Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,305
- 33,766
Kuntu! Ndio maana tunasema sauti, jeuri na dharau ya znz ni kwa kuwa Tanganyika haipo. Narudia tena na tena mfano huu, wiki iliyopita kamati ya maridhiano ya Zanzibar ilitoa mapendekezo na moja kati ya hayo ni kuwepo na uraia wa kila nchi huku passport za kusafiria zikiwa Tanzania-Tanganyika na Tanzania-Zanzibar. Zanzibar ilikataa kuitwa Tanzania visiwani au sehemu ya Tanzania siku za (ilikataa vipi msome Mchambuzi huko nyuma)Nguruvi3,
..Watanganyika tutapata serikali yetu.
..Hiyo itatupa nafasi ya kuwa na chombo kinachotusemea kuhusu masuala ya muungano.
..Wazanzibari wakidai wapewe 21% ya ajira za muungano, basi atakuwepo Mtanganyika atakayeuliza kwanini iwe hivyo.
..sasa hivi Makamu wa Raisi ni Mzanzibari. Ofisi yake ndiyo inashughulika na kero za muungano. Waziri wa nchi mwenye portfolio ya muungano naye anatokea Zanzibar. Sasa unategemea wa-Tanganyika tutatendewa haki hapo??
cc Mzee Mwanakijiji, Mchambuzi
Maana nzima ya suala la hilo ni kutambua Tanganyika ipo njiani na namna pekee ya ukaribu nayo ni jina Tanzania. Kwa jinsi Wazanzibar walivyofundishwa kuwachukia Watanganyika hilo neno Tanzania ni haramu ni najisi inayohitaji tohara kubwa. Inapofikia mahali wanakubali passport yao iwe na Tanzania lipo jambo zito
Juzi Jusa Ismaili ametaka sarafu iondolewe katika muungano. Mh alikwenda aliita sarafu ya sasa haina baraka. Wakati wanachukua biioni 32 hakuna aliyesema ni pesa haramu.Dr Magoti amesimamia chuo kilichogharim bilioni 5 za muungano hakukuwa na uharamu.Tanganyika ikirudi kila mmoja atasimamia haramu na halali zake.
Tanganyika irudi ili iwepo na kura ya maoni kuamua haja ya muungano tena.
Kama ipo basi kila mmoja aje mezani na mchango, siyo jina au sheria za ajira.
Bila Tanganyika kusimamia Watanganyika tutabaki kulipa kodi, zinakusanywa na kwenda kusikotarajiwa.
Zanzibar imepata mgao mkubwa wa bajeti ya muungano kuliko Singida!
Nani wa kuwaongelea Watanganyika wa Singida na wao watalalamika wapi ikiwa wao ndio muungano? Kwanini hatutaki kutoa fursa kwa Watanganyika kupanga mipango yao kama Zanzibar?