uuwa utaifa wenu wadanganyika mnamjua msiwalaumu wa zbr kwa kubaki na utaifa wake,mlijitahidi kwa takribani kwa miaka 50 sasa na imekushindeni kuufuta utaifa wa wazbr,hakuna njia nyengine mtakayoweza kuifuta zbr isipokuwa muirejeshe tanganyika yenu ili maisha yasonge mbele.
 
Kama mliuzika hai utaifa wenu basi msitarajie zbr kuuzika utaifa wake,aliye uuwa utaifa wenu wadanganyika mnamjua msiwalaumu wa zbr kwa kubaki na utaifa wake,mlijitahidi kwa takribani kwa miaka 50 sasa na imekushindeni kuufuta utaifa wa wazbr,hakuna njia nyengine mtakayoweza kuifuta zbr isipokuwa muirejeshe tanganyika yenu ili maisha yasonge mbele.
Hapana unakosea kuua utaifa wa Tanganyika kulizaa utaifa wa Tanzania ambao wewe pia unao. Hakuna mzanzibar anayeweza kusimama na kukataa kuwa hana utaifa wa Tanzania.

Kinachotokea ni kuwa znz wanataka utaifa wao halafu wanataka ''utaifa wetu''. Huu utaifa wetu ni kwa ajili ya kujibanza katika matatizo. Ndio maana utasikia mkataba au serikali 3 ya ulinzi na usalama.

Utaifa wetu sote wa Tanzania kwenu ninyi ni mafao ndio maana sasa hivi utasikia wazanzibar wakiwa wamejipanga kuwa na usawa wa vyeo na ajira. Hakuna anayeongelea gharama za muungano wa shirikisho. Si kamati ya maridhiano, siyo maalim au mwingine. Hapa ndipo tunasema endapo mtataka shirikisho gharama ziwekwe mezani kwanza halafu ndio nafasi zifuate.

Kinyume cha hapo ni kubunja muungano. Watanganyika hatutakubali tena kuwa begi la gharama, miaka 50 inatosha. Sisi hatuhitaji utaifa wenu kwahiyo nafasi yetu ni nzuri sana. Ninyi mnahitaji utaifa wetu

Tunachosema ni kuwa, midhali wenzetu hamtaki tena utaifa wa Tanzania basi ule wetu wa Tanganyika urudi ili mpate nafasi ya utaifa wenu.
Lakini pia msome vizuri sana Mwanakijiji ujiridhishe kuwa mna utaifa kama inavyodhaniwa.
Adui wenu Tanganyika akishakuwa na nchi yake hamtakuwa na adui tena! umeelewa?


 
Kwanza, nadhani nimejibu hoja yako kuhusiana na chama na serikali kutawala kwa wakati mmoja kisiasa na kiuchumi katika dunia ya sasa, na ulichofanya hapo juu haikuwa kujibu hoja zaidi ya kuzunguka zunguka;Pili, ni muhimu ufanye utafiti kidogo juu ya federalism elements zilizopo china; Nadhani hauna taarifa za kutosha juu ya federalism in China; Tatu, kuhusiana na federalism vs unitary system na efficiencies zilizopo kisiasa na kiuchumi, sio tu kwamba I can debate you on that as well, bali pia I already did;nimejadili sana hili kwenye uzi mwingine ambao nilikualika rasmi lakini hujashiriki kuja na counter arguments; Nikipata muda, nitazijadili katika uzi huu ingawa itakuwa ni kama kujirudia kwako;Nne, wewe kusema hauoni maana na umuhimu wa serikali tatu katika muungano wa nchi mbili, kwa kweli inatia shaka juu ya uelewa wako kuhusiana mfumo wa utawala katika mahusiano ya kimataifa katika muktadha wa muungano baina ya nchi husika; pia inaonyesha kwako serikali tatu is synonymous to marais watatu, na hili ndio linawasumbua zaidi, am I right? Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
You are very wrong.

Ninachozungumzia mimi ni dhana kuwa federalism(constitutional) ndiyo inayoleta maendeleo.
Na kuhusu mfano wako wa china kuwa federalism ndiyo iliyoleta maendeleo, hiyo dhana ni arguably wrong, na ningependa nitoe mfano wa China vs Russia kwa sababu nchi hizi zimepitia mifumo inayofanan kwa kiasi kikubwa kwenye historia yao.... ufalme, ujamaa na ubepari (market economy) na zote zina sub-national governments and local government apart from the central government.

Tofauti ya kimaendelelo mfano kwenye miaka ya 90 inachangiwa kwa kiasi kikubwa na the power of the central government kwenye nchi mbili hizi.

China kwa kupitia communist party, ina uwezo wa kumuondoa au kummpa cheo gavana kwa kumweka Beijing kwenye central govt, tofauti na Russia ambayo enzi za Yelstin, central govt was almost powerless na katafute data za maendeleo under Deng Xiaoping na Yelstin regimes halafu uje uniambie.

Russia imeweza kuwa kwenye BRIC kutokana na Putin kutumia Gazprom na National media kuwa na nguvu kwa subnational and local governments na hii imechochea sana maendeleo.

ningeweza kwenda kirefu zaidi kama muda ungeniruhusu na ku-discuss Brazil under Lula pia kama kiashirio cha umuhimu wa recentralization through unitarist policies ... kama unataka we can go one on one, na nilikujibu mwaliko wako, ila kwa kuwa threads zako nyingi ni one-way traffic na ni ndefu mno unakuwa unachanganya sana mambo na kujumuisha vitu vingi kwa mpigo.

But unitary governments duniani zipo nyingi tu na zina-perform vizuri tu.

Sitetei serikali mbili kama zilivyo sasa na still siombei serikali tatu au majimbo yawepo Tanzania, it's a recipe for disaster.

Nina uhakika na ninachosimamia, na nimeperuzi kwa undani hii issue kwa hiyo usiwe na wasiwasi na weledi wangu.
 
I'm so proud na wachangiaji kwenye mada hizi zote zinazohusiana na serikali tatu na mfumo wa Muungano. Not only am I impressed by the level of exchanges between the members but even more by the depth and quality of the discussions. Please keep it up!
 
Mimi napinga serikali tatu - naamini kama kweli watu wanataka tuimarishe Muungano basi ni kuunda nchi moja, serikali moja mifumo mbalimbali au utengano! Kwani nani kasema ni lazima tuungane? Hatutakuwa nchi ya kwanza duniani kuvunjika na watu kuendelea kuishi pamoja na ujirani mwema.
Mzee Mwakijiji, kiukweli nakuvulia kofia!, you are very intelligent man!. Ukisoma andiko lako hili kwa juu juu utadhani wewe ni muumini wa dhati wa muungano! kwa kuweka nukuu lukuki za uoga wa Mwalimu kuhusu serikali tatu!. Hii para ya mwisho ndio inayobeba uzito wote wa andiko lako!. Naona sasa unaiendeleza ile kampeni yako ya "let Zanzibar go!" kwa kuchagizwa kuvunjwa kwa muungano in a civilized manner ili usionekane ni mchochezi, kwa kupendekeza serikali moja!, unitary government, kitu ambacho unatambua fika, kamwe Zanzibar haiwezi kukubali!, hivyo tukishinikiza serikali moja, Wanzanzibari watakataa na kuamua bora watoke!.
Kwa mujibu wa Mwalimu, ile kufikiria tuu kuuvunja muungano, ni "Uhaini!". Kuandika kuhusu namna bora ya kuuvunja muungano ni "Uchochezi!".

Tuuendeleze huu mjadala wa kichochezi, tukiwachochea watu wetu, twende kwenye muungano wa serikali moja, hatimaye tuuhaini huu muungano wetu adhimu ujifie bila kunyoosheana vidole wala kutuhumiana!.

I for Tanzania moja!, sisi ni wamoja!, nchi moja! yenye serikali 2!.

Zidumu fikra za Mwenyekiti!.
Pasco.
 
Back
Top Bottom